WomanOfSubstance
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 5,457
- 956
Jamani mmeshawahi kujiuliza ni kwa vipi naweza kuwa na vitu ninavyovihitaji tu badala ya kujaza kila aina ya unachoweza kuwa nacho nguo, viatu, vitabu, makaratasi, michezo ya watoto, vyombo vya nyumbani, fenicha nzee,.vifaa vya kufanyia kazi tool boxes, majembe,vifaa vya ujenzi, magari mabovu nk.
Nimekutana na watu wengi tu wakiwa na tatizo hili na wengi wanakosa hata kufurahia mandhari ya nyumba zao kwa vile kuna msongamano wa vitu hivyo na wakati mwingine kuwa ni kero badala ya furaha. Kunazo njia mbalimbali za kupunguza tatizo hili.Lakini pa kuanzia ni kujiuliza yafuatayo:
Nimekutana na watu wengi tu wakiwa na tatizo hili na wengi wanakosa hata kufurahia mandhari ya nyumba zao kwa vile kuna msongamano wa vitu hivyo na wakati mwingine kuwa ni kero badala ya furaha. Kunazo njia mbalimbali za kupunguza tatizo hili.Lakini pa kuanzia ni kujiuliza yafuatayo:
- Inakuwaje hadi unakusanya vitu ambavyo huvihitaji?
- Kitu kama hujakitumia kwa mwaka au zaidi je unakihitaji? Mfano mzuri ni makabrasha/makaratasi/documents, magazeti ya zamani.
- Unaponunua vitu ambavyo tayari ni second hand kumbuka kulikuwa na mtu alikuwa havihitaji.Je wewe ndiyo wa kusaidia kukusanya junk unless u really need it?
- Kwa wale shopaholics wenye kupenda kununua nguo, viatu n.k. je unapojaza makabati na wakati mwingine wala huzivai? Huna mtu ambaye anahitaji ukampatia?
- Kwa wenye watoto je mwanao hawezi kuvaa nguo za aliyemtangulia kuzaliwa au ni mpaka ununue mpya hata kama zipo nzuri tu zenye kuweza kutumika bado?
- Unajisikiaje pale ambapo wewe umelundika vitu ambavyo hutumii na wakati huohuo kuna watu maskini, wenye kuhitaji kama yatima, wazee, waathirika wa majanga nk.?