Jei Efu Bana..

TANMO

JF-Expert Member
Apr 12, 2008
11,499
11,231
...nakumbuka zamani humu tulikuwa tunaitana Mkuu, bila kujali Umri wala jinsia.. Siku hizi watu wamebadilishana majina wanaitana Hane, Babu, Switi Hati, Laazizi, asali wa moyo n.k. Hii inatufanya mabachela tujisikie wapweke (au mkiita basi mtuite wote. Yes! haki sawa kwa wote).

... nakumbuka zamani watu walikuwa hawatongozani hovyo. Ila siku hizi siyo ajabu tena kukuta watu wanapigana denda hadharani kwenye masredi,, huko tuendako usishangae unafungua sredi unakuta watu wakifanya ngono humo.

...halafu sasa, zamani Bana vidume ndiyo tulikuwa tunarusha ndoano kwa mabinti humu JeiEfu, lakini siku hizi unashangaa Binti anakutongoza wewe tena macho makavu. Wengine hii mambo tunaogopa Bana, raha ya mchuchu uhangaike naye siyo yeye ndiyo ahangaike na wewe (wewe nanihii, ukinisumbua tena nakuanzishia sredi!!!!)

... nakumbuka watu walikuwa hawajisifu humu, wanasubiri wasifiwe, lakini siku hizi mtu hata akijamba basi atakuja kujisifu jinsi alivyoacha mtafaruku kwenye daladala baada ya kuachia kijambo cha kisailensa eti!!

...nakumbuka zamani watu walikuwa hawalewi hovyo humu JeiEfu, lakini siku hizi unaweza kufungua thread ukakutana na harufu kali sana ya Kangara, Mbege, Chang'aa, Kimpumu, Mnazi, nakazalika (wahusika mnajijua, hasa wewe babu sijui nani).. Kwa kuongezea siku hizi kuna kibabu kinajifanya kinafanya ukaguzi wa vibinti vya watu (ndiyo, wewe hapo unajijua!).

... nakumbuka zamani tulikuwa hatugombanii michuchu humu, lakini siku hizi hata ukimsalimia tu mchuchu wa mtu basi unaanzishiwa sredi huku ukisakamwa kama vile umeiba hela..

... Zamani Bana wanaume tulikuwa siyo wambeya, lakini siku hizi tuna wanaume (mwanaume?) wambeya (mbeya?) humu mpaka wanasutwa (I hopu ze meseji delivadi)

....nakumbuka,,,,, aaagh TANESSSSSSSSSSSSSSSKOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO!!!!!!

Ngoja niwashe kibatari, narudi.
 
Afu ww TANMO, umekuwa mgomvi! Kuhamia magomeni ishakuwa nongwa? Na ukikataliwa na msichana mmoja ndo unakata tamaa? Kuvunjika kwa koleo....
 
Last edited by a moderator:
Afu ww TANMO, umekuwa mgomvi! Kuhamia magomeni ishakuwa nongwa? Na ukikataliwa na msichana mmoja ndo unakata tamaa? Kuvunjika kwa koleo....
 
Last edited by a moderator:
yalaah mbavu zangu sa kwani kipindi kile kilikua ni transition period so sahiz mambo mulemuleeeeeee
 
Afu ww TANMO, umekuwa mgomvi! Kuhamia magomeni ishakuwa nongwa? Na ukikataliwa na msichana mmoja ndo unakata tamaa? Kuvunjika kwa koleo....

Kausha Bana,,, mbona unanimaind wakati mwenyewe unona kabisa sijagusia ishu ya Msuba kwa sababu nakufichia soo?
 
Aaaaaaaaaa, Aisee huo msala ni wa kwako huo Mkuu.. Mimi sijamtaja mtu hapa.
Na vile Bishanga anadai ana hela ni lazima akodishe wakili kutoka Nyu Yoku..
We ndio umemtaja ......kwani huo mwandiko wa nani?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom