Je somo moja la faa kumkosesha mtu cheti cha ualimu hata kama sio somo la kufundishia?

Jan 28, 2024
13
9
Mimi kama mdau wa jamii forum nimeona hoja na kero nyingi zikipatiwa ufumbuzi mbali mbali hivyo naomba kuwasilisha hoja yangu ya msingi hapa!

Ni kuhusu wizara ya elimu hapa nchini ninaomba waliangalie hili kwa umakini!

Mimi ni miongoni mwa watu waliohitimu mafunzo ya ualimu katika chuo cha ualimu Tabora mwaka 2015 lakini ndani ya mwaka huo na miaka mingine yote vyuo vya ualimu vyote vilikuwa chini ya NECTA yani baraza la mitihani lakini badae waliofuata waliwekwa chini ya NACTE na ndani ya mwaka huo kuliambatana na mabadliko mengi sana ikiwemo ya BRN nakumbuka tuko likizo ya Mwezi wa kumi na mbili tunapigiwa simu tukiwa majimbani kuwa vyuo vikifunguliwa kutakuwa na mitihani ya BRN

Ila hoja ya msingi hapa ni kwamba navoelewa mimi vyuo vya ualimu kwa kipindi hicho vilikuwa chini ya NECTA manake mitihani yetu yote ilisahishwa na baraza la mitihani yani hakuna utaofauti na shule za msingi na secondary yani O-levels na A-levels kwani wale mtu anapopata alama zile kuanzia alama A,B,C,D na F matokeo yake yanaoneshwa na alama alizozipata lakini wale wa O-level na A-levels na shule za msingi huwa wanapewa vyeti vyao hata kama kapata mfano alama F mbili anapata cheti lakini kwa vyuo vya ualimu kwa kipindi kile mtu hapewi cheti na unakuta amefeli somo moja tena basi sio masomo ya kufundishia lakini hapewi cheti chake.

Kwanini mtu huyu asipewe cheti kikionesha kuwa amefaulu masomo haya na haya na amefeli somo hili moja ili hicho cheti kimsadie mtaani kutafuta kazi hata shule za binafsi kwani serikali haiwez kuajiri wahitimu wote lakini kitendo cha kuwanyima vyeti kwa kufeli somo moja mimi kwangu naona sio haki sidhani kama somo moja linaweza kumfanya mtu asiwe na ufanisi na sio kweli kwamba kwa miaka miwili yote aliyokaa chuoni na kusoma mtu huyo hajatoka na chochote kisa somo Moja!

Kwangu sio haki mimi nilijaribu kuwasilisha maoni yangu kwa wizara husika bila mafanikio tena kipindi hiko mama Ndalichako ndo alikuwa waziri wa elimu nilipompigia simu alinijibu vibaya nikajaribu kumtumia ambae sasa ni waziri wa Kilimo mheshimiwa Hussein Bashe nae aka kaa kimya sikukata tamaa nikaamua kutuma maoni yangu ikulu bahati nzuri ikulu walinijibu barua pepe yangu wakanielekeza kupeleka maoni yangu kwa aliyekuwa katibu mkuu wa wizara ya elimu mheshimiwa Leonard Akwilapo alinitumia barua pepe akiniomba niandike maoni yangu kwa lugha ya kiswahili ili apate kunielewa vizuri nikafanya ivyo lakini mpka leo hajawahi kunijibu toka mwaka 2016 mpka leo


kwahiyo unakuta vijana wengi ambao walikuwa na tatizo kama langu au wenye tatizo kama langu! Wako mtaani wanakosa ajira kwasababu ya somo moja kuwaangusha mimi siamini na sitoamini kwamba somo moja linaweza kumfanya mtu asiwe na ufanisi! Sio kweli hivyo ninaomba kwa kuwa mabadiliko yale yalijua ghafla tunaomba waziri wa elimu aliangalie hili kwa jicho la tatu ili nasisi tupate vyeti vyetu ili vitusaidie kufanya maisha mengine huku mtaani!

Mimi kwa upande wangu nimeshajitolea mpka kuwasaidia au kufundisha shule za serikali bila malipo hivyo naomba jamii forum mkombozi wa fikra za jamii iweze kufikisha hoja hizi kwa wizara husika
 
Hakuna chuo chochote kila ambacho utapata cheti bila ya kufaulu course zote hakuna.

Pili, kuhusu Core Course ndio uwalimu wenyewe, uwalimu Pedagogical knowledge, classroom management nk sio some la kufundishia tu kama unavyojaribu kusema, fault course zote no excuse.
 
Pole Sana Ila nadhani huo mfumo ni wa chuo kuwa unahitaji ufaulu masomo yote ili upate cheti.

Hii pia ipo hadi VETA ukifeli somo moja haupati cheti.

Pole Sana unaweza kutumia njia nyingine kufikia malengo yako ya Elimu.

Ukiwa chuo kikuu ukafika mwaka wa tatu ikotokea umeacha chuo , utapewa higher diploma kwa vyuo vyenye mfumo wa nta level.
 
Mkuu jitahidi Ukafanye Sup somo hilo...
Hakuna mbadala wa shortcut...

Madaktari baada ya kupata Degree bado hawezi kutibu japo ana cheti cha kuwa na Degree (MD) mpaka afaulu Mitihani Mitatu "Siku hizi" Wakiwa Internship..

Pre intern (Kabla hajaanza kufanya Intern), Intern exam (Kipindi akiwa anafanya Intern) na Post Intern akimaliza Intern..

Ukifeli hapo hakuna Cha msamalia Mtume Ni lazima urudie..

Hata wanasheria hivyo hivyo..

Sasa kwanini wewe unataka Shortcut wakati wewe ni mwalimu unayefundisha watu waje wawe Madaktari,Wanasheria na Maproffesor kama unalalamika Wewe Unataka tutilie shaka Elimu yako ya nyuma..
 
Mkuu pole sana kwa yaliyo kukuta!
Lakini bado una tatizo la uandishi mbovu unatakiwa kulifanyia kazi mapema!

Tukirudi kwenye hoja yako!
Je hilo simo ulilofeli lina uzito gani kwenye kufundisha?

Ni somo la nguzo(core subject)? Kwani taratibu za kutakiwa kufaulu masomo yote mliopewa zilianzia kwenu?

Hakuna nafasi ya kulirudia somo kama mtu amefeli?
 
No shida shida sio kuwa nataka short cut hapana ila hoja yangu ni kwmba kwanini mabadiliko yanaletwa ghafla ghafla hivyo?
Lakini pia vyuo vya ualimu vilikuwa chini ya NECTA it means mitihani ilikuwa inasahishwa kama wanavyosahishiwa O-levels na A-levels! Labda pengine ufahamu wang kuhus sera ya elimu ya vyuo vya ualimu kwa kipindi hicho sina ila ni namna ambavyo nilikuwa najaribu kuwaza
 
yani umessap unataka ugraduate ebu kuwa serious basi kiongozi ushauri wangu kama umehitimu form six tumia cheti cha form six kupambana mtaani au rudi TTC ukasapue sawa
Mfumo wetu wa elimu una matobo mengi Sana Tena sana. Na hii hupelekea kuzalisha wahitimu wasio na uelewa wa mambo mengi. Hii yote husababishwa na wanasiasa wajinga tulio nao wanatokana na mfumo huu huu wa elimu yetu . Za kuwekeana Sheria ngumu sana katika elimu yetu.

Na hii ndo huzalisha wajinga wengi wenye vyeti lakin kichwa hamna kitu Kwa kusoma Kwa kukariri..
 
Huyu atafute fani nyingine tu...kwenye ualimu atatuharibia watoto.
Nashukuru ndugu yangu lakini jitahidi kuwa na lugha yenye stara ndani yake hunijui nilivyo then unasema kuwa nitawaharibia watoto wenuits not fair! Kwa taarifa yako ndugu yangu nimewafundisha watoto wengi sana na huwa wananipa feed back nzuri kwa masomo ambayo niliwafundisha na wamekuwa na mwendelezo mzuri hata huko sekondari so wakati mwingine kabla hujamshutumu mtu au kumtolea maneno yasiyo na busara ndani yake jaribu kuuliza background ya mtu! Hatuwezi kuwa sawa hata siku moja na kila mtu ana namna yake ya kutenda au kufanya jambo au kufikiria! Ila asante pia ni moja ya challenge napokea! Tuko pamoja!
 
Mfumo wetu wa elimu una matobo mengi Sana Tena sana. Na hii hupelekea kuzalisha wahitimu wasio na uelewa wa mambo mengi. Hii yote husababishwa na wanasiasa wajinga tulio nao wanatokana na mfumo huu huu wa elimu yetu . Za kuwekeana Sheria ngumu sana katika elimu yetu.

Na hii ndo huzalisha wajinga wengi wenye vyeti lakin kichwa hamna kitu Kwa kusoma Kwa kukariri..
True! Pia wanasiasa wanadhani kuwa wao kwa kuwa wengi wana umri mkubwa wao ndo wenye mawazo chanya vijana wenye elimu zao hawana fikra chanya ila sio mbaya tutafika tu!
 
Back
Top Bottom