Je, Hizi Terorizing za Ziara za Kushtukiza, Hakutajenga Nidhamu ya Woga, Kutasaidia?!.

Nchi inaenda tu kwa one man show, Bunge halionyeshwi maana wako bize na one man show. Haya yanafanyika kwa sababu ya kisiasa kaka Pasco wala siyo mapenzi ya dhati kutoka mioyoni.Tusubiri it is matter of time wataelewa kuwa wanafanya Comedy
 
Ni afadhali kukosa nidhamu kuliko nidhamu ya woga. Nidhamu ya woga ni sawa na unafiki, lakini kwa vile watanzania wote ni wanafiki heri yako wewe ume declare kuwa bora kuwa mnafiki. Taifa la wanafiki haliendelei hata siku moja, tutapiga mark time miaka mitano.

Mfano siku ile Wilson Kabwe anatumbuliwa nikajua mikataba yote ya makusanyo ya mapato kwenye vyanzo vikuu kama stendi na masoko ya nchi nzima vitaangaliwa na kuwatumbua wengine. Cha ajabu utumbuaji uliishia pale kwa vile ulimlenga mtu na sio mfumo.

Ili kumsaidia raisi wetu tumpatie ushauri mzuri, yeye ni mkubwa sana kuhojiana na mkaguzi wa airport, angeangalia kazi inafanyikaje anaenda kujadiliana na waziri wake na mkuu wa airport anaelezwa procedure na kushauri njia bora. Yaani tuanze tena kukaguliwa mizigo yetu tukifika tunakoenda kwa ajili ya kumfurahisha mtu mmoja JPM. Ama kweli upele umepata mkunaji
Nyie wapinga kila kitu hamuishi., kwahiyo mtu akishuka na private jet Terminal 1 na unga wa kutosha apite tu??, Raisi akigundua tatizo aanze kukaa kikao na waziri amuelekeze machine Fulani haifanyi kazi kaiangalie,. Kuzunguka zunguka tu,kama Kuna tatizo mahali ni kutumbua hapo hapo,hakuna muda wa kupoteza.. Then nidhamu ni nidhamu tu,nyie ibatize majina ya uoga,sijui nini watumishi wa serikali walikuwa wamefika mahali pabaya,Hata wakijikojolea wakimuona raisi ni Sawa tu,hii itarudisha heshima ya nchi.Wengine tumeombea mtu kama Huyu miaka mingi sana,mnaompinga Kwa kila kitu mnazidi kupungua Kwa kasi kubwa na mwishoni mtachemka.
 
Nchi inaenda tu kwa one man show, Bunge halionyeshwi maana wako bize na one man show. Haya yanafanyika kwa sababu ya kisiasa kaka Pasco wala siyo mapenzi ya dhati kutoka mioyoni.Tusubiri it is matter of time wataelewa kuwa wanafanya Comedy
muda ni judge mzuri...miezi Sita ijayo tu
 
Maajabu ya Mussa....kwa nini asingempigia katibu Mkuu au waziri badala ya kuongea na junior staff tena kwenye makamera?mawaziri wake wanajisikiaje? Hoja ya lissu ya instrument za mawaziri inapata nguvu,hoja ya lissu kwamba nchi inaongozwa na mtu mmoja kama Mali yake binafsi inapata nguvu
Nyie wazungusha mikono vipi??,mpuuzi kama Lissu kaingiaje sasa?,mnapinga kila kitu tu,Kuna uozo sehemu nyingi ukianza kufata mlolongo wa manager,Mkurugenzi,waziri hatutafika,Kuna tatizo mahali litatue hapo hapo sipo sasa sasa kama mlizozoea za kuunda time kuchunguza
 
Tatizo one man show swali la kujiuliza je hamna mteule kwenye wizara hiyo??mpk muda huo ahusike yy kufumua madudu hali mteule wa eneo hilo yupooo?je hii inatoa taswira gani ?na je ni hao watendaji pekee ndo tuwawajibishe na kumwacha mteule wake?nadhani mmenielewa hapo.
 
Ni afadhali kukosa nidhamu kuliko nidhamu ya woga. Nidhamu ya woga ni sawa na unafiki, lakini kwa vile watanzania wote ni wanafiki heri yako wewe ume declare kuwa bora kuwa mnafiki. Taifa la wanafiki haliendelei hata siku moja, tutapiga mark time miaka mitano.

Mfano siku ile Wilson Kabwe anatumbuliwa nikajua mikataba yote ya makusanyo ya mapato kwenye vyanzo vikuu kama stendi na masoko ya nchi nzima vitaangaliwa na kuwatumbua wengine. Cha ajabu utumbuaji uliishia pale kwa vile ulimlenga mtu na sio mfumo.

Ili kumsaidia raisi wetu tumpatie ushauri mzuri, yeye ni mkubwa sana kuhojiana na mkaguzi wa airport, angeangalia kazi inafanyikaje anaenda kujadiliana na waziri wake na mkuu wa airport anaelezwa procedure na kushauri njia bora. Yaani tuanze tena kukaguliwa mizigo yetu tukifika tunakoenda kwa ajili ya kumfurahisha mtu mmoja JPM. Ama kweli upele umepata mkunaji
Hujaeleweka ndugu,
Hivi unapendekeza nchi iongozwe kwa law of the jungle, halafu, kwa uzembe huo, pengine taifa liangamie [rasilimali ziendelee kutoroshwa, na madhara mengine ya kiusalama]. Nadhani huna uzoefu wa kusafiri nje ya nchi; ukishuka JF Kennedy, Heathrow, Schiphol, and the like unakaguliwa, na ukiwa Mtanzania ndio kabisa utamulikwa hadi mapafuni. Tanzania tunakaguliwa hivyo kwa sababu inaaminika airports zetu ni JK style leadership (haphazard). Sasa Rais anapotuma the right message to the right personnel kuwa business as usual is no more wewe unaona ni kosa. Hutaki wageni wanaoingia nchini kupitia airports zetu (wengine wakiwa wamebeba 'unga') wakaguiwe! Pole ndugu. Nimlize hoja hii kwa kunukuu maneno ya JPM jana, '...hivi Watanzania nani kawaloga?'
 
Tatizo one man show swali la kujiuliza je hamna mteule kwenye wizara hiyo??mpk muda huo ahusike yy kufumua madudu hali mteule wa eneo hilo yupooo?je hii inatoa taswira gani ?na je ni hao watendaji pekee ndo tuwawajibishe na kumwacha mteule wake?nadhani mmenielewa hapo.
Uko sahihi,Kuna watu wanahusika kabla ya raisi,kumbuka watu walikuwa wanafanya kazi Kwa mazoea,pale bandarini ile flow meter inamhusu waziri,Mkurugenzi etc ukiwawajibisha kila mtu utafukuza ofisi nzima au wizara kila siku,pale airport hivyo hivyo,ila ukipiga mkwara una wa alert na wa juu wanaohusika kwamba wazembe,ni kama warning., ukifata mlolongo wa ngazi za uongozi hatufiki nchi ni kubwa sana na ina uozo mwingi sana,ndo maana China wanapigwa risasi hadharani kama warning,angalia speed yao
 
Tatizo one man show swali la kujiuliza je hamna mteule kwenye wizara hiyo??mpk muda huo ahusike yy kufumua madudu hali mteule wa eneo hilo yupooo?je hii inatoa taswira gani ?na je ni hao watendaji pekee ndo tuwawajibishe na kumwacha mteule wake?nadhani mmenielewa hapo.
This is governance software revamp strtegy ndugu. We are moving away from JK leadership style (Masalia?).
 
Kama umenielewa nimesema nataka raisi Magufuli aweke misingi ambayo hata akikaa ofisini au yuko nyumbani na mama yetu Janet, huku chini kila mtu anatimiza wajibu. Asiye timiza wajibu na mwenye nidhamu ya woga anatumbuliwa huko huko na mkubwa wake. Hii itamsaidia sana raisi na misingi hii iko kwenye katiba ya Warioba
.... anachokifanya Rais ndio njia ya kufikia huko usemko/uwazako.
 
Heshima yako Pascal - hivi unakumbuka modus operandi ya Lowassa alipokuwa WAZIRI MKUU, alikuwa anatimua watu on the spot! Hakuwa na huruma hata kidogo - Pasco kasahau udikteita wa Lowassa!!

Lowassa aliwahi kumwachisha kazi mama wa watu ambaye alikuwa mkurugenzi wa Wilaya huko Arusha bila sababu za msingi tena kwenye mkutano wa adhara.

Dk. Magufuli ni. Mkali lakini at least ana UTU sana, we unafikiri uozo aliyougundua jana pale Uwanja wa ndege si angetimua wafanya kazi karibu wote kuanzia ma operators mpaka Mkurugenzi mkuu possibly na Waziri, sasa nini kilicho tokea ni nini Magufuli wa watu kawapa onyo tu, je angekuwa Lowassa angefanya nini? Jibu analo.

Leo nilikuangalia kwenye kipindi cha asubuhi cha StarTV you are unquestionably an inyelligent man lakini linapokuja suala la Dk. Magufuli una kawaida ya kupoteza dira kabisa! Tatizo lako huko so obsessed na Magufuli as a person mpaka unafikia hatua ya kujisahau kabisa - this is not healthy at all - personally I don't like your stance, sio kwamba nakuonea nataka kuwa mkweli - UMEZIDI.

We fikiria Mpaka muongoza kipidi na wasemaji wenzako uliyo kuwa nao kwenye studio wafikie hatua ya kukwambia kwamba usijaribu ku derail mada kwa kutumbukiza masuala ya Dk. Magufuli ujishtukii tu???

Mantra yako ya kusema kila upatapo jukwaa kwamba Dk. Magufuli anafanya the right thing using wrong method hatutaki kayasikia sisi, tuko vitani we subiri 2020 kama mtashinda basi ushauri wako mpatie Lowassa, sitaki kusema mengi hidipo kuwa nakushauri kwa nia njema tu kwamba jirekebishe - nyinyi si wajomba wa Dk.Magufuli kwa nini hutaki kumuunga mkono katika crusade zake zilizo tukuka au ukamkosoa kwa upendo bila ya ku resort kwenye stunt za media just to get even!!
 
.... anachokifanya Rais ndio njia ya kufikia huko usemko/uwazako.
Bro watu wanapinga tu mpaka Kuna wakati huwa najiuliza kama ni watanzania au wahamiaji.,Kuna machine za kuscan mbovu,ila zipo bado naona mtu humu anahoji kukaguliwa akifika home sio sahihi,hajui Kuna wabeba unga nk,halafu wanaleta siasa za JK za kuoneana aibu,sijui mpigie simu manager airport atoe maelezo Kwa Mkurugenzi,then mkuu wa mkoa.. Hizo zama zimekwisha Hapa Kazi Tu
 
Naam dadangu, aidha watu wana nidhamu au hawana. Na hakuna kitu kama "nidhamu ya woga". Ukiwa mtumishi wa umma ni lazima uogope; uogope kuvunja sheria, uogope kutumia madaraka yako vibaya, uogope kukutwa unavuruga! Unatakiwa utende kazi kwa kujiamini, kwa weledi na kwa ufanisi unaotakiwa kutokana na nafasi yako. Sasa bosi wako akitokea na kukuta umekunja nne ukaruka juu na kujimwagia chai na kuanza kujifanya unafanya kazi manake ni kuwa hukuwa mwoga in the first place! Ungekuwa unaogopa ungekuwa huna wasiwasi. Hivyo, woga wa kinidhamu unahitajika na viongozi waendelee kuwashtukiza na kuwatumbua hasa kama watumishi hawawaogopi mabosi wao au viongozi wao wajuu.

Tulidekezwa mno hadi tukadeka na kuamini tunatakiwa kudekezwa.
wee siku hizi umeisha kabisa. Tangu ujiunge na dini yenu ya washangiliaji kichwani umebaki mtupu
 
h
Wanabodi,

Naendelea na zile mada zangu za kusisitiza ukweli, ukiwa mkweli, ukweli utakuweka huru!. Hili ni swali, "Jee Hizi Terorizing za Ziara za Kushtukiza, Hakutajenga Nidhamu ya Woga?!. Jee, Kutasaidia?!.

Hiki nilichokishuhudia leo Eapoti jamani sio!. Tufike mahali watu wanaommudu, wamshauri, that is not the right way.

Leo nimemshuhudia ngosha pale eapoti anavyo waterorize wale maofisa pale!, tangu lini domestic arrival wanapita kwenye scanner?!, akashauri eti kwa nini nao wasizungukie pale kwenye scanner za depature ndipo waingie nchini!, kiukweli watu wenye akili zao, wanaanza kumuona huyu jamaa kama sio!, kiukweli ule ni terorising!, nitamshauri yule kaimu, vitu vingine viishie kwenye habari tuu na sio kuleta kipindi maalum wakidhani wanamjenga kumbe ndio wana mdhalilisha bure!, na jamaa anavyopenda masifa mbele ya kamera, kiukweli huu ushamba wa kabila langu sometimes unanchekesha!.

Nasisitiza naunga mkono kinachofanyika kuisafisha serikali yetu na madudu yaliyokithiri, the man is doing the right thing but in a wrong way!. Every human being needs dignity!. Pomoja na yote jamani, ka human dignity kawepo, na sio huu udhalilishaji mbele ya kamera halafu wanausha kipindi maalum!. Please wajemeni!.

Namshukuru sana Mzee wa kutumbua, leo kashtukiza lakini hakutumbua zile za papo kwa papo, labda sauti zetu zinaanza kusikika and to make sense, ila kufuatia nidhamu ya woga na kujikombakomba, mnaweza kushuhudia utumbuaji majipu ukifuatia ziaa hii pale Eapoti leo Jumamosi, au siku ya Jumatatu, kisa jamaa kapita pale kashuhudia na kadanyanywa!.

Tanzania inachohitaji sasa sio one man show, na movie za ze comedy!, tunahitaji kujenga mifumo, systems, kama hakuna scanner kwenye arrival zote duniani, bali kuna declaration forms, kila mzigo unaofikia arrival ulikuwa scanned kule ulikotoka na ukawa cleared ni majangili mataahira tuu ndio watauwa tembo wetu kisha wabebe pembe za ndovu kuingia nazo arrival! wakati mipaka yetu yote ni very porous!. Vitalu vyote vya uwindani vina private air strips midege inaingia na kutua na kujichukulia chochote na kuishia zao juu kwa juu, kwa kisingizio ni vitalu vya uwindaji!, ni kichaa tuu mwenye uwezo wa kutua porini kubeba nyara na kuja nazo arrival!.

Kila ndege kabla haijaingia Tanzania lazima ipate clearance toka TCAA, tuweke watu kwenye every private air stripe na kujenga mfumo toka TCAA kuwa hakuna ndege itakuwa cleared kutua kwenye shamba la bibi, bila bibi kutuma mjukuu ashuhudie hiyo ndege imeleta nini, na hakuna clearance kupaa hadi mjukuu athibitishe imebeba nini!.

Kiukweli hii ya leo kwangu ilikuwa Ze Comedy!, hatuwezi kwenda hivi jamani!.

Namalizia kwa lile swali la msingi, "Jee Hizi Terorizing za Ziara za Kushtukiza, Hakutajenga Nidhamu ya Woga, Kutasaidia?!".

Nawatakia Jumamosi Njema.

Pasco
heri nidhamu ya woga kuliko hali ya uzembe kupiga dili kukubalika kama ndio sawa.
 
Naam dadangu, aidha watu wana nidhamu au hawana. Na hakuna kitu kama "nidhamu ya woga". Ukiwa mtumishi wa umma ni lazima uogope; uogope kuvunja sheria, uogope kutumia madaraka yako vibaya, uogope kukutwa unavuruga! Unatakiwa utende kazi kwa kujiamini, kwa weledi na kwa ufanisi unaotakiwa kutokana na nafasi yako. Sasa bosi wako akitokea na kukuta umekunja nne ukaruka juu na kujimwagia chai na kuanza kujifanya unafanya kazi manake ni kuwa hukuwa mwoga in the first place! Ungekuwa unaogopa ungekuwa huna wasiwasi. Hivyo, woga wa kinidhamu unahitajika na viongozi waendelee kuwashtukiza na kuwatumbua hasa kama watumishi hawawaogopi mabosi wao au viongozi wao wajuu.

Tulidekezwa mno hadi tukadeka na kuamini tunatakiwa kudekezwa.
Manakijiji naona wewe na mimi tunakubaliana na mambo mengi siku hizi kumbe ni mzalendo wa kweli uanchukia ufisadi kama mimk
 
Nyie wapinga kila kitu hamuishi., kwahiyo mtu akishuka na private jet Terminal 1 na unga wa kutosha apite tu??, Raisi akigundua tatizo aanze kukaa kikao na waziri amuelekeze machine Fulani haifanyi kazi kaiangalie,. Kuzunguka zunguka tu,kama Kuna tatizo mahali ni kutumbua hapo hapo,hakuna muda wa kupoteza.. Then nidhamu ni nidhamu tu,nyie ibatize majina ya uoga,sijui nini watumishi wa serikali walikuwa wamefika mahali pabaya,Hata wakijikojolea wakimuona raisi ni Sawa tu,hii itarudisha heshima ya nchi.Wengine tumeombea mtu kama Huyu miaka mingi sana,mnaompinga Kwa kila kitu mnazidi kupungua Kwa kasi kubwa na mwishoni mtachemka.
Tatizo mkienda shule za kata huwa mnaenda kusomea ujinga ndio maana saizi mnasema maisha bila sukari yanawezekana na mtasema maisha bila elimu yanawezekana soon. Raisi anayo haki ya kufanya ziara kila sehemu ya nchi hii, lakini akimaliza ziara lazima aweke mfumo sawa isaidie sekta nzima. Hauwezi kuweka mfumo kwa kuongea na ATTENDANT mbele ya kamera. Magufuli ni mkemia na mathematics, anahitaji kujifunza vitu vingine toka kwa wataalam na washauri na sio kuamrisha kitu bila kuwa na background yake.
 
Wewe una utaalamu gani wa Management? Au ni wataalamu gani hao.Kwenye theory ipi ya management? Unaona sasa....

Hicho kitabu "In Search of Excellence ,A lesson From Americas Best-Run Companies" Cha Robert Waterman na Tom kiliandikwa karibia miongo mitatu iliyopita,1980s.

Nimekisoma na wewe ni aidha hujakisoma au umekisoma hujakielewa.

Yeye Mwenyewe alisema System and structures are the only tools for organizational Change. Acha uongo kisome tena au kama huna nakala nikuazime ukisome tena.Hakuna anachofanya Magufuli kinachofanana na hicho au anafanya in a twisted way

Nirudi kwenye mada sasa,

Mkuu Pasco,

Jana niliwaambia kwenye ule uzi waliokuja nao kwa Mbwembwe wakasema nina wivu ninamkejeli Rais

Hakuna Leadership Style ya Namna hii iliyowahi kufanikiwa Duniani

Hata Kim Jong-Un wa Korea ya Kaskazini anafanya vizuri zaidi ya hivi anavyofanya

Rais anafanya kazi ya Meneja wa uwanja wa Ndege au Security Manager

Tunahitaji atengeneze Chain of accountability.Ndio mfumo wa kitaasisi

Anavyofanya hivi akiwa hayupo watu wataanza kumtafuta Magufuli mwingine

Cha ajabu kuna wasomi(Sijui kama ni wasomi wenye viwango vya ukwelikweli) wanashabikia kama mazuzu.Hawana tofauti na wale walioenda Loliondo na wale walioliwa kwenye Upatu wa DECI

Rais anatangaza kutoa amri ya kuzuia kuagiza sukari wanashangilia "weweeee ...wewe ndio Jembe letu.Hakuna kama wewe.Yaani weee ndio Sokoine uliyefufuka"

Baada ya Mwezi Sukari hakuna au iliyopo inauzwa 3000-4000 .Wanakaa kimya

Rais anatoa Tamko kuwa "tutaagiza sukari Tani 70,000 kutoka nje .

Watu walewale wanashangilia weweeee.Wewe ndio mkombozi wetu,Wewe ni mchapakazi .Kweli nchi ilikua imeoza sasa unawanyoosha.Wewe huna tofauti na Nyerere"

Hawa ndio watakaokushambulia katika huu uzi

Kuna ule utafiti wa Nottingham University kuwa tu vinara wa unafiki Duniani bado unaendeleea kudhihirika

Kuna ule wa PEW Research kuwa Tunaongoza kwa kuamini katika Miujiza,Ushirikina duniani.Siwezi kuupinga maana hata hapa tunaamini katika Muujiza wa Magufuli kama Magufuli kushinda hata muujiza ambao ungeletwa na Rasimu ya Katiba ya Warioba au hata chain of accountability ambayo ingejengwa.Tunaamini muujiza wa Rais kuwa kila mahali kufanya kila shughuli

Kwa fikra na imani hizi kwanini tusichanjwe chale kwa waganga wa kienyeji au kutapeliwa makanisani.Kwanini tusifurike Loliondo na kuachana na tabibu za kisayansi mahospitalini(Hata Magufuli aliamini na akapata uzoefu kule na anapita njia ile ile ya Babu kwa kuwa watanzania ni wale wale walofurika kwa babu),Kwa nini DECI wasivune fedha nyingi kwetu ?

Nyerere alisema adui mkubwa kwetu ni ujinga.Ukimshinda tu umeshinda umaskini,Maradhi na hata ufisadi maana maadili yatakuwepo na uwezo wa kuwajibishana utakuwepo kwa kuwa hata ethics and principles of good governance zitakuwepo.

Ukute Rais kafanya tukio lile kupotezea sekeseke aliloliunda mwenyewe la Sukari na sakata la Lugumi. Kama kawaida watu wapo "Weweee huyu ndio Jembe,Hakuna kama wewe.UKAWA sidhani kama wangeweza hivi"

Halafu Sukari ni 3000 ,Asubuhi kama ya Leo wanaamka alfajiri zaidi ili kuikwepa familia na kujifanya kuwahi kwenye shughuli.
Umekariri ukiwa mpinzani ni kurusha makombora tu...... tena yaliyojaa dhihaka! ww kwa uelewa' wako unadhani mfumo wa utendaji haukuwepo? acheni kejeli za nitoke vp......
. kuna ubaya gani anko Magu.... kupita na kukagua airport kupita Kwake mapungufu yamebainika waziri usika atapita na kuweka sawa ..... miaka mitano( 5×12=60) sawa na miezi sitini (60-5=55) jamaa bado ana miezi 55 mifumo mipya itatengenezwa tu..... kwa sasa wacha mindset za watendaji wa serikali zibadirishwe.....After all ningemshangaa anko Magu apite airport bila kuchungulia chungulia pale..... wakati pamekuwa na malalamiko mengi ...ni sawa na baba asikie kelele jikoni ashindwe kwenda kangalia....... kunani kisa jikoni kunamuhusu mama!!!..... huo utakuwa uchawi...... hapana ubishi kwamba nchi hii inapita kipindi cha mpito .... swala la sukari ni la muda tu...... lkn serekali imejipanga....in a along run basis.... tatizo hili halitojirudia..... kwa kuongeza uzalishaji wa ndani na kuondoa miungu watu waliodominate soko hilo
 
Hakuna muda wa siasa siasa,mwaka mzima ni ubabe kwanza watu waogope.,China imefika ilipo Kwa chama kimoja na Sera za kibabe,tena wale mtumishi wa una ananyongwa,ukianza mambo ya wataalamu,washauri nk unachelewa,Kuna tatizo mahali Hata kama umetoka Ug Kwa Museveni piga mkwara hapo hapo no delay
 
Kama umenielewa nimesema nataka raisi Magufuli aweke misingi ambayo hata akikaa ofisini au yuko nyumbani na mama yetu Janet, huku chini kila mtu anatimiza wajibu. Asiye timiza wajibu na mwenye nidhamu ya woga anatumbuliwa huko huko na mkubwa wake. Hii itamsaidia sana raisi na misingi hii iko kwenye katiba ya Warioba
hicho kitu ccm hawawezifanya, ukiweka mifumo maana yake utaziba mianya ya ufisadi automatically utaiua ccm, survival ya ccm ni loop holes
 
Back
Top Bottom