Anaandika Jerry C. Muro
Taifa la Tanzania limeingia katika Historia ya Dunia Kufuatia Kampuni ya Barrick Gold kukubali kwa mara ya kwanza Kugawana asilimia hamsini kwa hamsini 50/50 ya Faida katika uzalishaji wa Dhahabu nje ya Asilimia 16 ya Mrahaba na Kodi ambayo taifa itapata.
Nimedadisi katika nchi mbalimbali ambazo Barrick wamefanya uwekezaji kama huu na kugundua Tanzania ndio nchi pekee ambayo imethubutu na kufanikiwa katika hili, Hongera Tanzania Hongera Rais Mzalendo Mhe, Dkt. John Pombe Magufuli katika kurekebisha kwa vitendo makosa ya watangulizi wako, huu ndio Uongozi unaoacha alama tukufu, naamini kwa sasa watangulizi wako wanafuraha kubwa ya kuona umesahihisha kwa vitendo pale walipokosea.
Muafaka Baina ya Tanzania na Barrick umewaacha "bila nguo" tena nasisitiza "bila nguo kama mnyama" wale wote waliokuwa wakisubiri Tanzania ipelekwe mahakama ya kimataifa kutokana na kuchukua hatua za kuzuia makinikia, kwangu nasema shame on you najua wamenielewa na wamesikia, Leo Tanzania imepata Shilingi Bilioni 700 kama hela tu ya kujenga uaminifu, bado nasubiria tupate kodi yetu, tupate Mrabaha wetu, kisha tugawane faida hamsini kwa hamsini.
Nimefarijika sana na kauli ya Mhe Rais, Dkt. John Pombe Magufuli ya kuwataka wawekezaji wengine wote katika Sekta ya Madini kujitafakari na kuanza kufuata uelekeo wa makubaliano kama Haya na Barrick, sasa tutaanza kuvuna neema kwenye Tanzanite, Almasi na kisha tutaingia kwenye Gesi na Mali asili zingine, Haya ni mafanikio makubwa katika kipindi cha takribani miaka miwili ya Uongozi wa Mhe Magufuli, naamini akimaliza miaka Mitano ya kwanza na ile mingine lazima Tanzania tutakuwa "Donor country"
Naomba nimalize kwa kufikisha salamu kule Nairobi, mwambieni kulikuwa na sababu ya Mungu kumuweka hai ili aje ashuhudie ukuu wa Mungu kupitia Mhe Magufuli, lile alilosema haliwezekani kwa sasa limewezekana na Hatimae Mhe Magufuli ameibuka shujaa na kinara wa kielelezo cha Rais Bora Africa anaepigania rasilimali za nchi yake, Mungu alisema Muombee sana "adui" yako aishi miaka mingi ili Ashuhudie Baraka za Mungu kwako, Hatimae maombi yetu yamejibu sasa.
Wasalamu
Jerry C. Muro
Dodoma, Tanzania
20/10/2017
jerry muro na wapumbavu wenzako, ninyi ni wehu?