Je, tutarajie kuuona msimamo wa Tanzania kuhusu vita ya Urusi ma Ukraine?

Kagosi DJ

Member
May 5, 2020
19
69
Baada ya kuwasili kwa Makamu wa Rais wa Marekani nchini Tanzania hapo jana, ajenda kadhaa zinatarajiwa kuletwa mezani.

Tanzania imekuwa haifungani na upande wowote ‘non-alignment’ kuhusu Vita inayoendelea Ukraine. Hili limejidhihirisha kwenye mfululizo wa kura zilizopigwa UNGA tangu kuanza kwa Vita hiyo, ambapo Tanzania imekuwa ikipiga kura ya kujizuia kuungana na upande wowote (abstain)

Ziara ya Makamu wa Rais wa Marekani inakuja wakati wa ushindani unaokua wa ushawishi barani Afrika kati yake na mataifa yenye nguvu duniani kama vile China na Urusi.

Moja ya mambo tunayotarajia yataibuliwa ni Tanzania kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Marekani na washirika wake huko Ukraine lakini pia kulaani kile Urusi inachoita Oparesheni ya kijeshi nchini Ukraine.

Swali ni je, Tanzania itatoa msimamo wake?
 
Zingekuwa nyakati za yule jamaa ni wazi naamini angekuwa wazi yupo pande gani, ila kwa nyakati hizi hata mwanangu huyu wa darasa la 3 anaweza akaniambia bila wasiwasi.
 
Wakati tunapata uhuru tulichukua mfumo wa uongozi wa Russia, hivyo tusitegemee kuwa Tz atamkana Russia hvy ni bora kupiga kura ya kutokuwa upande wowote mana hapo utakuwa bado umekaa kwenye line ya ushirikiano.
 
Wakati tunapata uhuru tulichukua mfumo wa uongozi wa Russia, hivyo tusitegemee kuwa Tz atamkana Russia hvy ni bora kupiga kura ya kutokuwa upande wowote mana hapo utakuwa bado umekaa kwenye line ya ushirikiano.

Unaunga mkono nchi kutofungamana na upande wowote?
 
Suala la tanzania kutofungamana na upande wowote sio uamuzi wa raisi, ni uamuzi wa nchi na mifumo yake!

Kikwete alikua pro-west, lakn bado kama nchi hatukufungamana na upande wowote.

Incase likajitokeza jambo la kutulazimu kuchagua upande, basi tutachagua east (kwa namna ya mifumo yetu ilivyo tunafungamana zaidi na east kuliko west),

Ofcoz ccm ni washirika wa mashariki, japo haisemwi wazi
 
Wakati tunapata uhuru tulichukua mfumo wa uongozi wa Russia, hivyo tusitegemee kuwa Tz atamkana Russia hvy ni bora kupiga kura ya kutokuwa upande wowote mana hapo utakuwa bado umekaa kwenye line ya ushirikiano.
Siyo kweli.

Wakati tunapata uhuru, tulichukua mfumo wa kimagharibi. Marekani ndio waliosaidia hata mazungumzo ya sisi kuungana na Zanzibar ili Zanzibar isiende upande wa Mashariki. Huo ni wakati wa utawala wa aliyekuwa Rais wa US A. F. Kennedy aliyekuwa rafiki mkubwa wa Mwalimu Nyerere. Baada ya kifo cha Kennedy, aliingia Johnson kwa kipindi kifupi kumalizia mhula uliokatishwa wa Kennedy.

Alipoingia Nixon, ndipo tukaamua kuachana na mfumo wa kimagharibi na kwenda Mashariki. Ni baada ya Nixon kutamka kuwa kwake Africa siyo priority. Marekani ikasitisha misaada yake jwa mataifa ya Africa. Mwalimu alikasirika, kwa hasiri akaamua kwenda upande wa maadui wa Marekani huku akitamka kuwa hataki kubanwa na sera za wababe wa Mashariki na Magharibi.

Msimamo wa Mwalimu ukaigharimu sana Tanzania maana hata mpango wa maendeleo uliokuwa unafadhiliwa na Ujerumani Magharibi ulifutwa.
 
Suala la tanzania kutofungamana na upande wowote sio uamuzi wa raisi, ni uamuzi wa nchi na mifumo yake!

Kikwete alikua pro-west, lakn bado kama nchi hatukufungamana na upande wowote.

Incase likajitokeza jambo la kutulazimu kuchagua upande, basi tutachagua east (kwa namna ya mifumo yetu ilivyo tunafungamana zaidi na east kuliko west),

Ofcoz ccm ni washirika wa mashariki, japo haisemwi wazi
Tukilazimika kutoa msimamo, Serikali ya Tanzania kamwe haina uwezo wa kutamka tupo Mashariki.

Nchi yetu imejaa misaada na usaidizi wa nchi za Magharibi, siyo Mashariki. Mpaka bajeti yetu ya kila mwaka inajazilizwa na nchi za Magharibi. Miradi mbalimbali ikiwemo ya afya, elimu, barabara, maji, umeme, au ni misaada au ni mikopo toka nchi za Magharibi.
 
Back
Top Bottom