Je tuhahitaji tena Ze Utamu?

Status
Not open for further replies.
Itafutwe server ya utamu, kisha ifungiwe.
Hamna haja ya kuendelea kuichekea tovuti hii ya kijinga.
Waswahili wanasema ukicheka na mbwa atakufuata msikini, pia mchelea mwana kulia hulia yeye.
 
Itafutwe server ya utamu, kisha ifungiwe.
Hamna haja ya kuendelea kuichekea tovuti hii ya kijinga.
Waswahili wanasema ukicheka na mbwa atakufuata msikini, pia mchelea mwana kulia hulia yeye.

Mkuu kufungia haiwezi kuwa ufumbuzi, sababu zitaibuka nyingine nyingi tu (as long as the guys behind this are still kicking aroubd in the streets).
Watafutwe popote walipo ijumuishe waendeshaji wa moja kwa moja na wawezeshaji wengine.
They can't be that smart!
 
100% ninaafiki hawa wapuuzi wakamatwe mara moja na kupewa adhabu kali sana. Nadhani jana nilitoa hint za kutosha za kuweza kuwakamata wahusika. Nilitoa IP address, location, na muhusika alisoma chuo gani na college ID yake ilikuwa ni nini?.


Kidatu

Unafanya watu humu watoto wadogo. Hizo unazoziita wewe ni "hint" hakuna lolote. Kama kweli unawafahamu huyo/ hao wahusika basi tuma e-mail/fax/piga simu polisi uwasaidie na kazi yao hii [ya kuwatafuta ze utamu] ya kijinga; hapo utakuwa umesaidia hela yetu ya kodi isipotee bure.

Jeshi la Polisi ni lazima wawasiline na "mmoja wapo" wa host wa hiyo website ambaye kwa sasa ukiwa U.K anaonekana ni theplanet.com. Zaidi ya hilo, wewe huna namna yoyote ya kuwajua wahusika (unless ni ndugu yako/jamaa/rafiki/rafiki wa rafiki n.k) lakini sio kwa kutumia sijui ip tracer.
 
100% ninaafiki hawa wapuuzi wakamatwe mara moja na kupewa adhabu kali sana. Nadhani jana nilitoa hint za kutosha za kuweza kuwakamata wahusika. Nilitoa IP address, location, na muhusika alisoma chuo gani na college ID yake ilikuwa ni nini?.

Acha ujinga na utoto wewe! unataka nikufungulie thread alaaah
 
hiyo picha ya kikwete iko wapi? mbona mi sijaiiona? au ndo wameogopa nakuiondoa???? Naombeni link.
 
hiyo picha ya kikwete iko wapi? mbona mi sijaiiona? au ndo wameogopa nakuiondoa???? Naombeni link.

its too late! picha imeshaondolewa zamaniii!washkaji naona wameogopa
 
Maadili unayaona leo?
mbona hapa yanabadikwa mapicha machafu machafu hamuoni kama ni kinyume na maadili yatu watz......

Yo yo nasikia una hizo picha za kikwete can u please send me nione. thanks
 
Napenda kuungana na wana JF wenzangu kullani kitendo cha ZE UTAMU kubandika barua ya kumdharilisha mheshimiwa raisi wetu. Siwezi epuka kumlaumu MODERATOR /Administrator wa hi blog (kama yupo) kwa kutoibandua mapema hiyo picha kama ilibandikwa yeye akiwa hana habari. Napenda kuelimishwa, huuyu Mkuchika ana madaraka vilevile ya kufungia blogs?? Tumemsikia mara anakimbilia kufungia magazeti yakianika kashifa za VIGOGO lakini yakiaandika kashifa za walala hoi wana hana habari. Magazeti ya udaku utakuta yamepiga picha za maiti wa ajali za gari / mitumbwi lakini Mkuchika kimya!! Nina hasira naweza sema vibaya!!!
 
Meza panadol Mama mdogo maumivu ya kichwa hauanza pole pole!

Labda ninywe RED BULL nipate nguvu nyingi hata kutwanga mtu!!! Ila tu naogopa sheria kuchukua mkondo wake. Mambo mengine yanatia hasira ati, wana JF tuwe tunaombeana kheri kwa MUUMBA wetu maana hizi shughuli za kupambana na MAFISADI na Wabadhilifu wa maadili ni nzito!!!
 
Labda ninywe RED BULL nipate nguvu nyingi hata kutwanga mtu!!!

Ohhh my Goodness! Do you know the side effects of RED BULL....immunostimulants...Red Bull wil give you more than just wings....usiipende sana ....labda baba mdogo !
 

Well said FM ES. Keep it up. Hatuwezi kumdhalilisha kiongozi wa nchi. Hapa tuweke tofauti ya itikadi pembeni tuongee habari za maadili na malezi. Achana na mapungufu ya kiongozi wetu mkuu huyu, of all anahitaji heshima yake.
 
Computer scientists ,Hivi kuna njia yoyote ile ambayo inaweza kumgindua mwenye Blog kama hajajitambulisha? Kwa sababu ya uelewa wangu mdogo wa mambo ya networking naona kama vile mtu anaweza kuwa South Africa alfu aka-register kwenye blog na kusema yuko South America.

Kitendo kilichofanywa na Ze utamu sio kizuri kabisa na hakikustaili kufanywa na mtu mwenye akili timamu. Sijui jeshi la polisi litatumia njia gani kuwapata hao wamiliki.
 

Mama mdogo punguza hasira. Tatizo ni kwamba kufungia blog ni ngumu kidogo kuliko kufungia magazeti. kama unakumbuka mwanzoni Ze utamu ilikuewa inaitwa The Utamu. kwa hiyo hata akifungia ze utamu inaweza kuja kwa jina jingine. kinachotakiwa administrator wa hii blog waweke some kind of restrictions kwa watu wanao post hizi picha.
 
Jeshi la polisi kutumia resources za walipa kodi kuwasaka wamiliki wa ze Utamu na hatimaye kuwatima mabaroni au LAA itakuwa ni kutumika vibaya kwa rasilimali hizo. Nashangaa kuona kuwa tumelia sana na majambazi, tumelia sana na ndugu zetu Albino kuchunwa hatukuwahi kusikia kuwa Jeshi la polisi linashirikiana na akina so and so kuwabaini wauwaju wa Albino, mpaka Mh. alipoamuru washukiwa washukiwe na mawe mpaka kufa na alipoambiwa atoe kauli aliamua kmwaga chozi ndio serikali ikaja na utaratibu wa kuwafanya wachache watengeneze pesa kwa kuratatibu zoezi la upigaji kura za siri kuwabaini watuhumiwa. Ningekuwa Mh. Rais ningemwambia mwandishi wangu kuwa awatangazie waTz kuwa mheshimiwa Rais ansema hiyo picha ni ya kutengenezwa na hahusiki na lolote lile wala hawaombi wahusika kuomba msamaha, wala hataamuru chochombo chochote kinachotumia kodi ya wanachi kumtafuta mhusika, naawaombeni wananchi mrudi kwenye kazi zenu hasa kipindi hiki cha mwanguko wa uchumi kidunia, Asanteni sana.

Kesho hiyo story isingekuwa story tena ingekuwa imekosa maana kabisa.
 

Labda hana uhakika je? Aseme tu, zikiwekwa na nyingine je?
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…