Je, Marekani ni adui wa ubinadamu?

Je, Marekani ni adui wa ubinadamu?

Marekani ni taifa kama yalivyo mataifa mengine, ila tofauti yake na haya mataifa mengine ni kwamba Marekani ni nchi ambayo raia wake wengi si watu wa asili wa eneo lile, wengi wa wamarekani asili yao ni UINGEREZA, AFRICA AND LATIN AMERICA NA WENGINE NI WAYAHUDI. Asili ya watu wa eneo lile ni RED INDIS. Halfu Marekani ndiyo super power wa hii dunia kwa saiv.
Sasa tunaposema Marekani tuna maana gani?

Tushaona Marekani sikitu kimoja.

Wao wenyewe wanapingana.

Sasa sisi tunaposema "Marekani hivi, Marekani vile" wakati Marekani yenyewe inajipinga vibaya sana, maana yetu ni nini?

Hata ukichukulia uongozi wa juu wa serikali.

Ukiangalia tu safari ya Donald Trump Saudi Arabia unaweza kuona msimamo wa nchi hii ulivyobadilika katika muda mfupi tu kutokautawala wa Obama mpaka sasa kuhusu Saudi Arabia na siasa nzima za Mashariki ya kati.

Sasa nchi ambayo inaweza kubadilika badilika hivi unawezaje kusema ikohivi au vile?
 
One thing at a time.

Why is the fact that America did not nuke the Nazis - or even the entire Japan for that matter, since after all, they (Americans) supposedly hate humanity- immaterial?
Roosevelt, Churchill and Stalin agreed at Yalta that if Germany surrenders Unconditionally then no excessive force would be used against it.

Now, how can a single nation be a Champion of an International Treaty?
 
Internet imeanzishwa kama research project ya wizara ya ulinzi ya Marekani. Enzi hizo mtandao ukiitwa ARPANET.

Anayetaka kujua zaidi Wiki iko hapa ARPANET - Wikipedia

Kwa msingi huu, ni kweli kwamba bila Marekani mfumo mzima wa internet kama ulivyo leo usingekuwepo.

Na hao wanaoisema Marekani labda wangeisema kwa alama za moshi.

Maana hata mfumo wa umeme tunaoutumia umegunduliwa Marekani.

Waswahili walisema "Baniani mbaya, kiatu chake dawa".

Marekani si nchi tu. Ni wazo.

Ni wazo kwamba kuna sehemu wajanja wote waliokataa ujinga ujinga wa sehemu nyingine huko duniani wanaweza kukutana.

Hawa Watanzania wanaoikandia Marekani leo hawajui kwamba bila Marekani Hitler angetawala dunia na aghalabu angerudisha utumwa kwa watu weusi wote.

Sisemi kwamba Marekani haina mabaya, lakini kusema Marekani ni adui wa ubinadamu ni kuionea. Kwa sababu ni kitu complex sana kinachokataa simple definition.

Angalia tu Wamisionari waliojituma kusaidia watoto waliopata ajali ya gari utaona kuna watu wana moyo wa upendo na kujitoa sana. Hapo kuna wabongo kibao wakiona ajali kitu cha kwanza wanachofanya ni kuzisachi maiti kama zina hela.

Sasa watu waseme kwamba Watanzania ni wanyama wanaombea wengine wafe ili wawasachi?

Magufuli kachukua fedha za rambirambi kapeleka serikalini.

Tuseme Watanzania wanaibia mpaka wafiwa?

Mtu anakwambia Marekani hivi au vile, wakati hiyo hivi au vile anayoihusisha na Marekani unakuta nusu ya Wamarekani wenyewe wanaipinga.
Sidhani kama ni sahihi kusema au kudhani kuwa kama jambo A limeanzishwa na mtu fulani basi asingekuwepo lisingekuwepo....

Ninaona ni makosa kufikiri hivyo kwasababu jambo linapohitajika kwa watu linahitaji sababu tu na uhitaji ni sababu na kama asingeanzisha aliyeanzisha lingeanzishwa na mtu mwingine tu....

Kuanza kufikiri bila huyo muanzilishi kusingekuwepo na jambo lililoanzishwa ni kuanza kuona binadamu wengine hawafikirii kabisa kitu ambacho siyo sahihi kabisa,huwa ni suala la muda tu.....
 
Najaribu tu kuwaza kwa sauti ingetokea taifa la asia ususani waarabu wakaitawala dunia maisha yatakuwaje.
 
Roosevelt, Churchill and Stalin agreed at Yalta that if Germany surrenders Unconditionally then no excessive force would be used against it.

Now, how can a single nation be a Champion of an International Treaty?

Kama kweli Marekani ni adui wa ubinadamu, kwa nini Roosevelt aheshimu maamuzi ya vikao vya watu ambao hawana bomb wakati yeye kashapata bomb?

Kwa nini asiwapige mabomu anaotaka kuwapiga mabomu tu bila kujali vikao,kwa sababu ana mabomu na wao hawana? Tena awapige kwelikuwawahi kabla hawajapata mabomu na wao na kuwa nguvu sawa,kwa nini hakufanya hivyo? Kama kweli Marekani haipendi ubinadamu?

Hitler alikubali makubaliano hivyo hivyo na Neville Chamberlain. Na wala hakuyatekeleza. Na wala hakuwa na nuclear.
Kwa hiyo kuheshimu makubalianoya karatasi wakati una mabomu ya kuwalipua wengine wote hapa ni sifa ya kupenda ubinadamu.

Si sifa ya kutopenda ubinadamu.

Hitler angelipata hilo bomu kabla ya Mmarekani historia ya dunia ingekuwa tofauti sana leo.

Halafu watu wanakwambia Marekani haipendi ubinadamu.

A single nation can be the champion of an international treaty if that treaty works towards world peace at the detriment of that nations supremacy.

Hitler angeanza kupata nuclear asingekuwa na muda wa kungojea wengine waanze kupata nuclear na kuongea nao wafanye mikataba ya kupunguza nuclear.

Angewapiga mabomu watu to smithereens ilimradi Ujerumani itawale dunia tu.

Marekani ilikuwa na nafasi hiyo.Haikutakakufanya hivyo.

Sasa utasemaje Marekani haipendi ubinadamu?
 
Sidhani kama ni sahihi kusema au kudhani kuwa kama jambo A limeanzishwa na mtu fulani basi asingekuwepo lisingekuwepo....

Ninaona ni makosa kufikiri hivyo kwasababu jambo linapohitajika kwa watu linahitaji sababu tu na uhitaji ni sababu na kama asingeanzisha aliyeanzisha lingeanzishwa na mtu mwingine tu....

Kuanza kufikiri bila huyo muanzilishi kusingekuwepo na jambo lililoanzishwa ni kuanza kuona binadamu wengine hawafikirii kabisa kitu ambacho siyo sahihi kabisa,huwa ni suala la muda tu.....

Point ya kwanza, tofautisha kusema jambo lisingekuwepo na kusema jambo lisingekuwepo kama lilivyo sasa.

Likishaanzishwa na mtu ukija kutumia, hata kama angeanzisha mwingine, kuja kuwa kama ilivyokuwa is a statistical impossibility.

Sijui kama umeelewa nuance hiyo.

I find this place has a problem, the currency of nuance is in short circulation.

Halafu point kubwa zaidi hujaijibu.

Kama vitu vimegunduliwa Marekani, vimesajiliwa Marekani, viko controlled na Mrekani, kwa nini hawa wanaosema Marekani inachukia ubinadamu bado wanavitumia?

Hawaogopi kutiliwa sumu na Marekani inayochukia ubinadamu?
 
Nani kaitaja Quran?

Ulimwengu wako umezungukwa na duality ya Bible na Quran tu?

Ushawahi kukisikia "The Principles of Quantum Mechanics" cha Paul Dirac ?


Swali nililotaka unijibu hujanijibu, swali unalonijibu sijakuuliza unijibu.

Kwa nini unafikiri Bible ni kitabu kizuri kinachofaa kutumiwa kama kitabu cha authority ya kimantiki na mtu aliyeelimika katika dunia ya leo?

Hujajibu swali hili.

Umeongelea kuhusu aliyotabiri Yesu.

Kukuonyesha kwamba Bible ni kitabu kisichoweza kukubalika na mtu mwenye akili zake timamu kama authority, unajua kwamba kuna watu walimuuliza Yesu atarudi lini baada ya kudaiwa kwamba amefufuka na iliposemekana kwamba atapaa kwenda mbinguni?

Unajua jibu la Yesu lilikuwaje?

Aliwaambia watu, amini amin nawambia, baadhi yenu hamtaonja mauti kabla sijarudi tena.

Watu wakauza nyumba na mashamba waishi kitawa wakimsubiri Yesu arudi kuwachukua.

Walijua atarudi katika muda wa maisha yao kama alivyosema.

Yesu kasema bwana, atadanganyaje?

Na mpakaleo zaidi ya miaka elfu mbili hajarudi.

Sasa unataka niamini habari za kitabu hiki kama kitabu cha authority?
Hebu weka wazi, tatizo lako nini?
Mimi nimejaribu kuchambua kwa kutumia bible juu ya kutajwa kwa Ubaya wa amerika.je wewe hukubaliani na uchambuzi wangu?
Je, kama hutaki watu wajifunze kuhusu hili kanusha na weka uchambuzi wako kwa kutumia kitabu chochote au hata kwa uwelewa wako tu.wacha kua na mahaba ya ajabu kiasi hicho.
 
Hebu weka wazi, tatizo lako nini?
Mimi nimejaribu kuchambua kwa kutumia bible juu ya kutajwa kwa Ubaya wa amerika.je wewe hukubaliani na uchambuzi wangu?
Je, kama hutaki watu wajifunze kuhusu hili kanusha na weka uchambuzi wako kwa kutumia kitabu chochote au hata kwa uwelewa wako tu.wacha kua na mahaba ya ajabu kiasi hicho.
Tatizo ni kwamba kitabu chako unachokitumia kama msingi wa kutuangaza kimejaa giza na hakina mamlaka ya kutuongoza.

Kwa hivyo, unapoanza kwa kutaja tu muongozo wa Bible, unakuwa ushakosea.

Kwa sababu msingi wako wa mamlaka ya kutuangazia ukweli umejaa giza na hauna mamlaka hayo.
 
Tatizo nikwamba kitabu chakounachokitumiakama msingi wa kutuangaza kimejaa giza na hakina mamlaka ya kutuongoza.

Kwa hivyo, unapoanza kwa kutaja tu muongozowa Bible, unakuwa ushakosea.

Kwa sababu msingi wako wa mamlaka ya kutuangazia ukweli umejaa giza na hauna mamlaka hayo.
[emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1]
Al watan wewe mtata sana.
Wacha tumpelekee uvomvi huu gwajima.uone motowake.
 
Kama kweli Marekani ni adui wa ubinadamu, hao international students kwenye taasisi za elimu ya juu za Marekani wanafanya nini huko?

Vyuo vya Marekani vimejaa wanafunzi wa kimataifa wanaoenda kupata elimu huko.

Nchi inayoongoza kutoa washindi wa tuzo za Nobeli hususan katika nyanja za sayansi na uchumi ndo adui wa ubinadamu?

Acheni masikhara bana,.
 
Kama kweli Marekani ni adui wa ubinadamu, hao international students kwenye taasisi za elimu ya juu za Marekani wanafanya nini huko?

Vyuo vya Marekani vimejaa wanafunzi wa kimataifa wanaoenda kupata elimu huko.

Nchi inayoongoza kutoa washindi wa tuzo za Nobeli hususan katika nyanja za sayansi na uchumi ndo adui wa ubinadamu?

Acheni masikhara bana,.
Umeenda mbali sana huko gwiji.

Hii Jamiiforums tuimesajiliwa Marekani. Inatumia Cloudflare kampuni ya Kimarekani.

Watu hawa ambao ni adui wa ubinadamu kama wanavyodai hawa wanaodai hivyo.

Kwa nini hawa watu wanaosema Marekani ni adui wa ubinadamu wanakubali kutumia Jamiiforums iliyo katika mifumo ya Kimarekani?

Wangeisusia tu. Waunde yaoinayotumia mifumo ya kwao.

Hapondipoutakapoona unafiki wa "Baniani mbaya, kiatu chake dawa".
 
Umeenda mbali sana huko gwiji.

Hii Jamiiforums tuimesajiliwa Marekani. Inatumia Cloudflare kampuni ya Kimarekani.

Watu hawa ambao ni adui wa ubinadamu kama wanavyodai hawa wanaodai hivyo.

Kwa nini hawa watu wanaosema Marekani ni adui wa ubinadamu wanakubali kutumia Jamiiforums iliyo katika mifumo ya Kimarekani?

Wangeisusia tu. Waunde yaoinayotumia mifumo ya kwao.

Hapondipoutakapoona unafiki wa "Baniani mbaya, kiatu chake dawa".

Wanachoshindwa kuelewa ni kwamba hapa duniani hakuna perfect society.

Kila jamii ina mazuri na mabaya yake.

Hata binadamu wamoja wamoja tuna mazuri na mapungufu yetu.

Ni uhalisia tu wa maisha ulivyo.

Mtu anadiriki kusema Marekani ni adui wa ubinadamu wakati kuna watoto wa Kitanzania huko Iowa wakipatiwa matibabu na madaktari na wauguzi wa Kimarekani.

Hao watoto wamepelekwa huko Iowa na Wamarekani sijui wamisionari wale.

Mtu akawaambie hao watoto na ndugu zao kuwa Marekani ni adui wa ubinadamu basi tuone....
 
Kama kweli Marekani ni adui wa ubinadamu, kwa nini Roosevelt aheshimu maamuzi ya vikao vya watu ambao hawana bomb wakati yeye kashapata bomb?

Kwa nini asiwapige mabomu anaotaka kuwapiga mabomu tu bila kujali vikao,kwa sababu ana mabomu na wao hawana? Tena awapige kwelikuwawahi kabla hawajapata mabomu na wao na kuwa nguvu sawa,kwa nini hakufanya hivyo? Kama kweli Marekani haipendi ubinadamu?

Hitler alikubali makubaliano hivyo hivyo na Neville Chamberlain. Na wala hakuyatekeleza. Na wala hakuwa na nuclear.
Kwa hiyo kuheshimu makubalianoya karatasi wakati una mabomu ya kuwalipua wengine wote hapa ni sifa ya kupenda ubinadamu.

Si sifa ya kutopenda ubinadamu.

Hitler angelipata hilo bomu kabla ya Mmarekani historia ya dunia ingekuwa tofauti sana leo.

Halafu watu wanakwambia Marekani haipendi ubinadamu.

A single nation can be the champion of an international treaty if that treaty works towards world peace at the detriment of that nations supremacy.

Hitler angeanza kupata nuclear asingekuwa na muda wa kungojea wengine waanze kupata nuclear na kuongea nao wafanye mikataba ya kupunguza nuclear.

Angewapiga mabomu watu to smithereens ilimradi Ujerumani itawale dunia tu.

Marekani ilikuwa na nafasi hiyo.Haikutakakufanya hivyo.

Sasa utasemaje Marekani haipendi ubinadamu?


Halafu unavyokazania kwamba Marekani anaheshimu Vikao (Ndiyo Ubinadamu)
Unajua hata unachokiongelea kweli wewe? Au labda uniambie maana yako ya Ubinadamu.

Kama kipimo chako cha Ubinadamu wa Marekani ni kuheshimu mikataba. Nasikitika sana kukwambia kwamba umepotea sana njia. Mimi ninaweza kupinga hoja yako kwa kusema hata Benitho Mussolini aliheshimu Vikao hadi mwisho wa utawala wake. Mfano Mzuri dikteta yule ndiye aliyesaini Mkataba wa Lateran wa mwaka 1929 (The Lateran Treaty) ili taifa la Vatican lizaliwe. Kwa hiyo huyu naye ni rafiki wa Ubinadamu kwasababu tu alikubaliana na kikao?

Marekani huyo huyo aliyeheshimu Kikao cha Yalta cha mwaka 1945, ndiye huyo huyo aliyevunja makubaliano ya Kikao cha Postdam mwaka 1945. Walikubaliana wasitumie Silaha na Urusi ndiyo ilitakiwa ivamie Japan kama ingekataa kusalimu amri. Kama Marekani alikuwa anapenda Ubinadamu kwanini Harry Truman alifanya maaumizi ya peke yake bila kuwashirikisha wenzake na kuamua kulipua Hiroshima na Nagasaki ambayo hata Stalin na Chiang-Kai-Shek walikuwa wanaweza kuimudu?

NB: A single nation can be the champion of an international treaty if that treaty works towards world peace at the detriment of that nations supremacy.

-Has the world achieved Peace so far?
-Please i would like to see you mention any treaty that has worked towards global peace at the detriment of nation's Supremacy..
 
Kama kweli Marekani ni adui wa ubinadamu, hao international students kwenye taasisi za elimu ya juu za Marekani wanafanya nini huko?

Vyuo vya Marekani vimejaa wanafunzi wa kimataifa wanaoenda kupata elimu huko.

Nchi inayoongoza kutoa washindi wa tuzo za Nobeli hususan katika nyanja za sayansi na uchumi ndo adui wa ubinadamu?

Acheni masikhara bana,.
Kupata nafasi ya kwenda kusoma kule no ghali ukilinganisha name nchi za Asia.na kama umeweza kugharamia name ukibahatika kupata nafasi ukaenda kusoma na ukiwamtaalam kweli,watakulaghai ubaki kwao ,ili utaalam wao usitoke nje .
 
Umeenda mbali sana huko gwiji.

Hii Jamiiforums tuimesajiliwa Marekani. Inatumia Cloudflare kampuni ya Kimarekani.

Watu hawa ambao ni adui wa ubinadamu kama wanavyodai hawa wanaodai hivyo.

Kwa nini hawa watu wanaosema Marekani ni adui wa ubinadamu wanakubali kutumia Jamiiforums iliyo katika mifumo ya Kimarekani?

Wangeisusia tu. Waunde yaoinayotumia mifumo ya kwao.

Hapondipoutakapoona unafiki wa "Baniani mbaya, kiatu chake dawa".
Tatizo unaangalia zaidi uzuri wa technologia kuliko mabaya na madhara ya technologia.
 
Halafu unavyokazania kwamba Marekani anaheshimu Vikao (Ndiyo Ubinadamu)
Unajua hata unachokiongelea kweli wewe? Au labda uniambie maana yako ya Ubinadamu.

Kama kipimo chako cha Ubinadamu wa Marekani ni kuheshimu mikataba. Nasikitika sana kukwambia kwamba umepotea sana njia. Mimi ninaweza kupinga hoja yako kwa kusema hata Benitho Mussolini aliheshimu Vikao hadi mwisho wa utawala wake. Mfano Mzuri dikteta yule ndiye aliyesaini Mkataba wa Lateran wa mwaka 1929 (The Lateran Treaty) ili taifa la Vatican lizaliwe. Kwa hiyo huyu naye ni rafiki wa Ubinadamu kwasababu tu alikubaliana na kikao?

Umenukuu pale ulipotaka na kuacha pale muhimu. Benito Mussolini na Wamarekani wote washaheshimu na kuvunja mikataba.

Marekani ishavunja mikataba na Indians. Mussolini kashavunja mikataba na Hungary.

Mtu anatakiwa kumsikiliza His Imperial Majesty tu katika hotuba yake ya Geneva alivyoionya dunia kuhusu udhalimu wa Mussolini na jinsi Mussolini alivyovunja mikataba ya kimataifa na kuvamia Abyssinia (Ethiopia).

Kuvunja mkataba si threshold niliyoiweka, labda hujanisoma.

Nimeongelea stakes. Nimeongelea nchi kutotaka kuvunja mkataba wakati ina bomu ambalo linaweza kuihakikishia inavunja mkataba na kuishinda dunia nzima.

Sasa Mussolini aliwahikuwa na bomu la atomiki kwa namna hiyo?

Marekani huyo huyo aliyeheshimu Kikao cha Yalta cha mwaka 1945, ndiye huyo huyo aliyevunja makubaliano ya Kikao cha Postdam mwaka 1945. Walikubaliana wasitumie Silaha na Urusi ndiyo ilitakiwa ivamie Japan kama ingekataa kusalimu amri. Kama Marekani alikuwa anapenda Ubinadamu kwanini Harry Truman alifanya maaumizi ya peke yake bila kuwashirikisha wenzake na kuamua kulipua Hiroshima na Nagasaki ambayo hata Stalin na Chiang-Kai-Shek walikuwa wanaweza kuimudu?

Hii habari ni moot kwa sababu threshold ni kutawala dunia kwa kutumia mabomu ya atomiki.

Mtu asiyependa ubinadamu angeifutiliambali Ujapani na Ujerumani na kujisimika yeye muuaji wa binadamu karibu wote duniani.

Hatujaona hilo.

Tumeona Wamarekani, mpaka waliotengeneza hilo bomu wenyewe kina Oppenheimer wakiwa mstari wa mbele kupinga matumizi ya bomu la atomiki. Katika muda ambao Marekani pekee ndiyo ilikuwa nchi yenye bomu hilo.

Hivi kweli hawa ndio watu ambao hawapendi ubinadamu?

NB: A single nation can be the champion of an international treaty if that treaty works towards world peace at the detriment of that nations supremacy.

-Has the world achieved Peace so far?
-Please i would like to see you mention any treaty that has worked towards global peace at the detriment of nation's Supremacy..
Why does world peace need to be achieved for my statement to be valid?

Have you ever heard of Nuclear Proliferation Treaty?

SALT 1 and 2? START?

Hao Wamarekani kama kweli hawapendi ubinadamu kwanini hawajalipua mibomu ya nuclear waue watu vizuri tangu 1945?
 
Kwa hiyo madhara ya teknolojia ndo yanaifanya Marekani iwe adui wa ubinadamu?
Technology haikwepeki kwa kizazi hiki,ni lazima kuitumia.
Ila usiifulahie kwa mahaba mazito kwasababu inamadhara makubwa kwetu.
Jitahidi kila unaposiki kuna kitu kipya cha kitekinoloji kimeanza kutumika muombe mungu akusamehe kwa kutumia kifaa ambacho c Salama kwako.ila muombe akubali kuwa hakuna namna kukitumia.
ACHA KABISA KUWA NA MAHABA MAZITO NA TECHNOLOGY. ingawa hatuna jinsi kuvitumia.

NA BADO TECHNOLOGY ITAKUA SANA DUNIANI MAANA WATAALAM WANATUAMBIA MPAKA SASA UJUZI WOTE AMBAO MWANADAM AMEFIKIA HADI LEO HII ,BADO HATA 50% HAJAFIKIA.
 
Back
Top Bottom