Je, Makonda kavunja mwiko?


Salaam.

Hapa hatuongeleai wala hatuchambui kama kuna ukweli au uongo kwa aliyosema Makonda, hapa tunaongelea ile kuweza kutamka tu aliyoyatamka, kwangu mimi ni ushujaa tosha.
 
Yani Makonda kafanya mageuzi makubwa sana tena mno...angewasema hivi hivi bila kuwa na ushahidi kuwa yeye alifuatwa na kuhogwa ningesema mnafiki na mzandiki.Lakini kasema wazi wazi kuwa yeye alifuatwa na kumegewa taarifa na ka kikundi ka watu kumi wampe mgao wa milioni 50 kwa mwezi ili akae kimya swala la shisha yeye akakataa..

Swali la msingi ambalo ndio kiini cha Makonda ..ni kuwa kama waliweza kwenda kwake yeye Mkubwa watashindwa nii kwenda kwa wadogo zke yeye ambao ndio wenye jukumu la kuwakamata wao waliokwenda kwake..[Logic] Na walikwenda kwake kama kutanua wigo wa kunyamazisha.Kama yeye alifikiwa na amesema hadharani kwanini wao washindwe kusema hadharani kuwa HATUKUFIKIWA? na kama walifikiwa wasema nao WALIFIKIWA na MGAO waliukataaa...na ndio maana zoezi la SHISHA lilifanikiwa na hivyo swala la SHISHA kuwa ipo mtaani ni uongo...hivyo Mh Waziri Mkuu anapombana Mkuu wa MKoa taarifa alizonazo si kweli na taarifa anazozitoa Makonda hazina uhalisia hivyo katika kuwajibika kwa Jamhuri wao taarifa zao ndizo sahihi.

Rais Magufuli na Mh Waziri Mkuu wana kazi...nzito lakini nafurahi wanajua nii wanachotaka kutupatia na wasiogope kuwaludisha Watuumishi wa Umma Mitaani kwa kuwanyima KAZI ikiwa na kufungwa kuna husu wafungwe sie Watanzania tutajifunza kuwa Tunataka Taifa makini..na utii wa sheria bila kujali nani ana nafasi gani...awe tajiri ama masikini.
 
Mkuu mbona hizo ni tuhuma tu? Kuna ushahidi wowote mpaka sasa kwamba Siro kapokea rushwa?
Kweli ni tuhuma ila tuache kusema Makonda anatafuta sifa, kana kwamba huyo Siro ni Mungu hawezi kuchukua rushwa! Nchi hii kuna watu na heshima zao wameliabisha taifa!
 
Sijui tunabishana nini? Au unataka nilete coment zako za humu kuonesha uchadema wako?
 
Hekima au Busara ndiyo nadhani vimekosekana!

Kumtuhumu mtu hadharani bila ya unachokituhumu kuthibitishwa na taasisi husika ni tatizo, vipi ikija kuthibitika siyo kweli kwa tuhuma za RC dhidi ya Siro?

Kwakuwa amemtuhumu Siro hadharani, Siro ange jihudhuru ama angeondolewa nafasi yake ili kupisha uchunguzi.

Ushujaa wa RC ungeanza na yeye kwataja kwa majina "hadaharani" wale woote waliojaribu kumuhonga na kuweka bayana tuhuma zake kwa Siro na jeshi la polisi!

RC kwa nafasi yake, ange[peleka tuhuma zake pahala husika na zikisibitika haikuwa mbaya kuzisema hadharani, lakini kwa sasa wakazi woote wa Dar na Tz kwa ujumla tunaaminishwa kutokuwa na imani na jeshi la polisi hadi pale itakapo thibitika vinginevyo.
 

Binafsi ningemwona shujaa kama angewataja hadharani hao wafanya biashara wa @5M, na atake mienendo yao ichunguzwe ili kubaini uhusika wao kuwatia polisi kigugumizi! Rushwa ni kosa la jinai kwa anayetoa na kwa anayepokea, ila yeye alielekea kuwarushia polisi tuhuma kisiasa ili yeye "apone" na sio kutaka hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya jinai husika!
 
Ni kitendo cha kishujaa sana. Jwtz nao wako kikaangoni, askari wake wengi wanajifanya wababe kwa raia na barabarani, ukiwahoji wanaweza kukuchangia kukupiga, wanajenga ukuta na raia! Nidhamu ya uoga dhidi yao ma wananchi ndo kilichopo katikati!
Ni kama ugomvi wa wachawi. Hata wakigombana bado kila mmoja akikupatia anakudhuru vilevile. Hata hivyo RC kusubiri hadhara/matukio ni tabia/utamaduni mbaya, sio ushujaa.
 
Mbowe ana nguvu kuliko rais na dola?!!?
Hongera Mbowe.
Ndioaana JPM kaamua maandamano na mikitano "ikafanywe" Hai, tunatakiwa tufanye kazi sio kuamdamana nchi nzima, nafikiri umenielewa!
 
Huyu bwana mdogo anafanya mambo utadhani hakuna kesho.
 
Ila Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu, mi itendeke namna hapo, sio bure!!!
 
Duu!! Wewe Bi. Mkubwa kweli kiboko. Inaonekana moderators bado hawajakufahamu vizuri. Wape darsa ili wasiokufahamu waweze kukufahamu vizuri.
 
Kuwataka haitoshi. Angewakamata ingeeleweka. Tunajuaje kama si yeye aliyewaomba hao watu kila mmoja wao awe anampatia sh 5m kila mwezi. Iliposhindikana ndipo anatoka hadharani kulalamika. Makonda siyo malaika. Anashiba na kupata njaa.
 
Huo ndio mwanzo wa mwisho wa Mh Kondakta.
 

binafsi siungi mkono hoja yako kabisa.

itakuwa ni makosa makubwa sana kama tunaweza kuwa na viongozi ambao wanashindwa kutoa maelekezo kwa watu walioko chini yoa na wakawasimamia kutekekeleza maelekezo hayo na badala yake kiongozi anaibuka na hoja ambayo ambayo kaifikiria yeye peke yake na anatumia mikutano kutangaza hoja na kujaribu kutafuta mbinu zozote kuwashawishi watu walioko juu kushinikiza wazo lake au kuonyesha kukwama kwa wazo ni makosa ya wengine.

sijasema yeye aliyetoa tuhuma alitumia njia hii, ila najiuliza alikuwa na uhakika kuwa aliyemtuhumu kafanya kosa hilo au yeye katafuta hoja ya kisiasa kwenye jukwaa.

hatuwezi kupiga hatua hatua kwa njia hii na hii ni njia ambayo kiongozi anawagawa wafuasi walioko chini yake.

mimi naamini kama kiongozi ni kosa kubwa kusimama kusimama kwenye jukwaa kumtuhumu mtu aliyeko chini yako au aliyeko juu yako. kama kunajambo huridhiki nalo lichukulie hatua katika taratibu za serikali.

iawapo wananchi wameleta malalamiko hayo ndiyo unaweza kuwaahidikuyashughulikia na ukibaini uzembe ndio unaweza kusimama kwenye majukwaa kuwaeleza wananchi hatua mlizochukua.

kwangu mimi naona hili ni kosa kubwa na ambalo linatakiwa kuwafundisha wote wanaolifuatilia kuwa.
1. kama kiongozi unatakiwa kukaa na watendaji wako mkajadili hoja kwa kuangalia tatizo na mtalitatuaje.
2. mkishajadili nakukubaliana ndio kongozi anaweza kusimama kwenyejukwaa kutoa sumary ya kile walichokubaliana kama kuoa maagizo. labda liwetukio la emergency lilitukia ghafla na linahitaji maamuzi.
3. kongzi kazi yake sikuongea kwenye majukwaa tu. anaka na watu wake wanapanga, anasimamai watu walioko chini yake kuhakikisha wanatekeleza na anatumia majukwaa kuhamasisha utekelezaji.
4. Timu moja moja hamuwezi kulaumiana uwanjani mkapata mafanikio. ukiona timu wanaanza kulaumiana uwanjani basi mara zote huwa wanatoka kwenye mchezo na ni mwanzo wa kufungwa. ukiwa uwanjani kazi yako ni kucheza yanatukia yakiwa chni yako chukua hatua na yaliyoko juu yako yaripoti sehemu husika kwa taratibu za kiofisi. yupo kocha pembeni anayetazama nani kafanya makosa yeye ndiye atajua nani wa kumuwajibisha na nani wa kumuacha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…