Je, Mjamzito kupata hedhi kuna tatizo?

Je, Mjamzito kupata hedhi kuna tatizo?

Inawezekana sana. Kuna dada mpaka mimba ina miezi 7 alikua anaingia period kama kawaida. Kilichomshitua ni tumbo kukua kwa kasi. Mwanzo alijua ni mihogo na chips ndo vinajaza tumbo.

Kwenda hosptal kumbe ni mjamzito
 
leo nimeandamana na mke wangu kule kituoni cha kliniki na tumepata mafunzo na maelezo ambayo kwa kijuujuu ningetaka kushiriki na wadada wote. uwe umetunga mimba ama bado maana ni vyema kuwa na ujuzi ili ujapo wakati ukajipata ushatunga na mambo haya yakakufika usiwe mashakani.

kwanza, kuna hili aliloliita kwa kimombo "vaginal bleeding"kwa kawaida, huwa linatokea kwa muda wa kama juma moja kabla ya tarehe kamili au muda kamili wa hedhi..hili si la hatari ila bado ni vyema upate ushauri kutoka kwa mtaalamu. kisababishi kikuu huwa ule utungaji wa mimba kwani wakati huo damu nyingi sana huelekea kule ili kurinda ujauzito na hivyo ukajipata wakati mwingine damu inatoka.

Fahamu kuwa ile si hedhi na kwa kuitofautisha huwa ni nyepesi sana kama na huwa ya siku au siku mbili..mengine yanayosababisha hili ni alichokiita "pap smear"(hilo chunguza mwenyewe) pia kuna "vaginal examination" tendo la unyumba pia huchangia hivyo ni vyema ujue staili zipi hupendekezwa wakati wa ujauzito.

visababu hatari vya jambo hili kutokea ni kama "infections"hapa mwanadada unafaa kuwa mwenye usafi sana maana kama nilivyofahamu infections husababishwa na vichembechembe vya uchafu utokao kunako na kuwa kama "yeast"

lingine ni "placental problems"ambapo unapaswa kumtembelea mtaalamu..kama una historia ya kuavya mimba yakupasa uwe makini manake hili pia huwa na mchango mkubwa..la hatari kabisa ni hili lililoitwa "ectopic pregnancy"hili linamaanisha mimba haijatunga katika sehemu ndani ya nyungu la mtoto bali kwingineko hasa kwenye ile mifereji ya fallopian tubes..ikiwa hukuchunguza ukajua mapema yaweza fikia hata kifo manake ile sehemu ndogo ukizingatia mimba inaendelea kukua.

wataalamu wanapendekeza mambo ya kupimwa yafanywe muda baada ya muda ili kujua hali yako kwa ajili ya utunzaji wa mimba ipasavyo...wadada wenye matatizo haya wana ruhusa ya kwenda moja kwa moja hadi kwenye chumba cha emergency iwapo utamkosa daktari wako ama awe anamhudumia mgonjwa mwingine.....

asanteni
 
Inawezekana sana. Kuna dada mpaka mimba ina miezi 7 alikua anaingia period kama kawaida. Kilichomshitua ni tumbo kukua kwa kasi. Mwanzo alijua ni mihogo na chips ndo vinajaza tumbo.

Kwenda hosptal kumbe ni mjamzito
hilo la mimba kukua kwa kasi hutegemea maumbile ya mtu binafsi ila kama ile kasi si ya kawaida ni vyema akapate ushauri
 
hilo la mimba kukua kwa kasi hutegemea maumbile ya mtu binafsi ila kama ile kasi si ya kawaida ni vyema akapate ushauri
Miezi kuanzia 6 o 7 tumbo ndio hukua sana kwa wengine. Mwez wa 5 kushuka chini anakua hana tumbo kubwa. Alishaenda hosptali na ameshajifungua binti yake
 
Nasikia inawezekana
Kuna best yangu alikuwa anayo ila hakugundua kama anayo(kwa madai yake miezi mitatu ya mwanzo wa preg alikuwa anaenda period kama kawaida)
natumai alipata ushauri..
 
Miezi kuanzia 6 o 7 tumbo ndio hukua sana kwa wengine. Mwez wa 5 kushuka chini anakua hana tumbo kubwa. Alishaenda hosptali na ameshajifungua binti yake
nashukuru kama yote yalienda sawa manake nimegundua ujauzito waweza kuwa na hatari zake
 
Usiwe na wasiwasi Ipo tena saaana. .. kidume changu sahii kina miaka 4, mamake kama kawa aliendelea kutembea mwezini mpaka siku ya kujifungua ilikuwa vigumu kwake kubaini... lakini kadume kalitoka poa sana bila shida wala tatizo.
 
Biology nilipata zero na masikio yake, lakini sitashindwa kuchangia kiduchu .Hedhi itatoka wapi wakati wa ujauzito kwani mayai yanastopishwa kwa mda huo wa miezi tisa? Hedhi wakati wa
Mimba ni ugonjwa,ni kumuona doctor wa akina mama stoe suluhisho. Wakiofaulu biology mnisaidie kwani sayansi sio siasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ninavyojua mimi karibu na siku za hedhi mimba haiwezi kutungwa


 
Biology nilipata zero na masikio yake, lakini sitashindwa kuchangia kiduchu .Hedhi itatoka wapi wakati wa ujauzito kwani mayai yanastopishwa kwa mda huo wa miezi tisa? Hedhi wakati wa
Mimba ni ugonjwa,ni kumuona doctor wa akina mama stoe suluhisho. Wakiofaulu biology mnisaidie kwani sayansi sio siasa

Sent using Jamii Forums mobile app
Hamna mkuu mimi niko na jirani yangu anakua mjamzito na hedhi kama kawaida, na alishakwenda hospital zaidi ya mimba moja akaambiwa ni kawaida. Anajifungua salama na amani na mpaka leo anakua hivyo hivyo mimba zote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom