nyumbamungu
JF-Expert Member
- Mar 3, 2017
- 1,034
- 900
Leo katika kipindi cha PB Clouds Fm nilimsikia Masoud Kipanya, akimuuliza Sam Sasali kama Kirusi "Virus" ni Kiumbe Hai au la!
Ningependa kujua kuhusu hili swali wakuu.
====
Ningependa kujua kuhusu hili swali wakuu.
====
Kirusi ni kweli kina tabia za viumbe hai na visivyo hai.
Lakini kwenye upande wa tabia za viumbe hai hakikamilishi sifa zote kama excretion, growth na reproduction
Kina act kama kiumbe hai kikiwa ndani ya host cell na kinatumia protein machinery ya cell kupitia control room ya cell ambayo ni nucleus ambamo kuna DNA na kuunda copy zake nyingi nyingi kisha seli hufa na kuachia virusi wengine wengi.
Lakini kikiwa nje ya host cell kinakuwa ni kama molecule kama ilivyo molecule ya chumvi au hydrocarbon yaa protein coat yenye nucleic acid ndani yake
Ni ngumu ku deal na virus kwa sababu kudeal na virus kunahitaji udeal na means yake ya kujiunda kupitia host cell
Kumaanisha utahitajika ku deal na genetic material yake ili kumdhibiti lakini shida ni kuwa hawa virusi wana fanya mutation ili kukwepa vipingamizi.