Je, Meli ya Mv Victoria ni mbovu?

Je, Meli ya Mv Victoria ni mbovu?

Hiyo source yako tuu imenichosha aisee, hao abiria walikuwa wanaenda engine room,wanaikagua meli hadi uvunguni?

Sawa bwana ili mradi tuu tuonekane kila serikali inachokifanya hakifai.
Ina maana wewe mwenzetu ni kiziwi kiasi kwamba ukipanda pantoni pale feri halafu injini ikazima huwezi kusikia?

Hizi akili zenu ni study case zinahitaji kufanyiwa utafiti.

Sent from my Infinix X653 using JamiiForums mobile app
 
Uza ubongo huo, mabadiliko ya ardhi yako kwenye jengo moja tu, huku majengo mengine yakiwa mazima?
Ahaaa, kama ni substandard kwa nini yasipasuke yote?

Quality control haifanyiki kwa macho Komrade
 
Hiyo meli niliipanda Bukoba-Mwanza 2013, dalili nilizoziona niliapa hata kama mbeleni itaboreshwa iweze hata kupaa kama bombardier sitokaa nisafiri na meli hiyo.

Pia usafiri wa majini kwa ujumla ni risk sana, hata ukerewe huwa napanda MV Nyehunge kwa tabu sana.
Usafiri wa majini wa uhakika unatolewa na Azzam tu na yule mbunge mstaarabu aliyegharamia ndege iliyompeleka Lisu Nairobi marehemu Turky Mungu ampumzishe Firdaus pepo ya juu kabisa.

Sent from my Infinix X653 using JamiiForums mobile app
 
Ina maana wewe mwenzetu ni kiziwi kiasi kwamba ukipanda pantoni pale feri halafu injini ikazima huwezi kusikia?

Hizi akili zenu ni study case zinahitaji kufanyiwa utafiti.

Sent from my Infinix X653 using JamiiForums mobile app
Sikujua kama pantoni na meli vipo sawasawa [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787].

Umeshawahi kuipanda MV Victoria lakini au ndio basi tuu ufurahishe jukwaa?

Kumbuka hilo jina la ID yangu kwanza,then watu wanafaulishwa kwenye boti hahahahah! Huu ni zaidi ya uzushi huu ni "ushuzi" kabisa.
 
Usafiri wa majini wa uhakika unatolewa na Azzam tu na yule mbunge mstaarabu aliyegharamia ndege iliyompeleka Lisu Nairobi marehemu Turky Mungu ampumzishe Firdaus pepo ya juu kabisa.

Sent from my Infinix X653 using JamiiForums mobile app
Apumzike kwa amani.

Naziogopa sana meli za masafa marefu, hasa nikisikia ajali imetokea. Kinachoniogopesha zaidi safari za Bk-Mza ni za usiku, yaani meli ikifika kina kirefu usiku wa manane inaanza kuyumba halafu ukichungulia kwa nje huoni hata kisiwa!
 
Kwani ni samaki kwamba mmoja akioza wote wameoza?
Kwa mantiki hii usilete hoja mfu kwenye mambo ya kitalaamu,eti miradi ya awamu hii ni substandard! Kama ni hivyo tungeshuhudia Kila majengo na barabara yanabomoka.
 
Apumzike kwa amani.

Naziogopa sana meli za masafa marefu, hasa nikisikia ajali imetokea. Kinachoniogopesha zaidi safari za Bk-Mza ni za usiku, yaani meli ikifika kina kirefu usiku wa manane inaanza kuyumba halafu ukichungulia kwa nje huoni hata kisiwa!

Usiku inakuwa hivi . Hii picha nilipiga mida ya saa tisa usiku
IMG_0778.jpg
 
Hii meli ilipark pale bandari ya Mwanza kusini (Mwanza South Port) kwa miaka mingi.

Hivi karibu kwenye utawala wa Magufuli meli hii imekarabatiwa kwa kupakwa rangi na kutengenezwa baadhi ya sehemu, inasemekana hadi Injini ilibadilishwa.

Hivi majuzi kuna jamaa yangu wa karibu alisafiri na hii meli kwenda Bukoba, kwa kweli kwa maelekezo yake hii meli ni Kimeo, ilizimika Mara kadhaa njiani wakati Mvua inanyesha na baadhi ya maeneo kupitisha maji.

Siku kadhaa nyuma meli ilizima tena ikabidi watu wafaulishwe kwenye maboti.

Meli imekaribia bandari ya kemondo ikazima tena.

Sasa muhimu kuchukua tahadhali mapema ili kuepusha majanga.

Serikali isipende sifa kwamba imetengeneza meli kumbe meli yenyewe mtego tu wa kuua watu.


Source: abiria wa kwenda BkView attachment 1633137
Eti Meli ilizama Mara kadhaa ziwani
Hata uongo si hivyo harafu hujui usemalo Mungu anakuona
 
Meli ni ile ile ila kuna Mambo yaliyonivutia

Chakula kwenye restaurant kimekuwa cheap tofauti na zamani. Beer juice n.k bei sawa na mtaani, ni bora ukanywe na kula kwenye meli kuliko kula mtaani (Kwa wale wa second sleeping/siku hizi inaitwa economy sijui business na first class)

Kuna siku kunakuwa na live band ndani ya pub ya meli.

Kuingia usumbufu umepungua ingawa upande wa bukoba naona Kama usumbufu wa kuingia umekuwa maradufu

Ulinzi, sehem kubwa ya meli kumejaa polisi na wanazunguka zunguka mara nyingi.
 
Hii meli ni kaburi linalotembea muda na siku yeyote tutashusha tena bendera nusu mlingoti
 
Bombadier Ilianza Hivi Hivi Mpaka Viongozi Wa Serikali Wakatoka Uchochoroni Kufafanua Haraka Sana Kuondoa Ukakasi.


Hili La Meli Isiwe Kimya Kesho Serikali Ije Na Majibu
Zinakuja Sikukuu Noeli Na Mwaka Mpya
Watu Watahofia Kupanda Dude Hilo.


Dkt Abasi Yupo Wapi? Aje Haraka
 
Kuna kitu siyo kibovu kwenye nchi hii?



 
Siyo kazi ndogo wanayoifanya kina Zitto na Lissu!!

Mwishowe mmeshika somo sasa!

Yaani mnaamua kuwa waongo mchana kweupe kuwashinda hata walimu wenu siyo?

Yaani mzigo unaobebwa na Meli ufaulishwe kwenye boti??

Pumbavu
Pumbavu mwenyewe

Waliofaulishwa ni abiria na si mizigo
 
Hili sina uhakika nalo, ila kuwa miundombinu mingi ni substandard ili kusaka political millage, hilo halina mjadala. Inawezekana mzigo haukifaulishwa bali watu ili kuokoa maisha yao. Lakini kwakuwa vyombo vya habari haviko huru, huwezi kusikia hili kwenye vyombo rasmi vya habari zaidi ya huku mitandaoni. Hivyo wangalau tunaona 50% kuna ukweli, na 50% tunasubiri udhibitisho.
Mimi nimezungumzia waliofaulishwa ni watu na si mizigo,umejibu vyema mkuu
 
Back
Top Bottom