Je, ipo nia ya dhati kuukarabati uwanja wa Benjamin Mkapa kwa wakati?

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,164
7,941
Habari za mipango ya kufanyiwa ukarabati uwanja wa Benjamin Mkapa zimeanza kutolewa zaidi ya miezi 3 iliyopita. Najua serikali ina taratibu zake kuanzia kutafuta pesa hadi wazabuni wa kufanya kazi husika, ila naona kuna hali fulani ya kujikongoja na kujivuta kwenye suala hili. Zamani kabisa niliwahi kutoa angalizo kuwa Simba ijiandae kwa lolote kwenye hili suala. CAF walitoa mwongozo wa mambo yanayotakiwa kufanyiwa kazi mapema yawe yamekamilika (nadhani walitoa hadi mwezi wa 6 au 7). Wote tukiangalia uwanja unavyofanana sasa, kidogo unaweza kuona labda pitch tu ndiyo kidogo imeboreshwa lakini siyo sana, maeneo mengine yote hayajaguswa. Sina uhakika kama kile walichotaka kuwa kimefanyika kweli kimefanyiwa kazi.

Nikiangalia list ya vitu na maeneo yaliyotajwa yanaenda kufanyiwa kazi katika ukarabati huu, sioni ni jinsi gani haya yote yanaweza kufanyika ndani ya miezi 2 tena wakati huo huo uwanja ukiendelea kutumika. Najua Wachina wanaweza kufanya kazi usiku na mchana ila nina wasiwasi sana na hili suala. Pia nitashangaa sana CAF waendelee kuweka rehani maandaliizi ya kiwango cha juu ya uzinduzi na ratiba za mashindano kwa ukarabati huu wa dakika za lala salama.

Natoa tu angalizo maana huu wasiwasi wangu nimekuwa nautoa kwa miezi kadhaa sasa. Tusipokuwa makini, Tanzania itapoteza uenyeji wa uzinduzi wa mashindano haya.
 
CaF walishakagua uwanja kwa ajili ya michuano ya Afrika super cup na wakatoa mapendekezo ila utekelezaji umechelewa kutokana na viongozi kufikiria namna gani watapata na wao ulaji
Hayo mapendekezo yalitolewa miezi zaidi ya 4 iliyopita. Kwa jinsi CAF walivyopania mashindano haya yawe bora, kuna maamuzi magumu yanaweza kuja kufanyika yakatucost.
 
Habari za mipango ya kufanyiwa ukarabati uwanja wa Benjamin Mkapa zimeanza kutolewa zaidi ya miezi 3 iliyopita. Najua serikali ina taratibu zake kuanzia kutafuta pesa hadi wazabuni wa kufanya kazi husika, ila naona kuna hali fulani ya kujikongoja na kujivuta kwenye suala hili. Zamani kabisa niliwahi kutoa angalizo kuwa Simba ijiandae kwa lolote kwenye hili suala. CAF walitoa mwongozo wa mambo yanayotakiwa kufanyiwa kazi mapema yawe yamekamilika (nadhani walitoa hadi mwezi wa 6 au 7). Wote tukiangalia uwanja unavyofanana sasa, kidogo unaweza kuona labda pitch tu ndiyo kidogo imeboreshwa lakini siyo sana, maeneo mengine yote hayajaguswa. Sina uhakika kama kile walichotaka kuwa kimefanyika kweli kimefanyiwa kazi.

Nikiangalia list ya vitu na maeneo yaliyotajwa yanaenda kufanyiwa kazi katika ukarabati huu, sioni ni jinsi gani haya yote yanaweza kufanyika ndani ya miezi 2 tena wakati huo huo uwanja ukiendelea kutumika. Najua Wachina wanaweza kufanya kazi usiku na mchana ila nina wasiwasi sana na hili suala. Pia nitashangaa sana CAF waendelee kuweka rehani maandaliizi ya kiwango cha juu ya uzinduzi na ratiba za mashindano kwa ukarabati huu wa dakika za lala salama.

Natoa tu angalizo maana huu wasiwasi wangu nimekuwa nautoa kwa miezi kadhaa sasa. Tusipokuwa makini, Tanzania itapoteza uenyeji wa uzinduzi wa mashindano haya.
tatizo hamfanyi utafiti na mtatoavlawama za kijinga sasa kesho kandarasi ya ukarabati inatiwa sainibsijui utaweka wapi uso wako

Sent from my CPH2371 using JamiiForums mobile app
 
tatizo hamfanyi utafiti na mtatoavlawama za kijinga sasa kesho kandarasi ya ukarabati inatiwa sainibsijui utaweka wapi uso wako

Sent from my CPH2371 using JamiiForums mobile app
Kwa hiyo kumbe hata saini hazijatiwa kwa hiyo yale mapichapicha ya juzi yalikuwa ya nini? Na hata kama wamesaini bado hoja niliyoleta ipo pale pale. Soma uelewe.
 
CaF walishakagua uwanja kwa ajili ya michuano ya Afrika super cup na wakatoa mapendekezo ila utekelezaji umechelewa kutokana na viongozi kufikiria namna gani watapata na wao ulaji
DP world waliahidi kutoa pesa za ukarabati $100m, mlivyoanza kuchonga juu ya wao wasipewe bandari wakasusa.
 
DP world waliahidi kutoa pesa za ukarabati $100m, mlivyoanza kuchonga juu ya wao wasipewe bandari wakasusa.
Suala siyo pesa, suala ni muda uliobaki kabla ya uzinduzi. Labda kama maboresho mengine si lazima yakamilike ndani ya miezi 2 ijayo
 
Suala siyo pesa, suala ni muda uliobaki kabla ya uzinduzi. Labda kama maboresho mengine si lazima yakamilike ndani ya miezi 2 ijayo
Hawa dpw walikuwa watoe hii hela May, sasa mlipoanza kuwasagia kunguni wakasusa. Sasa hivi wameona bora wajenge misikiti mbeya huko
 
Hawa dpw walikuwa watoe hii hela May, sasa mlipoanza kuwasagia kunguni wakasusa. Sasa hivi wameona bora wajenge misikiti mbeya huko
Kwa matumizi ya nchi hii, hiyo hela ya uwanja tunayo wala hatuhitaji kuwategemea hao DPW. Labda uniambie suala hilo hatulipi kipaumbele
 
Kama SELIKALI ingekuwa serious uwanja ungefungiliwa hata Mwezi WA nane.

Maelekezo yalitoka miezi MITATU ILIYOPITA.

Na KIBAYA ZAIDI Simba na yanga zikapelekwa chamazi KUMALIZIKA LIGI.
 
Kama SELIKALI ingekuwa serious uwanja ungefungiliwa hata Mwezi WA nane.

Maelekezo yalitoka miezi MITATU ILIYOPITA.

Na KIBAYA ZAIDI Simba na yanga zikapelekwa chamazi KUMALIZIKA LIGI.
Tena nilishasahau hilo la Chamazi. Leo wanajitapa uwanja hautafungwa na wakati huo huo timu zinapelekwa Tanga!
 
Nimeona video ya Katibu Mkuu wa Wizara akisema ukarabati huu utachukua miezi 12. Pia anasema baada ya Simba Day uwanja utafungwa hadi October wakati siku ile ile Imani Kajula alimnukuhu kiongozi huyo huyo akisema uwanja hautafungwa. Ngoja tuone itakuwaje.

fimboyaasali, CAPO DELGADO
 
Kwa matumizi ya nchi hii, hiyo hela ya uwanja tunayo wala hatuhitaji kuwategemea hao DPW. Labda uniambie suala hilo hatulipi kipaumbele
Hiyo pesa muipate wapi, petroli yenyewe mnaagiza robo robo kwa sababu hamna dollar.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom