'Jeneza' la Simba: Fear of the unknown

'Jeneza' la Simba: Fear of the unknown

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
371,460
Reaction score
860,327
Hofu ni kitu kibaya sana.. Inaua kimwili na kiroho pia, inafubaza akili na kufisha ndoto nyingi sana.. Ukiweza kuishinda hofu umewin maisha katika nyanja nyingi sana

Ni wazi kuna upande haukufurahishwa kabisa na mafanikio ya SIMBA day jana, kuanzia mpangilio wa shughuli, mahudhurio mpaka ushindi mnono wa goli mbili dhidi ya waalikwa

Wenye kutafuta sababu wanaojifanya ni wana SIMBA wanajaribu kutengeneza dosari mbalimbali kama hizi
. Ni bonanza tu
. Tumealika timu mbovu
. SIMBA eti ilibebwa
. Na kali kuliko yote ambayo ndio imefanikiwa kuzua mjadala ni 'jeneza'
Kwamba mafanikio ya SIMBA day yametiwa dosari na hilo jeneza ! HOFU!... Nimejaribu kujiuliza dosari ni ipi kati ya mtani aliyepigwa mbili bila ama SIMBA aliyeshinda mbili bila?[emoji23]

Jeneza ni kiashiria cha umauti ama kifo, ni kiwakilishi cha huzuni na majonzi na simanzi... Msanii anapotumia jeneza kama nyenzo ya kufikisha ujumbe tarajiwa hana maana nyingine zaidi ya hizo hapo juu

Waandishi hutumia neno KUUA inapotokea timu moja imeshinda... Kwenye lahaja za lugha kuna viwakilishi vya maneno na kuna viwakilishi vya alama na kuna viwakilishi vya vikaragosi ama michoro picha

Mfungaji anapofunga goli hutumia vidole vya mikono yake kuonesha alama ya kukata shingo.. Tafsiri yake hapa ni kuua..lakini si kwa maana ile ya kuondosha uhai

Juzi kati hapa mwana masumbwi Madongo aliyepoteza pambano round ya nne alijaribu vilivyo kupeleka hofu kwa mpinzani wake kwa tambo mbalimbali na hata kutumia neno kuua.. Lakini mpinzani wake hakubabaika na kilichotokea wote tulikiona.

Mifano ni mingi lakini itoshe tu kusema 'jeneza' la SIMBA ilikuwa ni sehemu ya sanaa na kunogesha shughuli nzima..hakuna dosari iliyotiwa wala hakuna kanuni iliyovunjwa...

maxresdefault.jpg
 
Hofu ni kitu kibaya sana.. Inaua kimwili na kiroho pia, inafubaza akili na kufisha ndoto nyingi sana.. Ukiweza kuishinda hofu umewin maisha katika nyanja nyingi sana
Hili la majeneza hata ungeandika kwa herufi kubwa tupu bado halitawaingia wenye busara. Iwe Simba iwe Yanga bado kuna vitu vya kuigiza na vikaleta maana kuliko majeneza.
 
Kuogopa jeneza wakati kufa kupo ni uoga wa kijinga, hao ndio wale wanaowachukia mpaka wanaofanya biashara ya majeneza ili kujitafutia riziki zao.
 
Kuingia na jeneza jana huku wakiwa wamebeba msalaba na albino aliyefungwa fungwa kamba halafu kukaendana na maneno ya kebehi, dhihaka dhidi ya Yanga kuliharibu tamasha la Simba. Ni usanii wa kipumbavu. Mimi ni Simba lakini sijafurahishwa na hilo.
 
Hofu ni kitu kibaya sana.. Inaua kimwili na kiroho pia, inafubaza akili na kufisha ndoto nyingi sana.. Ukiweza kuishinda hofu umewin maisha katika nyanja nyingi sana
Mimi ilinihuzunisha sana, ila kwa maelezo yako kichwa kimekaa sawa.
 
Hili la majeneza hata ungeandika kwa herufi kubwa tupu bado halitawaingia wenye busara. Iwe Simba iwe Yanga bado kuna vitu vya kuigiza na vikaleta maana kuliko majeneza.
Ni mtazamo pia siwezi kukubishia
 
Hivi kwanini wahusika hawakubeba 'Jeneza' la kiislamu na kuigiza kama mashekh badala yake wakaigiza kama mazishi ya kikristo?
Kwahiyo unataka kuwapangia cha kufanya!?[emoji23]
 
Utani uwe kama utani ila ukishafika kwenye masuala kama haya unakuwa sio utani tena , mara paap jitu limeingia kwenye jeneza limeshindwa kuanmka , mtakuja kujua kama hamjui.
 
Utani uwe kama utani ila ukishafika kwenye masuala kama haya unakuwa sio utani tena , mara paap jitu limeingia kwenye jeneza limeshindwa kuanmka , mtakuja kujua kama hamjui.
maxresdefault.jpg
mqdefault.jpg
 
Back
Top Bottom