Mhusika mkuu
JF-Expert Member
- Jun 13, 2013
- 432
- 510
Ingawa Biblia haina orodha ya mazoea yote tunayopaswa kuepuka, ina kanuni zinazoweza kutusaidia kuelewa jinsi Yehova anavyohisi kuhusiana na mazoea hayo. Hataki tuvute sigara, kutumia kileo kupita kiasi, au kutumia dawa za kulevya. Ikiwa sisi ni rafiki za Mungu, tutaepuka kufanya mambo hayo. Kwa nini? Kwa sababu tunaheshimu sana zawadi ya uhai. Tabia kama hizo zinaweza kufupisha uhai wetu, kudhuru afya yetu, na kuwadhuru watu walio karibu nasi. Watu wengi hujaribu kuacha mazoea hayo ili walinde afya zao. Hata hivyo, tukiwa rafiki za Yehova, tunaacha mazoea hayo kwa sababu tunampenda. Mwanamke mmoja kijana alisema hivi: “Kwa msaada wa Yehova, nilisafisha maisha yangu na kuacha uraibu wangu. . . . Ninafikiri isingekuwa rahisi kwangu kufanya mabadiliko hayo kwa nguvu zangu mwenyewe.” Acheni tuzungumzie kanuni tano za Biblia ambazo zitamsaidia mtu kuacha mazoea yenye kudhuru.
“Wapendwa, kwa kuwa tuna ahadi hizi, acheni tujisafishe kila unajisi wa mwili na roho, tukiukamilisha utakatifu katika kumwogopa Mungu.” (2 Wakorintho 7:1) Yehova anataka tuwe huru kutokana na mazoea yasiyo safi ambayo yanaweza kuchafua akili au mwili wetu.
Sababu kuu ya ‘kujisafisha kila unajisi’ inaelezwa kwenye 2 Wakorintho 6:17, 18. Yehova anatuambia: “Mwache kugusa kitu kichafu.” Kisha anatuahidi hivi: “Nitawakaribisha ndani. Nami nitakuwa baba kwenu, nanyi mtakuwa wana na mabinti kwangu.” Naam, kama vile baba anavyowapenda watoto wake ndivyo Yehova atakavyotupenda ikiwa tutaepuka kitu chochote kinachoweza kutufanya tusiwe safi mbele zake.
“Lazima umpende Yehova Mungu wako kwamoyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote.” (Mathayo 22:37) Hii ndiyo amri muhimu zaidi kuliko zote. (Mathayo 22:38) Yehova anastahili upendo wetu kamili. Tunawezaje kudai kwamba tunampenda kikamili ikiwa tunaamua kufanya jambo linaloweza kufupisha uhai wetu au kuharibu ubongo wetu? Badala yake, tunafanya chochote tunachoweza ili kuonyesha kwamba tunaheshimu uhai ambao ametupatia.
“[Yehova] huwapa watu wote uhai na pumzi na vitu vyote.” (Matendo 17:24, 25) Rafiki yako akikupa zawadi ya pekee, je, unaweza kuitupa au kuiharibu? Uhai ni zawadi ya pekee sana kutoka kwa Yehova. Tunaithamini sana zawadi hiyo. Kwa hiyo, tunataka kuutumia uhai wetu kwa njia ambayo itamletea utukufu.— Zaburi 36:9.
“Lazima umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.” (Mathayo 22:39) Mazoea yasiyo safi hayatudhuru sisi tu. Yanaweza kuwadhuru watu wengine pia, na mara nyingi yanawadhuru watu tunaowapenda sana. Kwa mfano, mtu anayeishi na mvutaji wa sigaraanaweza kupata ugonjwa mbaya kwa sababu tu ya moshi wa sigara. Lakini tunapoacha mazoea hayo, tunawaonyesha watu walio karibu nasi kwamba tunawapenda.—1 Yohana 4:20, 21.
“Endelea kuwakumbusha wajitiishe na kuzitii serikali na mamlaka.” (Tito 3:1) Katika maeneo mengi ni kosa kisheria kutumia au kuwa na dawa za kulevya. Kwa kuwa Yehova anatuamuru tuheshimu serikali, tunatii sheria hizo.—Waroma 13:1.
“Wapendwa, kwa kuwa tuna ahadi hizi, acheni tujisafishe kila unajisi wa mwili na roho, tukiukamilisha utakatifu katika kumwogopa Mungu.” (2 Wakorintho 7:1) Yehova anataka tuwe huru kutokana na mazoea yasiyo safi ambayo yanaweza kuchafua akili au mwili wetu.
Sababu kuu ya ‘kujisafisha kila unajisi’ inaelezwa kwenye 2 Wakorintho 6:17, 18. Yehova anatuambia: “Mwache kugusa kitu kichafu.” Kisha anatuahidi hivi: “Nitawakaribisha ndani. Nami nitakuwa baba kwenu, nanyi mtakuwa wana na mabinti kwangu.” Naam, kama vile baba anavyowapenda watoto wake ndivyo Yehova atakavyotupenda ikiwa tutaepuka kitu chochote kinachoweza kutufanya tusiwe safi mbele zake.
“Lazima umpende Yehova Mungu wako kwamoyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote.” (Mathayo 22:37) Hii ndiyo amri muhimu zaidi kuliko zote. (Mathayo 22:38) Yehova anastahili upendo wetu kamili. Tunawezaje kudai kwamba tunampenda kikamili ikiwa tunaamua kufanya jambo linaloweza kufupisha uhai wetu au kuharibu ubongo wetu? Badala yake, tunafanya chochote tunachoweza ili kuonyesha kwamba tunaheshimu uhai ambao ametupatia.
“[Yehova] huwapa watu wote uhai na pumzi na vitu vyote.” (Matendo 17:24, 25) Rafiki yako akikupa zawadi ya pekee, je, unaweza kuitupa au kuiharibu? Uhai ni zawadi ya pekee sana kutoka kwa Yehova. Tunaithamini sana zawadi hiyo. Kwa hiyo, tunataka kuutumia uhai wetu kwa njia ambayo itamletea utukufu.— Zaburi 36:9.
“Lazima umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.” (Mathayo 22:39) Mazoea yasiyo safi hayatudhuru sisi tu. Yanaweza kuwadhuru watu wengine pia, na mara nyingi yanawadhuru watu tunaowapenda sana. Kwa mfano, mtu anayeishi na mvutaji wa sigaraanaweza kupata ugonjwa mbaya kwa sababu tu ya moshi wa sigara. Lakini tunapoacha mazoea hayo, tunawaonyesha watu walio karibu nasi kwamba tunawapenda.—1 Yohana 4:20, 21.
“Endelea kuwakumbusha wajitiishe na kuzitii serikali na mamlaka.” (Tito 3:1) Katika maeneo mengi ni kosa kisheria kutumia au kuwa na dawa za kulevya. Kwa kuwa Yehova anatuamuru tuheshimu serikali, tunatii sheria hizo.—Waroma 13:1.