Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,527
- 7,121
Ubatizo wa maji mengi ni ishara yenye maana sana kiroho. Mtu anapozamishwa ndani ya maji mengi, wakati wa kubatizwa, anaonyesha kuwa utu wake wa kale uliojaa dhambi, umekufa na kuzikwa pamoja na Kristo. Na anapotoka majini, ni ishara ya kufufuka pamoja na Yesu na kuanza maisha mapya ya utakatifu.
Mtume Paulo anasema katika
Warumi 6:4
"Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.”
Ubatizo wa maji mengi ni kitendo cha kuonyesha hadharani kwamba mtu ameacha maisha ya kale, amekubali Yesu Kristo awe Mwokozi wake, na sasa anaishi maisha mapya ya wokovu.
Mtume Paulo anasema katika
Warumi 6:4
"Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.”
Ubatizo wa maji mengi ni kitendo cha kuonyesha hadharani kwamba mtu ameacha maisha ya kale, amekubali Yesu Kristo awe Mwokozi wake, na sasa anaishi maisha mapya ya wokovu.