Habari za pilika waungwana? Naombeni busara zenu wajameni! Mpenzi amenitia jeraha la moyo? Mi nilikuwa na demu, tulipendana sana na ukweli nilimuamini sana na nikawa namtimizia kila kilichokuwa ndani ya uwezo wangu. Yeye aliishi na wazazi wake nami nikiwa kwangu nimepanga. Siku moja nilipata safari ya kikazi kwenda mkoa mwingine. Asubuhi moja nikiwa huko kama saa 1:30 nilimpigia cm kumjulia hali. Sikuamini masikio yangu, kwani nilipokelewa na matusi mazito ya nguoni kutoka kwa mwanaume akiniambia ati nikome kumpigia mke wa mtu! Sauti nilíitambua vema sana, ni ya mfanyakazi mwenzangu pale kazini. Kukwepa shari, nikaikata.Siku 4 baadaye demu akanipigia akilaumu ati mbona simpigii! Nilimsimulia matusi yale na nikamwambia simtaki tena aendelee na huyo "mume" wake. Juzi tena kaja kwangu ati anataka tena penzi! Nilipouliza kuhusu mwanaume wake aliyenitukana, hasemi ukweli. Nilimfukuza. Je, wanaJf, nilikosea kuamua hivyo.