Father of All
JF-Expert Member
- May 30, 2026
- 265
- 491
Kwa sasa, hakuna mtu mwenye kusikika na kusababisha utata kama mwana wa mfalme Muhoozi Keinerugaba. Anakamata wale wanaopinga. Anafungia vyombo vya habari. Anatoa matamshi kana kwamba yeye ndiye rais. Je, hii nguvu kaipata wapi? Je, kuna kitu anakijua kuhusiana na afya ya baba yake ambacho wengi hawajui? Je, baba yake ameamua kumpa ukanda na kupima maji tayari kwa kumuachia mamlaka? Maswali ni mengi kuliko majibu.