Je, ukimkata Nyoka mkia ataendelea kuishi?

Je, ukimkata Nyoka mkia ataendelea kuishi?

The Legacy

JF-Expert Member
Joined
Jun 1, 2022
Posts
8,217
Reaction score
16,089
Habari wadau,

Naomba kuuliza kama ukimkata nyoka mkia ataendela kuishi.

Leo baada ya mihangaiko yangu nimerudi nyumbani mapema nikaona ni vyema nishughulikie bustani yangu ya matunda na mboga mboga.

Sasa wakati nachimba mche kwa kutumia kisu ghafla akatokea nyoka mweusi na kuanza kutambaa kutoka kwenye shimo.
Kwakua nilikua na kisu mkononi nikafanikiwa kumkata mkiani kwa kutumia kisu kama inavyoonyesha hapo kwa picha.

Bahati mbaya akakimbia lakini yuko ndani ya uzio.

Sasa nawaza je ataendelea kuishi huyu mdudu

Wajuzi Naombeni maarifa yenu
 

Attachments

  • IMG_6715.jpeg
    IMG_6715.jpeg
    908 KB · Views: 13
Ila wanaume wa huo mkoa mmezidi uoga mazee..teh😜
Kuna jamaa aliwahi kupambana na panya ndani kesho yake akaja na uzi kabisa na ushahidi wa picha na akasimulia jinsi alivyo pambana usiku kucha...🤣
 
Tafuta taili lilikwisha isha matumizi yake iwe la gari ,pikipiki au baiskeli lichome humo ndani moshi na harufu yake itamkimbiza joka kutoka katika himaya yake .

Ila wakati mwingine ukimuona nyoka shika kichwa tia vibao viwili then kamtupe nje aendelee na harakati zake
 
Nyoka angekufa kama ungemkata kwenye maeneo hatari ya mwili.Mfano eneo lenye tumbo na organ nyingine muhimum

Hapo umemkata mkia tu,atanusurika na kifo but uwezo wake wa kutambaa utapungua kwa sababu ya ulemavu ulio msababishia.

Fanya uweke mazingira salama. Nyoka huyo aonekana kuwa na sumu hatari.
 
Habari wadau,

Naomba kuuliza kama ukimkata nyoka mkia ataendela kuishi.

Leo baada ya mihangaiko yangu nimerudi nyumbani mapema nikaona ni vyema nishughulikie bustani yangu ya matunda na mboga mboga.

Sasa wakati nachimba mche kwa kutumia kisu ghafla akatokea nyoka mweusi na kuanza kutambaa kutoka kwenye shimo.
Kwakua nilikua na kisu mkononi nikafanikiwa kumkata mkiani kwa kutumia kisu kama inavyoonyesha hapo kwa picha.

Bahati mbaya akakimbia lakini yuko ndani ya uzio.

Sasa nawaza je ataendelea kuishi huyu mdudu

Wajuzi Naombeni maarifa yenu
Umeleta uzi huu kwa sababu ya woga wa kumtafuta mpaka ummalize. Hakikisha unamtafuta huyo nyoka mpaka umponde kichwa chote.
 
Kama umekata sehemu anayotolea haja "cloaca" basi atakuwa amekufa vinginevyo atakuwa anateseka huko alipo ni suala la kuhakikisha unampata na kummalizia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom