Nina ndugu alipata ajali na kupata ulemavu wa kudumu na hiyo ajali alisababishiwa kwani dereva alihama upande wake na kumfata. Sasa chombo chake hakikuwa na bima na alienda kudai fidia yake kwani hicho chombo kilisababisha ajali kilikatiwa third party na yeye alienda kudai fidia ya kwake kwa ulemavu aliopata na sio chombo chake kwakuwa anafahamu hakikuwa na bima. Sasa watu wa bima hawataki kumlipa kisa tu alipata ajali kwenye chombo kilichokuwa hakina bima.
Swali langu je kuna sheria yoyote inayosema mtu aliesababishiwa ajali asilipwe kama chombo chake hakina bima?
Naombeni kuelimishwa hapo.
Swali langu je kuna sheria yoyote inayosema mtu aliesababishiwa ajali asilipwe kama chombo chake hakina bima?
Naombeni kuelimishwa hapo.