Jerry Muro amehasiwa kitaaluma?

Jerry Muro amehasiwa kitaaluma?

12STONE

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2013
Posts
1,190
Reaction score
409
Huyu Kijana alikuwa Jasiri sana, Kabla ya 2010. Enzi hizo anatembea na Camera za kidukuzi pamoja na pingu. Nguvu ya Dume la Ng'ombe (Bull) ziko dhahiri popote pale utaona vurugu, machachari na umahiri wa kupigana kwake Bull wakati bado Halija HASIWA.

Mara tu likigongwa zile kede zake baaasi hata mulio hubadilika na kuwa sio wa yule Dume tuliomzoea huegeuka na kuanza kutoa mulio kaa wa Ndama au Ngo'mbe Jike.Mara moja hata Jina lake hubadilika na kuanza kuitwa MAKISAI.

JERRY MURO! JERRY MURO! JERRY MURO!

Uko Wapi? Hiyo kashfa ya kupokea Rushwa ilikuwa ya kweli? Au Wanasiasa waliwahi kuku-Mute ili usiwaletee Madhara kwenye kampeni za 2010. Ulikuwa POSITIVE / CHANYA (+) ghafla umegeuzwa na umekubaliana na hio hali ya KUHASIWA kuwa NEGATIVE / HASI (-).

Hivyo vipindi vyako vya PPRA vinakufaa kwa ajili ya tumbo lako tu. Umeacha wito wako halisi ambao ni wa KUJIHATARISHA KWA MASLAHI YA UMMA WA WATANZANIA. Umeacha, ukasahau tena umeifukia chini Talanta yako. 2015 RUDI KWENYE NAFASI YAKO.

Taifa linakuhitaji.

Nawasilisha Jamii ijue..
 
Jerry Muro ni Mhariri wa habari na kama sikosei ni mwenyekiti wa jukwaa la Wahariri.. So usitegemee kumkuta sana kwenye interactive Journalism. Pili kuna habari ziliwahi kuletwa hapa kwamba amepata kazi CNN. Ila sijui ziliishia wapi.....!

attachment.php
attachment.php


Sent from my iPhone using JamiiForums app
 
Pamoja na nia nzuri aliyokuwa nayo Jeri Muro ya kutaka kusaidia jamii hasa katika kuanika maovu kandamizi kwa jamii, baada ya yeye kupata matatizo jamii aliyokuwa anaitumikia hakuonyesha kukubali(Appreciate) na kumsaidia zaidi tuliona kejeli nyingi hata kutoka kwa wanataaluma wenzake. Hii ni dhahiri kuwa watu wanaweza kuonyesha wanakuunga mkono wakati unawatetea lakini upopata tatizo kila mtu atabeba mzigo wake.
 
Huyu Kijana alikuwa Jasiri sana,Kabla ya 2010.Enzi hizo anatembea na Camera za kidukuzi pamoja na pingu.

Nguvu ya Dume la Ng'imbe (Bull) Ziko dhahiri popote pale utaona vurugu,machachari na umahiri wa kupiga kwake Bull wakati bado Halija HASIWA.


Mara tu likigongowa zile kede zake baaasi hata mulio hubadilika na kuwa sio wa yule Dume tuliomzoea huegeuka na kuanza kutoa mulio kaa wa Ndama au Ngo'mbe Jike.Mara moja hata Jina lake hubadilika na kuanza kuitwa MAKISAI.

JERRY MURO! JERRY MURO! JERRY MURO!
Uko Wapi? Hio kashfa ya kupokea Rushwa ilikuwa ya kweli?

Au wana siasa waliwahi kuku-Mute ili usiwaletee Madhara kwenye kampeni za 2010.

Ulikuwa POSTIVE/CHANYA (+) ghafla umegeuzwa na umekubaliana na hio hali ya KUHASIWA.Kuwa NEGATIVE/HASI (-).

Hivyo vipindi vyako vya PPRA vinakufaa kwa Ajili ya tumbo lako tu.Umeacha wito wako halisi ambao ni WAKUJIHATARISHA KWA MASLAHI YA UMMA WA WATANZANIA.

Umeacha,ukasahau tena umeifukia chini Talanta yako,2015 RUDI KWENYE NAFASI YAKO.
TAIFA LINAKUHITAJI.

NAWASILISHA JAMII IJUE.

Post hii ni mwaka 1970? Mods hii ikoje?
 
alipopatwa na majaribu ya kusingiziwa na kova hadi kufukuzwa kazi tbc na baadae alishinda kesi,hukujitokeza kumsaidia kipindi kigumu alichopitia kwa sababu tu ya kuanika maovu .

sasa hivi ni mwendo wa kila mtu kuubeba msalaba wake
 
Mimi nacheka sana mapro mkulu wakisifu eti mkulu akiondoka ataacha legacy ya uhuru wa habari or freedom of press.
 
Huyo tapeli yuko yanga siku hizi. Ndio anaelekea shimoni tena..zile pingu zake za kuwatishA watu anaogopa kutembea nazo siku hizi..njaa kali!
 
ulitaka ang'olewe kucha bila ganzi?Jamaa siku hizi ni Msemaji wa klabu ya Yanga hana hamu kabisa na hizo habari zenu za Sisa
 
"WITO WA KUJIHATARISHA KWA MASLAHI YA UMMA WA WATANZANIA"

Labda uwe mgeni na huo umma wa watanzania, maana hauna ushirikiano bla bla nyingi vitendo sifuri. Mwisho ws siku ni wewe na familia yako ndo mtahangaika likitokea tatizo.
 
Mzito Kabwela
12STONE

Jerry Muro alikata tamaa mapema mno. Wakristu husema "majaribu ndo mtaji wa Imani".

Majaribu ya Jerry ndo ulikuwa mtaji wake wa kusonga mbele na kuwa na jina kubwa katika nchi na nje ya nchi. Lakini yeye kaamua kupokea mtaji na kuutia kwenye kibuyu mvunguni.

Hebu aone kazi nzuri za investigative journalist Mohammed Ali wa NTV ya kenya. ( JICHO PEVU: Makri ya Injili: http://youtu.be/mSi5UHlDOCA) .
We need him to get inspired and kick off again. Aache uoga.
 
Last edited by a moderator:
Sasa Amejiunga Na Klabu Ya Wendawazimu Hivyo Lazima Na Yeye Sasa Atakuwa Mwendawazimu Tu. Kufanya Kazi Yanga Ni Sawa Na Kukaribia Mlango Wa JEHANAM! Ameshakwisha Huyu Kijana.
 
Nilikutana nae siku moja pale Mlimani City akiwa anapaki ki-corona chake. Tukaongea kwa kifupi sana lakini kikubwa ni nia yake ya kugombea ubunge huko kwao kwa tiketi ya moja ya vyama vya ukawa.

Hebu Tuache Dharau Kwani Alichokupa Wewe Yeye Kamnyima Na Kuna Tunu Pengine Muro Anayo Na Wewe Pamoja Na Utajiri Wako Huo Wa Vipesa Vya Ngama Huna! ktk Maisha Yangu HUWA NACHUKIA MNO na SANA WATU WENYE DHARAU KAMA Wewe. Na Si Ajabu Ukawa Huna CHOCHOTE Kuanzia Akili Na Mali. Nimechukizwa Na Sentensi Yako Kuwa Nimemkuta Na Ki Korona Chake..........Umeniboa Na Umenikera Mkuu Na Hongera Zako Wewe Uliyebarikiwa Kuwa Na Magari Makuu Kuu.
 
Namkubali Jerry Muro na ukimya wakati mwingine ni jawabu.
Kila mtu na maisha yake. Akifa utalea familia yake? Huoni kama mke wake bado mbichi kabisa, au una ajenda ya siri kwa familia hii?

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Jerry Muro alikata tamaa mapema mno. Wakristu husema "majaribu ndo mtaji wa Imani".
Majaribu ya Jerry ndo ulikuwa mtaji wake wa kusonga mbele na kuwa na jina kubwa katika nchi na nje ya nchi. Lakini yeye kaamua kupokea mtaji na kuutia kwenye kibuyu mvunguni.
Hebu aone kazi nzuri za investigative journalist Mohammed Ali wa NTV ya kenya. ( JICHO PEVU: Makri ya Injili: http://youtu.be/mSi5UHlDOCA) .
We need him to get inspired and kick off again. Aache uoga.

Hakika Mohammed Ali ni risk taker..
 
Hebu Tuache Dharau Kwani Alichokupa Wewe Yeye Kamnyima Na Kuna Tunu Pengine Muro Anayo Na Wewe Pamoja Na Utajiri Wako Huo Wa Vipesa Vya Ngama Huna! ktk Maisha Yangu HUWA NACHUKIA MNO na SANA WATU WENYE DHARAU KAMA Wewe. Na Si Ajabu Ukawa Huna CHOCHOTE Kuanzia Akili Na Mali. Nimechukizwa Na Sentensi Yako Kuwa Nimemkuta Na Ki Korona Chake..........Umeniboa Na Umenikera Mkuu Na Hongera Zako Wewe Uliyebarikiwa Kuwa Na Magari Makuu Kuu.

Hata mimi kanisikitisha dharau nyingine eti ki korona, jana nimemwona Sinza lego, akiwa na harrier sasa ki korona na harrier, tuache dharau Vijana, au mnataka kila mtu awe na gari za kina Mosha.
 
Back
Top Bottom