Jengo jipya la ubalozi DC - Dola milioni 10?

Naam kwa maoni yangu kuna priorities ambazo zina umuhimu mkubwa zaidi ya kujenga ofisi ya ubalozi DC. Kwa mfano majengo ya shule zetu ambazo nyingi hayana hata hadhi ya kuitwa shule. Wanafunzi wa shule nyingi bado wanakaa chini au kuboresha drainage system ya Dar ambayo kwa sasa ni hovyo kabisa maana mvua kubwaya dakika 20 tu basi mafuriko kila kona ya jiji. Hizo bilioni 10 zingeelekezwa huko nadhani zingekuwa na matokeo mazuri sana badala ya kujenga jengo ambalo lazima gharama zake zitagubikwa na ufisadi wa hali ya juu. Tusubiri kama hizo gharama tunazoambiwa sasa hazitaongezeka mara tatu au hata zaidi jengo hilo litakapokwisha.
BAK,
Jengo lilishajengwa zamani. Limenunuliwa limeshamalizika.
 
Jamani wakuu lazima kuvalue hii jengo na thamani ya eneo husika kwa eneo husika pia, kwa hiyo pengine jengo hilo pamoja na kukarabati na thamani ya ndani yake< then location yake pia
 
..je, ununuzi wa jengo la ubalozi ulikuwepo kwenye ahadi za uchaguzi za JK?

..fedha walizonunulia hilo jengo la ubalozi wangeweza kujenga maabara na maktaba ktk shule zote za wilayani kwetu.

..binafsi naona watoto wetu kule kijijini kuwa na maabara na maktaba ni muhimu kuliko huo ubalozi.

Mkuu bila shaka wewe ndio mchumi ambaye mnapinga maswala ya Ujamaa, iweje tena leo muitake serikali ile ile mlopinga maswala ya elimu na afya kutolewa bure iwe ndio tiba nzuri ya umaskini wetu. Hizo shule na maabara mnatakiwa kujenga nyie. serikali inaacha mwanya kwenu wafanyabiashara mpate kuwekeza..

Mkuu katika dunia hii ya uwekezaji ni muhimu sana kusambaza fedha zake mahala panapolipa ili serikali itakapo jenga maabara au shule isiwe tena swala la wananchi kuuliza tutapata wapi fedha za kuendesha maabara na shule hizo na sii kutegemea tu kodi za walalahoi..
Kitu muhimu cha kujiuliza - is it a good investment?..
 
Inabidi kujenga heshima ya nchi kwa jengi zuri. Lakini hapo kuna 45% na sio 10% mtu kavuta
 
Hapo Balozi Mahalu akibahatika akishinda kesi yake lkama Zombe halafu akapelekwa kuwa Balozi wetu huko Washington DC, mtaona kazi yake kama hatalipiga mnada hilo jengo lenu!!
 
Naomba ofisi ya GAO/serikali wafanye evaluation sio kuachia tuu,States hakuna longolongo wakiwa serious ni swala la kufuata process tuu ambayo iko wazi kabisa watajua thamani halisi ya jengo...nina wasiwasi hapo kama mtu hajavuta zaidi ya 50%,housing market ya DC naijua kidogo na hiyo sehemu naijua lakini kwa 10mUSD pluuuuuuz!
 
I thought the entire free market move was to move away from government involvement in business, hii si ndiyo sababu tumebinafsisha mashirika ya umma? Sasa tunaelekea wapi?

Tunataka serikali iendelee kumiliki biashara au hatutaki?

Maana kama tunataka huko kwenda DC mbali sana, waichukue bandari tu ile wairudishe chini ya TPA, after all mkataba wenyewe ulikuwa fraudulent.

Hawa watu wanatafuta sehemu ya kula tu, hamna lolote!
 
Tusishangae baada ya ujenzi wa jengo hilo kwisha tukaambiwa kutokana na kupanda gharama za ujenzi gharama halisi za jengo hilo ni shilingi bilioni 40, msisahau yaliyotokea kwenye ujenzi wa Twin Towers maana Tanzania ndiyo inaliwa hivyo ati! na mafisadi.

Baada ya ujenzi upi Bubu?
 
I thought the entire free market move was to move away from government involvement in business, hii si ndiyo sababu tumebinafsisha mashirika ya umma? Sasa tunaelekea wapi?

Tunataka serikali iendelee kumiliki biashara au hatutaki?

Maana kama tunataka huko kwenda DC mbali sana, waichukue bandari tu ile wairudishe chini ya TPA, after all mkataba wenyewe ulikuwa fraudulent.

Hawa watu wanatafuta sehemu ya kula tu, hamna lolote!
Kumiliki nyumba haihusiani kabisa na mfumo wa biashara...hata hizo nchi Mabepari wanazo nyumba za serikali ndani na nje..
Kwa akili yako unafikiri ule ubalozi wa Marekani hapo Dar wamepanga?..
 
Kumiliki nyumba haihusiani kabisa na mfumo wa biashara...hata hizo nchi Mabepari wanazo nyumba za serikali ndani na nje..
Kwa akili yako unafikiri ule ubalozi wa Marekani hapo Dar wamepanga?..

Ubalozi wa Marekani hawajapanga, I agree.

Sijasema kitu chochote kupinga kumiliki nyumba, nimepinga serikali kufanya biashara ya nyumba, hususan baada ya kuuza nyumba zake yenyewe kwa minajili ya kutotaka kujihusisha na overheads, na kuuza mashirika yake ya umma kwa kutotaka kujihusisha na biashara.

Kwa kufuata mfano wako wa ubalozi wa Marekani, swali kwako ni, je ubalozi wa Marekani unapangisha jengo lake?
 
Jasusi,

..tatizo tumetumia billion 10 kununua hilo jengo, halafu baada ya hapo Raisi anaanza kuchanja mbuga kuomba misaada na mikopo.

..kivuko cha Kigamboni kimetumia billion 8.5. Kilombero tumetumia billion 2 za msaada toka WB[yenye makao makuu Washington DC] kununua kivuko kibovu kinachohatarisha maisha ya wananchi.

..hivi hizi pesa tungewapa wananchi wa wilaya ya Kilombero mnafikiri wangependekeza tununue hilo jengo la ubalozi huko DC?

..hivi wafadhili wa WB wanatuonaje tunapokwenda kuwalilia shinda watusaidie billioni 2 kununua kivuko, halafu tunazunguka mitaa miwili toka hapo tunanunua jengo lenye thamani ya billioni 10?
 
8D6U2065.JPG
 
Inanikumbusha mambo ya Mahalu kule Rome!! Je hawa jamaa hawajainflate hiyo gharama ya jengo lenyewe? Ni kweli value ya jengo hilo ni hizo dola millioni 10? Au ndio tumepigwa dongo tena nusu imewekwa kando ya uchaguzi wa mwaka kesho; si mnajua tena huku mambo ya BOT na EPA ndio wamekwishastukiwa!! Mkwere mwenyewe kasalimu amri kwa mafisadi kwani amekili kuwa wamemzidi akili!! Angalia hapo kwenye picha hapo juu mbele ya jengo jamaa walivyopiga PAMBA utafikri nyumbani kwao hakuna njaa; wanamtandao hao wanakula wasivyopanda na Mungu atawalaani!!
 
Jengo baya zaidi ya ghala la nafaka halafu ndio dola milioni kumi.
 
Jengo baya zaidi ya ghala la nafaka halafu ndio dola milioni kumi.
Blueray,
Location, location, location. Watu wanaofanya kazi real estate watakwambia hivyo. It is not the look of the bldg it is where it is!
 
Mkandara said:
Mkuu bila shaka wewe ndio mchumi ambaye mnapinga maswala ya Ujamaa, iweje tena leo muitake serikali ile ile mlopinga maswala ya elimu na afya kutolewa bure iwe ndio tiba nzuri ya umaskini wetu. Hizo shule na maabara mnatakiwa kujenga nyie. serikali inaacha mwanya kwenu wafanyabiashara mpate kuwekeza..

Mkuu katika dunia hii ya uwekezaji ni muhimu sana kusambaza fedha zake mahala panapolipa ili serikali itakapo jenga maabara au shule isiwe tena swala la wananchi kuuliza tutapata wapi fedha za kuendesha maabara na shule hizo na sii kutegemea tu kodi za walalahoi..
Kitu muhimu cha kujiuliza - is it a good investment?..

Mkandara,

..nilichopinga mimi ni serikali kujenga "UTITIRI" wa shule zenye viwango duni ambazo wahitimu wake hawana faida yoyote ile kwa nchi.

..India wanatamba duniani kwa kuwekeza ktk ELIMU yenye VIWANGO.

..kwanini unanibeza ninapopiga mayowe serikali yetu iwe makini zaidi ktk uwekezaji kwenye sekta ya elimu?
 
Je kuinvest kwenye real estate kwenye soko la DC ni wazo zuri? Litalipa?
ni wazo zuri sana na linalipa lakini umesahau kitu kimoja mzee je faida itakuwa ni ya walengwa ( walipa kodi kuendeleza maendeleo ya nchi} au faida itakuwa ni ya wa janja kama kawaida (mafisadi)? hili ndio jambo muhimu manake historia yetu inaonesha kuna vitu vingi vimetia hasara taifa lakini sio kwamba havina faida,faida zipo lakini zinaishia kwa wezi.
 
Wakati mwingine inasikitisha kuona the "great thinkers" wakiongea mautumbotumbo na kuendeleza lawama za kisiasa hata pale serikali inapofanya jambo zuri.

Ubalozi wa Tz marekani haupo pale kwa muda mfupi. Gharama za kupangisha ofisi na nyumba zinaongezeka kila mwaka sambamba na matumizi ya balozi zetu. Kama sisi ni great thinkers basi ni bora tukapiga mahesabu tuone uwiano wa hasara na faida za ununuzi wa jengo kabla hatujaendeleza propaganda.

Halafu haya mawazo mgando ya kudai kwamba faida haitakuwa kwa wananchi ni mawazo yanayolenga kupotosha. Kwa hiyo tuwache kuwekeza kwa sababu ya wasiwasi kwamba wananchi hawatafaidika? Je wananchi wangefaidika vipi kama hizo $10 million zingebaki mfukoni mwa serikali?
 
Last edited:
Back
Top Bottom