Je tuhahitaji tena Ze Utamu?

Status
Not open for further replies.
mkuu nakufungulia thread.......
 
hizi ndio kauli ambazo hatuziitaji hapa JF zinatushia hadhi........
 
hizi ndio kauli ambazo hatuziitaji hapa JF zinatushia hadhi........

Na kauli nzuri ni ipi?.au ulitaka niseme vajj?.

Oh well kiswahili kigumu na maneno yake ni mazito compared na ukiyatamka kwa kingredha.

e.g ukisema kutongoza lina sound wierd lakini ukisema approach aah very simple.
 


Ume-sound kama upo sober kwa zaidi ya wiki......POINT!😎
 
Na kauli nzuri ni ipi?.au ulitaka niseme vajj?.

Oh well kiswahili kigumu na maneno yake ni mazito compared na ukiyatamka kwa kingredha.

e.g ukisema kutongoza lina sound wierd lakini ukisema approach aah very simple.
kuna watu wanaita matusi.....
 
Bila matusi hata wao wasingezaliwa, achana nao hao wanaolalamika.....

Thinking alike.Nilikuwa nataka kusema hivyo.

Eva na Adam walikula tunda katika bustani ya eden ambalo kila mtu ana practise na tunazidi kuelendeleza vizazi.

Mficha uchi hazai.
 
Thinking alike.Nilikuwa nataka kusema hivyo.

Eva na Adam walikula tunda katika bustani ya edena mbalo kila mtu ana practise na tunazidi kuelendeleza vizazi.

Mficha uchi hazai.
sasa hapo unatafuta mengine bi sasha........ngoja wafasiri wa kuran na bible watuambie maana ya lile tunda ni kama hio unaosemea wewe......
 
msitumie njia hii kuingilia bungeni.....

- Inaonekana kuingia bungeni kwako ndio mwanzo na mwisho wa dunia, samahani sio wote wenye hizo ndoto, ni zako tu! sisi tunatafuta hela kwanza siasa itakuja baadaye hatuna haraka nayo kama wewe!

- Na kama kuna bunge duniani linaloweza kuigiliwa kwa njia hii basi hilo sio bunge ila ni kilabu cha pombe cha walevi walevi hivi, hapa tunatota maoni yetu kulingana na ishu iliyopo mezani, na sio lazima wote tuwe na mawazo kama yako mkuu, ya kufurahia hii picha isiyo na heshima kabisa mbele ya jamii!

- Wazee wetu kama Society zetu, wengi hawajui kama Europe na US ni mabara tofauti, Nigga kwa akwaida huwa hajui kama Africa ina nchi zaidi ya 45, huwa anafikiri ni nchi moja tu, kama wazee wetu huamini kuwa mbongo yoyote anayeenda Ulaya, ni lazima akutane na wabongo wengine, huwa hawajui kwamba kuna nchi nyingi mbali mbali na miji tofauti na sio rahisi kwa wabongo walioko majuu kuonana, na sisi mabingwa wa Internent tunaofahamika na jamii hapa tumelowa maji machafu kwa sababu sio rahisi kuwashawishi wanaotusikia na Internent kwamba hatuhusiki na haya ya ajabu, tukipita sasa itkuwa huyu naye ni wa huko Internent ni fedheha kubwa sana kwa sisi wastaarabu na wapenda ukweli, hizi za picha zingekua za ukweli isingekuwa taabu,

- Narudia tena kwamba leo ni siku ya giza kwangu binafsi, sikutegema kwamba one day katika uhai wangu, kama M-Tanzania niliyelelewa kizalendo, niliyezaliwa bongo na kutahiriwa kitamaduni kijijini kwetu, na kufundishwa madhara ya utawala wa mkoloni nikiwa Primary School, nikafundishwa namna ya kujitegemea nikiwa Secondari, nikafundishwa kufanya kazi nikiwa JKT, nikaenda Ulaya na kujionea faida za kutopitia utumwa katika maisha yangu kama weusi wa US, kama wa-Surinam wa Holland, kama weusi wa Arabuni. Mwalimu akanipa elimu kuhusu utaifa wangu, akanipa nationality, akanipa ID, baada ya miaka 14 majuu siku moja nikarudi bongo nikiwa nimeelewa uzuri na utamu wa maisha yangu ya kibongo na mapungufu yake, na uzuri na mapungufu ya maisha ya majuu, bado bongo ni tambarare, lakini kwenda majuu na kurudi nyumbani na this kind of education, ya kumuweka uchi kiongozi wa taifa kama alivyofanyiwa leo ni aibu yetu wananchi wote wa Tanzania, licha ya wale tu tunaoingia kwenye mitandao.

- Kwa wale mnaoshangilia ni haki yenu, isiyokuwa haki yenu ni ku-question haki za wengine kutoshangilia, mnachotakwia kutufundisha hapa kwenye uwanja huu wa Great Thinkers ni vipi this thing inaweza kutusaidia taifa na maendeleo yake, na hasa vipi hii new ideology yenu inakwenda samba samba na masilahi yetu kitaifa.

- Kumbuka kwa shujaa huenda kilio, lakini kwa muoga siku zote huwa ni kicheko!

FMES!
 
sasa hapo unatafuta mengine bi sasha........ngoja wafasiri wa kuran na bible watuambie maana ya lile tunda ni kama hio unaosemea wewe......

Ubovu wenyewe ni kuwa, vitabu vya dini navyo saa nyingine vinastori kama za kwenye zeutamu tu....mfano hiyo stori ya Adam na Hawa au ile ya Paulo kumiminwa alipokuwa jela n.k....haya ni mambo ya kawaida na yalikuwepo toka enzi na enzi!
 
What is just happened must been cursed denounced by any Tanzanian..not because it also happen somewhere in the world that we must copy everything...,there so many ways of expresing our frustration to the encumbent....that irking picture is not one of them ..by one simple reason ..it is not our culture.........

kwa namna yeyote taswira inayoonekana pale ..kwa mila zetu sio za kiongozi ..hata wa familia sembuse wa nchi!!????..it was not a proper or accepted way of expressing concerns..and it will never ..be one ..for the betterment of the civilized future...

lakini kwa updande mwingine tunapata funzo moja kuwa lazima kuwa makini ..kwani watu wanaaza kukosa uvumilivu wa kawaida!!!..wanavuka mipaka..haijapata kutokea ..lazima wana mikakati wa mzee wakae chini na waangalie wafanye nini!
 
- Inaonekana kuingia bungeni kwako ndio mwanzo na mwisho wa dunia, samahani sio wote wenye hizo ndoto, ni zako tu! sisi tunatafuta hela kwanza siasa itakuja baadaye hatuna haraka nayo kama wewe!

FMES!
yah man......next?
 
dada belinda sasa tovuti hiyo imeshafungwa toka saa 10 mchana wa leo saa za afrika ya mashariki


wapo hewani...imebidi niingie baada ya kusikia haya na wako hewani...



si wameshaponea mara kumi kufungiwa hawa ..wanabadili IP na anwani kila mara na wanaaendelea...kuna wakati mh masha walipomgusa aliwaondoa hewani pia wakarudi na jina jipya ..

ni ngumu..kupigana na adui msiyemuona
 
lakini kwa updande mwingine tunapata funzo moja kuwa lazima kuwa makini ..kwani watu wanaaza kukosa uvumilivu wa kawaida!!!..wanavuka mipaka..haijapata kutokea ..lazima wana mikakati wa mzee wakae chini na waangalie wafanye nini!

- Mkuu PM, with all due respect as a nation tusirihusu au kushauri hizi tabia chafu kutumika katika jamii yetu kama fimbo ya ku-deal na marekebisho ya mapungufu yetu kisiasa, kwa sababu ukisha yakubali haya basi hakutakuwa na fine line tena na halitakuwa ni taifa tena, hapana tusikubali hizi tabia katika jamii yetu, sio yote ya wazungu ni mazuri.

Respect.

FMES
 


Hivi hatuna Napster?(Computer genius/Hacker)"check spelling". ambaye anaweza kucheza na huyu mtu akamuingilia mpaka kwenye PC yake akamuingizia virus?.
 
Haya malalamiko pelekeni tume ya Mawasiliano na kwa ISP wote ndani ya Tanzania waiblock ili isiwe accessible nchini.
Na kama umechafuliwa au ndugu yako amechafuliwa wasiliana na Host wao ukiambatanisha na ushahidi
Unachoandika hapo juu Icadon ndicho kilichofanyika. ISP wote Tanzania wamekuwa ordered wai-block Ze Uchungu na ikatekelezwa HARAKA SANA. Lakini nadhani wamekosea bado, kwa anayeelewa namaanisha nini anajua kuwa ni kazi bure, Proxy servers zipo, mwenye dhamira ya kutembelea tovuti ile anaipata uzuuri kabisa. Halafu, ni kosa KUBWA (kisheria)! Wrong decision I may say. Kwa wale walio nje wanaipata vema hivyo wanaweza kusambaza nakala za yanayoongelewa mle kwa njia ya barua pepe ama vinginevyo.

dada belinda sasa tovuti hiyo imeshafungwa toka saa 10 mchana wa leo saa za afrika ya mashariki
Shy,

Nadhani ungekaa kimya UMEKOSEA!
 
Wewe nae....
....siku hizi JF kuna vi thread vya ajabu ajabu vya kujikomba komba.....

......hebu tuletee kidhibitisho cha kuchafuliwa raisi

Jamani kwani ze utamu huijui??? go and see urself!!! Those who did it should be prosecuted hata kama ni uigaji basi hapo pamepita kikomo!! niuozo wa mawazo na ufinyu wa kufikiria. Hiyo aliyefanya hivyo je angekuwa ni yeye kafanywa vile angejisikiaje? au je angekuwa ni baba yake!!
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…