Jedwali la Mengi: Nani hayumo?

Bila shaka wamekupata GAME THEORY. Tuna tatizo kubwa sana Tz. Kuna watu bila aibu wanathubutu kuwatetea mafisadi! Hebu waanzishe Forum yao tujue moja: kwamba wanawatetea mafisadi kwa maslahi yao. Watuachie hii JF tupambane kwa lengo la kuirejesha nchi yetu kwenye mwelekeo sahihi. Magazeti uliyoyataja yanamilikiwa na mafisadi kama ifuatavyo: Sauti Huru (Subash Patel), Nyundo/Tazama (Lowassa), Mtanzania/Rai (Rostam Aziz), Taifa Tanzania (Nazir Karamagi). Na sasa fisadi Tanil Somaiya ameinunua Channel 10. Hebu sikilizeni upuuzi kwenye TV station hii iliyokuwa inaheshimika kabla ya kuangukia mikononi mwa mafisadi. Inasikitisha. Lakini ushindi katika vita hii ngumu dhidi ya ufisadi ni lazima!
Mbona haujataja utitili wa magazeti ya Mzee Mengi??tumekuwa wahanga wa jambo tusilolijua!

Tujenge nchi yetu iliyo dodnoka..

Hivi kwanini tusianze upya tu??
 
Wakati haya mapambano yanaanza hata mengi mwenyewe alikuwa kimya kabisa hakuna hata gazeti lake lililokuwa linaandika haya. Baadaye wakaanza kwanini no body knowz.

you nailed it.. watu wanakuja katikati ya mapambano wanafikiri tumeanza jana.. wengine tunayoyasema haya tumeyasema miaka 10 iliyopita tangu enzi za Nyenzi, Young African, Bcstimes, Jamboforums na sasa Jamii.. wakati huo wale ambao wanaitwa mashujaa leo na kusherekewa walikuwa kimya... sasa leo kwa vile wanatuunga mkono imekuwa nongwa.. tuache sasa ili tusionekane tunaungwa mkono na matajiri wa nchi hii ambao nao wanachukizwa na ufisadi.. tusikubali tunapoona watu mashuhuru wamejiunga upande wetu.. tuwakatae kwa sababu wao ni watu mashuhuri....

Ndiyo tatizo la kudandia treni kwa mbele kwani hujui limetokea wapi na huko lilikotoka limebeba nini!
 
umependa nini zaidi?habari yenyewe kuwa umelipwa na Mengi kumtetea au?

Period!

Inawezekana wewe ndio No 1 kwenye opposite pay roll such that unajaribu kutuficha kwa kusema otherwise. Haiingii akilini kwa uovu wote ambao tumeushuhudia ukifanywa na Rostam, kuanzia Richmond, Dowans ... I am sorry, kuanzia EPA (pamoja na kuwa imeibuliwa nyuma, ilitangulia. Alizikomba hizo pesa kabla) na mengine mengi. Sioni ni kwanini hujali muasia toka Iran aje kuivuruga nchi yetu kiasi viongozi wanadiriki kusema wakiguswa mafisadi nchi itatetereka. Sielewi ni kwanini Bw Gembe huoni umuhimu wa kupiga mayowe yanayowezesha kuinusuru nchi hii kutakana na mporomoko unaoendelea. Anyway, nalazimika kuheshimu mawazo yako, kwa kuwa kila mtu anahaki ya kutoa mawazo yake, hata kama kimuonekano na wengi atakuwa amepotoka.
 
Mimi siko kwenye payroll ya Mengi wala Rostam, lakini kwenye orodha ya ufisadi, ni kitendawili kujua haswa nani anayemzidi mwenzake kati ya hawa wawili. SIWATETEI!
 
Mimi siko kwenye payroll ya Mengi wala Rostam, lakini kwenye orodha ya ufisadi, ni kitendawili kujua haswa nani anayemzidi mwenzake kati ya hawa wawili. SIWATETEI!

neutrality is the position of the weak and those who don't want to offend.. (MM)
 
neutrality is the position of the weak and those who don't want to offend.. (MM)

Huyu hayupo neutral ana position yake, si unakumbuka aliishamfungia mtu huduma kwa kisingizio cha kukosa kulipia subscription?, huenda alitumwa afanye hivyo na upande mmoja. Akane
 
Back
Top Bottom