Je, kuna kudanganya umma kwa manufaa ya umma?

Je, kuna kudanganya umma kwa manufaa ya umma?

Kamundu

Platinum Member
Joined
Nov 22, 2006
Posts
9,615
Reaction score
15,021
Ni swali najiuliza tu. Kuna wanasome tusiogope chochote wakati hata wakisimama kuongea wanakuwa na mwanajeshi nyuma! Sasa kama kweli huohopi kwanini wanajeshi kila mahali. Kama kweli viongozi hawaogopi chochote basi tusipoteze pesa za wananchi kulinda mpaka na mahilikopya wakati wanafunzi hawana madawati na Mungu ana walinda.

Watu wanaaibishwa kwa kuvaa barakoa kujikinga lakini wanaambiwa wakienda nyumbani walale kwenye neti kujikinga na malaria! Kwanini kulala kwenye neti isiwe kitu cha aibu kwani tunaogopa nini?

Sisi wenyewe hapa tuna machanjo chungu nzima tumepigwa tukiwa watoto hata sasa serikali ina shauri watoto waende kupigwa chanjo ambazo zinatoka makampuni ya mabeberu. Makampuni hayahayo tunajifanya kama vile sasa wanataka kutuuwa wakati Watanzania 100% ya watu wazima wanachanjo kwanini wasingetuua wakati huo miaka hiyo yote?

Tusidanganyike tujikinge na tupiganie chanjo hao viongozi wataishia kujichanja wenyewe kwa siri tusipokuwa makini.

Sasa eti anasema mtoto wangu, wadogo zangu na wengi wamepata na kupona sasa mbona tena ulituambia corona haipo!! au wote hawa walipata kabla? Kuna dalili

Za kupunic na kutokujua anachokiongea. Si kweli kwamba Dunia inatutakia mabaya! Muda mwingi ni fikra zetu wenyewe za kutokujiamini.
 
Huyu mtu wetu Mimi huwa sioni hiyo Nia njema kwa nchi yetu wanayosema anayo zaidi ya maigizo,Ila moyoni mwake naona amejaa hila na uovu kwa nchi hii na watu wake
 
Sidhani kama wanadanganya umma, uelewa wao ndipo ulipofikia kwamba nyungu, malimao, tangawizi na vitunguu swaumu ndio tiba sahihi.Kwamba kuna watu wana ajenda hasi dhidi ya nchi n.k
 
Huyu mtu wetu Mimi huwa sioni hiyo Nia njema kwa nchi yetu wanayosema anayo zaidi ya maigizo,Ila moyoni mwake naona amejaa hila na uovu kwa nchi hii na watu wake

Hata mimi huwa nashangaa sana nikisikia wapambe wake wanasema eti ana nia njema kwa nchi, kwani nia njema ni mpaka wao watuambie sisi hatuwezi kuiona?
 
Taabu nyingi sana Mungu amemgawia kila mtu, na nira nzito ipo juu ya mwanadamu; tangu siku yao ya kutoka tumboni mwa mama zao, hata siku ile watakapoirudia nchi, mama wa wote walio hai.
 
Sidhani kama wanadanganya umma, uelewa wao ndipo ulipofikia kwamba nyungu, malimao, tangawizi na vitunguu swaumu ndio tiba sahihi.Kwamba kuna watu wana ajenda hasi dhidi ya nchi n.k
kama ni hivyo, basi tuna safari ndefu sana.
na wataalam wote tunaowapeleka nje kusoma na wao ndio wamekwamia hapo?.
 
Halafu kwanini ni corona tu?
Mbona magonjwa mengine tunafata kila kitu wanachosema wataalam wa afya?
Kwanini corona ?
Shida ni kwamba rais wako amejipa sifa ya umungu hivyo hataki kuonekana amekosea, yaani yeye kujifunza kutokana na kosa alilofanya na kubadirika hawezi ,analazimisha tu watu muendelee kuamini yupo sahihi labda mpaka na yeye afe ninyi mfe.
 
Kwa sababu Corona ilipokuja ilivamiwa na wahubiri uchawara na conspiracists. Itachukua muda mrefu sana kuiondoa akilini hiyo sumu iliyopandikizwa akilini mwa watu katika atua za awali.

Kuna watu wana elimu kubwa sana na hawako serikalini wala vibarua vyao havitishwi kwa kuzungumza ukweli kuhusu Corona ila cha ajabu wamejaa conspiracies na elimu potofu kabisa kuhusu Corona.
Halafu kwanini ni corona tu?
Mbona magonjwa mengine tunafata kila kitu wanachosema wataalam wa afya?
Kwanini corona ?
 
Ii ina maana Uyu bwana angekuepo toka zaman ata izo chanjo tusinge pigwa
Yaani tungekufa na manjano, surua, pepopunda, na angetuambia tumtangulize Mungu mbele, Mungu gani atakubali uzembe? Eti tuombe, tufunge! Ahaaa!
 
Shida ni kwamba rais wako amejipa sifa ya umungu hivyo hataki kuonekana amekosea, yaani yeye kujifunza kutokana na kosa alilofanya na kubadirika hawezi ,analazimisha tu watu muendelee kuamini yupo sahihi labda mpaka na yeye afe ninyi mfe.
Inatokana na tabia ya kulazimisha mambo toka uchaguzi kura kuporwa na kulazimisha ushindi wa kishindo, sasa analazimisha kuondoa maradhi kwa maombi!
 
Serikali ya awamu hii imejaa unafika, uwongo na siasa za ulaghai. Hawa tuwapuuze.

Kwa sasa ni aheri tuwasikilize viongozi wa dini ambao tunaamini kuwa kweli ni viongozi wa dini siyo wale matapeli wa kutumia neno la Mungu, wakitoka madhabahuni wanaenda kutengeneza clips za ngono.
 
Hata mimi huwa nashangaa sana nikisikia wapambe wake wanasema eti ana nia njema kwa nchi, kwani nia njema ni mpaka wao watuambie sisi hatuwezi kuiona?
Mtu anaua raia, anateka na kupoteza watu, anabmbikia watu kesi za uhujumu uchumi, halafu awe na nia njema na raia?
 
Back
Top Bottom