Je, tumeshamsahau Wakili Mzalendo Peter Madeleka? Nini kifanyike?

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,606
29,755
Screenshot_20230810_080851_Google.jpg


Julai 17 2023 Mahakama ya Rufaa ilitoa maamuzi ya rufani iliyowasilishwa na Wakili Msomi Peter Madeleka dhidi ya plea bargain iliyoingiwa kati yake na DPP. Tangu siku hiyo ya hukumu Wakili Mzalendo, Msomi Peter Madeleka yupo rumande akisubiri mchakato wa kesi yake ya msingi uanze.

Mahakama kuonesha uchungu na maumivu makubwa ya serikali kuhusu hoja za mrufani zilizoiangusha iliamua kusimama upande wa serikali ambapo ilitoa uamuzi tata wa kuamuru kesi ya msingi ianze kusikilizwa.

Maamuzi hayo yalikuja baada mrufani kuonesha ujasiri wa kuhoji na kukosoa dhamira ya mkuu wa nchi kuingia mkataba tata baina ya serikali na DP World kwa mlango wa Dubai. Jambo hilo liliwaudhi wakuu wa serikali na ndani ya Chama Tawala hivyo kwa mwenendo wa kesi hiyo ya rufaa iliamua kuhitimishwa kwa kuhakikisha Wakili Msomi Peter Madeleka ananyamazishwa kwani kesi yake ya msingi haina dhamana.

Serikali ya awamu ya sita imejipambanua wazi namna isivyoweza kulinda rasilimali zetu kwa kuamua kuzikabidhi kwa wawekezaji milele huku mikataba inayoiingia ikiwapa ulinzi na haki za kipekee wawekezJi hao.

Mara baada ya kukamatwa Peter Madeleka, jamii ya wapenda haki imepigwa na mstuko na kuamua kukaa kimya bila kupaza sauti wala kufuatilia hatima ya wakili msomi mzalendo Peter Madeleka.


NINI KIFANYIKE
  1. Kuiburuza serikali kwenye mahakama za kikanda na kimataifa dhidi ya sheria zinazokiuka haki za binadamu ikiwemo sheria ya makosa ya mtandao na uhujumu uchumi ambayo inawanyima watuhumiwa haki ya dhamana ambayo ni ya Kikatiba
  2. Kuiomba jamii yq kimataifa kukemea mwenendo wa serikali yetu kudhibiti, kukamata na kuwatesa wakosoaji wake mbalimbali.
  3. Wakili msomi Mwabukusi naye anatafutwa kwenye mawanda ya kisheria na soon anaweza kupewa kesi ya uhaini. Dalili zipo wazi na maandalizi yanaelekea kukamilika
  4. Wanasheria wazalendo wafungue kesi (PIL) Mahakama Kuu ili sheria ya kinga kwa Spika na maafisa wa usalama wa taifa ifutwe kwa sababu haiendani na Utawala Bora, Uwajibikaji na Utii kwa Katiba na Sheria za nchi.
KImya chetu ndiyo mauti yetu
 
Adv. Madeleka kukaa rumande sio kwa sababu anataka kutoka na imeshindikana, bali ameamua kukaa huko ili kuhakikisha haki inakuwepo siku zote, na sio kutishana kwa kuwekwa ndani, hii ni kwa mujibu wa Adv. Mwabukusi, anayesimamia shauri lake.
 
Mungu amtetee.
Mungu atashuka kumtetea kupitia sisi wanadamu i.e mimi na wewe na wengine wote kwa kulielewa, kuliamini na kulifanyia kazi agizo lake hili👇👇

".....Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru...."
Luka 10:19 SUV

Twendeni kazini, tutumie mamlaka na amri aliyotupa Bwana wetu Yesu Kristo ili tuyakanyage manyoka, nge wote pamoja na kila aina ya nguvu za maadui wenye sura za binadamu lakini ni mashetani 100% kama tu alivyo baba yao ibilisi yule nyoka huku tukiwa tumehakikishiwa kuwa HAKUNA KITU KITATUDHURU..!!

(Maana yake hakuna ufalme au mamlaka ya kidunia ikiwemo ya serikali ya Tanzania iliyo kuu na juu ya mamlaka ya mbinguni ambayo sisi tu wawakilishi na wafalme wake hapa duniani/Tanzania!)

Walioko mahakamani (wakili wetu) wafanye kazi Kwa kujiamini bila woga maana wana back up kubwa yenye nguvu kupitia kiasi isiyoonekana kwa macho. MSIOGOPE!!

Na sisi ambao tumetapakaa nchini na duniani kote, tuungane na mawakili wetu kwa kuzitumia kikamilifu silaha za kiroho tulizopewa; upanga wa roho (Neno la Mungu), imani ktk uweza wa Mungu ktk Kristo Yesu, maombi, sala na dua popote pale mtu alipo na tuungane na Mch. Mbarikiwa(Mbeya) anayewapiga kisawasawa na matokeo yameshaanza kuonekana kwa macho.

Jana Jaji mmoja wa kesi ya bandari huko Mbeya wanaotumiwa na serikali kupindisha hukumu na kunyima haki watu kafiwa na mke wake mpenzi Kwa sababu ya kukataa kutubu dhambi yake..

Na bado Kwa sababu Mungu tumwabuduye sisi hadhihakiwi na kishindo chake mpaka wapige magoti peupe uwanjani na kukiri kwa ndimi zao kuwa, hakika hawa ni wana Mungu aliye mkuu sana na wa kweli..!!

HAKIKISHO LA USHINDI WETU HALINA SHAKA..
 
Leo nimesikiliza clip ya majlhojiano ya Wakili Mzalendo Mwabukusi akielezea suala la mzalendo Peter Madeleka.

Naona amejibu hoja yangu. Najua alishaona hoja zetu humu
 
Madeleka kalipoacha kazi ya Polisi alifungua kampuni yake ya UWAKILI. Halafu kumbuka Mrs Madeleka alikuwa ni Mtumishi wa IMMIGRARION Mkoa wa Arusha akiwa kitengo kinachohusiana na wahamiaji haramu.

Kesi zote ambazo Peter Madeleka alikuwa anashinda zilikuwa zinaharibiwa na mkewe ofsini. Na wahamiaji haramu wengi alikuwa anawasukuma kwa mumewe kwa ajili ya kutetewa mahakamani.

Hivyo Madeleka na mkewe walihujumu sana jeshi la Immigration Arusha hadi baadaye uongozi wa Makao Makuu ukagundua.

Madeleka yalifanya plea bargain halafu karudi kuichallenge tena kama haikuwa voluntary. Alishinda kesi na plea bargain kufutwa so kesi inaanza upya ya kwake

Unajua anachemka na hii battle haitomwendea vizuri kwani anavyoipeleka practice yake anahama from Proffesional views to political/activist view. Ni shida. Inabidi uchague kimoja
 
View attachment 2713278

Julai 17 2023 Mahakama ya Rufaa ilitoa maamuzi ya rufani iliyowasilishwa na Wakili Msomi Peter Madeleka dhidi ya plea bargain iliyoingiwa kati yake na DPP. Tangu siku hiyo ya hukumu Wakili Mzalendo, Msomi Peter Madeleka yupo rumande akisubiri mchakato wa kesi yake ya msingi uanze.

Mahakama kuonesha uchungu na maumivu makubwa ya serikali kuhusu hoja za mrufani zilizoiangusha iliamua kusimama upande wa serikali ambapo ilitoa uamuzi tata wa kuamuru kesi ya msingi ianze kusikilizwa.

Maamuzi hayo yalikuja baada mrufani kuonesha ujasiri wa kuhoji na kukosoa dhamira ya mkuu wa nchi kuingia mkataba tata baina ya serikali na DP World kwa mlango wa Dubai. Jambo hilo liliwaudhi wakuu wa serikali na ndani ya Chama Tawala hivyo kwa mwenendo wa kesi hiyo ya rufaa iliamua kuhitimishwa kwa kuhakikisha Wakili Msomi Peter Madeleka ananyamazishwa kwani kesi yake ya msingi haina dhamana.

Serikali ya awamu ya sita imejipambanua wazi namna isivyoweza kulinda rasilimali zetu kwa kuamua kuzikabidhi kwa wawekezaji milele huku mikataba inayoiingia ikiwapa ulinzi na haki za kipekee wawekezJi hao.

Mara baada ya kukamatwa Peter Madeleka, jamii ya wapenda haki imepigwa na mstuko na kuamua kukaa kimya bila kupaza sauti wala kufuatilia hatima ya wakili msomi mzalendo Peter Madeleka.


NINI KIFANYIKE
  1. Kuiburuza serikali kwenye mahakama za kikanda na kimataifa dhidi ya sheria zinazokiuka haki za binadamu ikiwemo sheria ya makosa ya mtandao na uhujumu uchumi ambayo inawanyima watuhumiwa haki ya dhamana ambayo ni ya Kikatiba
  2. Kuiomba jamii yq kimataifa kukemea mwenendo wa serikali yetu kudhibiti, kukamata na kuwatesa wakosoaji wake mbalimbali.
  3. Wakili msomi Mwabukusi naye anatafutwa kwenye mawanda ya kisheria na soon anaweza kupewa kesi ya uhaini. Dalili zipo wazi na maandalizi yanaelekea kukamilika
  4. Wanasheria wazalendo wafungue kesi (PIL) Mahakama Kuu ili sheria ya kinga kwa Spika na maafisa wa usalama wa taifa ifutwe kwa sababu haiendani na Utawala Bora, Uwajibikaji na Utii kwa Katiba na Sheria za nchi.
KImya chetu ndiyo mauti yetu

Kwa kweli Mungu atusaidie haya yafanyike maana tuendako ni kiza kinene
 
Back
Top Bottom