Internet imeanzishwa kama research project ya wizara ya ulinzi ya Marekani. Enzi hizo mtandao ukiitwa ARPANET.
Anayetaka kujua zaidi Wiki iko hapa
ARPANET - Wikipedia
Kwa msingi huu, ni kweli kwamba bila Marekani mfumo mzima wa internet kama ulivyo leo usingekuwepo.
Na hao wanaoisema Marekani labda wangeisema kwa alama za moshi.
Maana hata mfumo wa umeme tunaoutumia umegunduliwa Marekani.
Waswahili walisema "Baniani mbaya, kiatu chake dawa".
Marekani si nchi tu. Ni wazo.
Ni wazo kwamba kuna sehemu wajanja wote waliokataa ujinga ujinga wa sehemu nyingine huko duniani wanaweza kukutana.
Hawa Watanzania wanaoikandia Marekani leo hawajui kwamba bila Marekani Hitler angetawala dunia na aghalabu angerudisha utumwa kwa watu weusi wote.
Sisemi kwamba Marekani haina mabaya, lakini kusema Marekani ni adui wa ubinadamu ni kuionea. Kwa sababu ni kitu complex sana kinachokataa simple definition.
Angalia tu Wamisionari waliojituma kusaidia watoto waliopata ajali ya gari utaona kuna watu wana moyo wa upendo na kujitoa sana. Hapo kuna wabongo kibao wakiona ajali kitu cha kwanza wanachofanya ni kuzisachi maiti kama zina hela.
Sasa watu waseme kwamba Watanzania ni wanyama wanaombea wengine wafe ili wawasachi?
Magufuli kachukua fedha za rambirambi kapeleka serikalini.
Tuseme Watanzania wanaibia mpaka wafiwa?
Mtu anakwambia Marekani hivi au vile, wakati hiyo hivi au vile anayoihusisha na Marekani unakuta nusu ya Wamarekani wenyewe wanaipinga.