Je, mahali panapoitwa Ngende ni pakusadikika?

Je, mahali panapoitwa Ngende ni pakusadikika?

Ndio, hiyo sehemu ipo, na ipo ktk Kijiji kiitwacho Mkwera ktk Mkoa wa Lindi ni mpakani mwa Mtwara na Lindi, kwa wale wanaoifahamu Nyangao basi ukitoka hapo unapta vjj km viwili au kimoja. NA HAYO MAMBO YAPO SANA TANGIA MIAKA MINGI, NA UKIKIUKA MASHARTI USISHANGAE WW MWENYEWENA EITHER FAMILY AKO MKAPOTEZA MAISHA

Sent using Jamii Forums mobile app
Ngende si ipo liwale mkuu? Kulikofanywa zindiko la uhuru wa Tanzania mpya?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hahaaha...daah huo msitu kuna jmaa yangu alitusimulia kafika huko...full mauza uza
 
yes
Sehemu hiyo ipo kweli inapatikana wilaya ya Liwale nkoa wa Lindi katikati ya msitu wa Selous,moja ya wataalam wahudumu katika kilinge hicho ni ukoo niliozaliwa Mimi so mababu zangu walihudumia Ngende miaka mingi tu,ila kwa sasa kilinge kimepungua nguvu,pale unapewa utajiri kwa sharti la kurudisha shukrani ukijifanya kusahau unatumiwa mnyama yoyote yule anakuja kukudhuru,pale ngende ukienda unapokelewa na nyani na wanyama wengine nao wanazungumza karibia lugha zote duniani

Karibu Ngende kwa Wamagingo au Wangindo

Sent using Jamii Forums mobile app
Jamaa yangu alienda alishangaa anatajwa jina lake huku hajamwambia mtu yoyote alafu lugha yake pia ndo alikua anaongea na mtu asie mwona kilugha chake mshikaji..Inatisha kama ni utajiri acha Mungu atakavonibariki maishani nitaridhika.
 
hap
uongo bhana,hizo ni stori tuu bhana.
hapana kiongozi jamaa yangu alifika kwenye kijiji kimoja anasema hicho kijiji watu wamevaaa mahirizi tu shingon, mkononi,kiunoni...akakutana na mtu akamuuliza umekuja hapa wa ajili ya kwenda ngende jamaa akasema ndio umejuaje? huyo mwenyeji aksema tangu unavopanga safari yako kuja huku tunakua tumeshajua ujio wako...Mwenyeji akamwambia ila ujio wako hautafanikiwa...!! jamaa akasema nitafanikiwa...mwenyeji akasema twende, jamaa akapewa hirizi mkononi humo njiani alikua anapishana na kundi la simba lakini haliwadhuru sababu ya ile hirizi.....niishie hapo😀
 
Ngende iko Lindi,.ni sehemu maarufu kwa ushirikina wa hali ya juu,.wanasiasa,wafanya biashara,na watu mbalimbali huenda kuweka mambo yao sawa na hasa kuomba utajiri,..

Ukifanikiwa mambo yako,utaambiwa upeleke shukrani yako kwa mizimu,na ajabu unaweza ambiwa upeleke pini,sindano au hata njiti ya kibiriti hapo ndipo watu wanapojisahau na kuanza kuteseka kwa kudaiwa...
 
Aliyesema ipo kata ya mpiga miti Yuko sahihi, nyingine ni story za kutishana, mi nilifika mpaka kwenye zahanati ya mpya ya mpiga miti
 
Ipo wilaya ya Liwale mkoa wa Lindi, kuna mjomba angu mmoja alinisimulia aliwahi kwenda kwa shida zake sasa ikawa njianj akikutana na watu wakumuuliza unaenda wapi? Anajibu "tunaenda kusikiliza uongo wao kwa hawa jamaa"(anamaanisha huko Ngende kwa waganga yaani ni waongo hawaamini ila anakwenda kujaribu) Sasa alipofika akaulizwa umekuja kufanya nini huku na wakati sisi ni waongo? Ikabidi awe mpole na kuomba radhi akaambiwa usiniombe mimi kamuombe yule pale anaoneshwa chatu mmoja mkubwa sana kama Anaconda akawekewa unga kiganjani akamlambishe ndio msamaha. Sasa Anko akifikiria maneno aliyoyasema njiani na huyo jamaa wakuombwa radhi jinsi alivyo ule unga wa kiganjani atashiba kweli au ndio atakuwa yeye mwenyewe ni msosi?.

Ila ni sehemu maarufu kwa kusini inasadikia kwa kutoa utajiri na mambo mengine mengi ya kishirikina.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu msalimie Mh Membe...
 
Back
Top Bottom