Recta
JF-Expert Member
- Dec 8, 2006
- 855
- 38
Kama ningekuwa na bunge ambalo asilimia tisini ni wabunge wa chama changu, ningelivunja siku ya pili baada ya kuapishwa na kutaka nusu ya majimbo yote chama changu hakitasimamisha mgombea! Tunafanya uchaguzi mkuu mpya ili hatimaye tuwe na Bunge ambalo linaweza kusababisha yote yaliyopendekezwa humu kutekelezwa.
Wakati bunge linafanya mambo hayo mimi nitakaa tayari kutia sahihi miswada yote ya sheria zenye maslahi ya nchi.
Lakini la pili nitamtimua Mtanzania yeyote ambate atatumia neno "Hatuwezi" au "haiwezekani". Wale watakaotumia neno "ni vigumu" tutawatafutia kisiwa ambacho watafungwa hadi fikra zao zibadilike na kuanza kutafuta msamiati mwingine..msamiati ambao hauusiani na kushindwa au kutoweza au kuwa duni!
Wakati hawa wanahangaika nitafungua gereza jipya pembezoni ya mapango ya Amboni ambako Marais wa zamani, mawaziri na watumishi wa umma waliokutwa na hatia za ufisadi watatumikia kifungo chao. Gereza hilo kazi yake kubwa ya uzalishaji itakuwa kutoa maelezo ya kwanini wasitolewe kifungoni!
Mkuu umenichekesha sana. Ila naomba ufahamu tu kwamba, ukilivunja Bunge, Katiba inakufuta uRais hapohapo na uchaguzi mpya unaitishwa. Kwa mantiki hiyo, hautakuwa na nguvu za kufanya maamuzi hayo, maana nani atakaejua kama utashinda tena? [media]https://www.jamiiforums.com/images/icons/icon10.gif[/media]