Chief Mtangi
Member
- May 11, 2020
- 74
- 119
Uharamia (piracy) sio jambo jipya katika sanaa nchini, lilichangia kuanguka kwa BONGO MOVIE hasa baada ya mapato kupungua leo wasanii wamebaki kulaumu foreign films, TV shows and series wakati ukweli wanaujua dhahiri.
Now jinamizi hili limeshika hatamu katika upande wa Bongo fleva, tangu digital era took the lead now piracy/uharamia umeshamiri mno, utitiri wa blogs na websites ambazo unofficially zimekuwa zikishusha kazi za wasanii bure, jambo ambalo limeleta kilio cha wasanii kulalamika mapato duni ya kazi, licha ya gharama kubwa katika kuandaa kazi zao ila zimekuwa zikiishia mikononi mwa mashabiki huku zikiwaacha wasanii mikono mitupu ama mapato kiduchu.
Japo kumekuwepo na digital platforms kadhaa kama YouTube, Spotify, Deezer, Amazon Music, iTunes music, BoomPlay, Audiomack, Mkito, Mziiki, Mdundo etc. lakini ni ukweli ni kwamba kazi nyingi zimekuwa zikiishia katika utitiri na nyomi la blogs na websites ambapo kazi zimekuwa zikishushwa (downloaded) bure, pia ni ukweli usiopingika kuwa blogs/websites hizi hazina makubaliano yeyote ya usambazaji wa kazi za wasanii, huku zile official platforms zikipokea watembeleaji wachache mno hivyo kufinya mapato ya wasanii.
Pamoja na hali hii bado wasanii, vyama vya wasanii, COSOTA, BASATA, TRA, TCRA na Wizara husika zimekaa kimya na kushindwa kuchukua hatua yeyote. Kwangu nimeshangaa kuona walengwa (wasanii) kuchukulia bila uzito wowote jambo hili huku wakilalamika mapato kiduchu. Ni kweli blogs/websites hizi zili/zimechangia kuwatambulisha wasanii baada ya kazi zao kusambaa, lakini katika dunia ya leo ambapo wasanii wapo kibiashara (music as business) sites hizo poses as parasites hazina faida yeyote hasa katika muktadha wa kibiashara
Wapo wasanii wakubwa lakini wamekuwa wakihemea mapato kiduchu ilhali ni maarufu mtaani. Swali ninalojiuliza je, wasanii wamekubaliana na uharamia huu wa kazi na jasho lao?
Now jinamizi hili limeshika hatamu katika upande wa Bongo fleva, tangu digital era took the lead now piracy/uharamia umeshamiri mno, utitiri wa blogs na websites ambazo unofficially zimekuwa zikishusha kazi za wasanii bure, jambo ambalo limeleta kilio cha wasanii kulalamika mapato duni ya kazi, licha ya gharama kubwa katika kuandaa kazi zao ila zimekuwa zikiishia mikononi mwa mashabiki huku zikiwaacha wasanii mikono mitupu ama mapato kiduchu.
Japo kumekuwepo na digital platforms kadhaa kama YouTube, Spotify, Deezer, Amazon Music, iTunes music, BoomPlay, Audiomack, Mkito, Mziiki, Mdundo etc. lakini ni ukweli ni kwamba kazi nyingi zimekuwa zikiishia katika utitiri na nyomi la blogs na websites ambapo kazi zimekuwa zikishushwa (downloaded) bure, pia ni ukweli usiopingika kuwa blogs/websites hizi hazina makubaliano yeyote ya usambazaji wa kazi za wasanii, huku zile official platforms zikipokea watembeleaji wachache mno hivyo kufinya mapato ya wasanii.
Pamoja na hali hii bado wasanii, vyama vya wasanii, COSOTA, BASATA, TRA, TCRA na Wizara husika zimekaa kimya na kushindwa kuchukua hatua yeyote. Kwangu nimeshangaa kuona walengwa (wasanii) kuchukulia bila uzito wowote jambo hili huku wakilalamika mapato kiduchu. Ni kweli blogs/websites hizi zili/zimechangia kuwatambulisha wasanii baada ya kazi zao kusambaa, lakini katika dunia ya leo ambapo wasanii wapo kibiashara (music as business) sites hizo poses as parasites hazina faida yeyote hasa katika muktadha wa kibiashara
Wapo wasanii wakubwa lakini wamekuwa wakihemea mapato kiduchu ilhali ni maarufu mtaani. Swali ninalojiuliza je, wasanii wamekubaliana na uharamia huu wa kazi na jasho lao?