Usemayo ni kweli kabisa lakini mimi binafsi naamini kuwa tuna wajibu
wa kuwaelimisha hawa ndugu zetu.
Katika kufanya hivyo huenda tukaiepusha nchi yetu na hili janga ambalo
si muda mrefu litakumba jamii yetu.
Wewe Mohammed Said huna lolote la maana unaloweza kuisaidia jamii yako. Unachotaka ni kuonekana wa maana mbele ya watu wasiofahamu propaganda na kupata sifa za kijinga zisizo na manufaa.
Umekuwa mwingi wa kuandika makala za Nyerere alifanya hili baya kwa Waislam, Serikali inawanyima hiki Waislam....hauishi kutupa lawama kwa huyu na yule ili mradi tu kushindwa kwenu iwe lawama ya mtu mwingine.
Unapenda mada za kukupa sifa na umaarufu mbele za watu japo huzingatii kuwa kusifiwa na watu wasio na ufahamu wa kutosha juu ya jambo unaloongea hakukupi credits mbele ya wasomi na wenye ufahamu. Ni sawa na watu wa kijijini wasiojua Kiingereza wakusifie kuwa unaongea Kiingereza safi ilhal wao hawakijui. Sasa hujiulizi wanakusifia kwa kukupima kwa kipimo gani, unachojali wewe ni sifa.
Makala zako zinawafanya Waislam wanaocheza bao msikitini saa zote waamini kuwa watoto wao wanafeli shuleni sababu ya Kanisa Katoliki. Unahubiri yale wanayopenda kusikia, ukisahau kuwaambia kuwa kitu pekee ambacho serikali inaweza kumfanyia mwanafunzi ni kumpa darasa na mwalimu lkn si kumbadilishia ubongo na kumpa mpya wa Kikatoliki.
Historia ya nchi yetu unaijua (japo unapenda kuipindisha kwa manufaa yako) na historia ya dini hizi mbili hapa Tanzania unaijua. Kuna wakati upotoshaji wenu unalenga kuonesha ubaya wa Nyerere katika sehemu ambazo alipaswa kushukuriwa na nyie msio na SHUKRANI.
Mmoja wenu siku fulani hapa hapa JF aliwahi kutuandikia utumbo kuwa Wakristo walipendelewa na Nyerere kielimu kwani hata Scholarship za kwenda kusoma
'kwenye nchi za maana' (USA, UK,German n.k) walipewa wao (Wakristo) na Waislam waliishia kupata zile za kwenda kwenye nchi zisizo na tija kama China, Uturuki n.k.
Hapo utaona namna fulani ya UTAAHIRA wa mawazo tangu kwenye mwanzo wa hoja yenyewe. Kumbe hata mnafahamu kuwa kuna NCHI ZA MAANA na zilizopiga hatua. Kinachonishangaza ni kutojiuliza kwa nini zimekuwa za maana. Kwa hiyo Waislam wanatamani kwenda German kusoma, ikiwa na maana ya kujifunza toka kwa Wajerumani ambao kufanikiwa kwao kunatokana na yale wanayoyaamini.
Mohammed Said unayetafuta sifa miongoni mwa Waislam wasio na uelewa, unasahau kuwaambia waislam wasioelewa kuwa, mara baada ya ukoloni, hizo Scholarship zilikuwa zinatolewa na wakoloni hao hao ambao tulikuwa nao hapa wakijenga Makanisa na Shule ambazo waislamu hawakupenda kuingia. Agents wale wale wa Ukoloni (Missionaries) ndio waliokuwa na uelewa na Africa na ndio waliokuwa wakitoa mapendekezo kwa serikali zao kuhusu misaada ya maendeleo huko walikotoka.
Serikali ya Ujerumani inatoa Scholarship kwa vijana 20 kusomea jambo fulani huko Ujerumani, na sharti muambata ni kwamba Barua zao za utambulisho zipitie kwa PAROKO wa Parokia anayotoka na kugongwa muhuri wa Askofu wa jimbo husika, Nyerere alitakiwa azikatae kwa kuwa Waislam hawawezi kwenda?
Zinatoka Scholarship toka serikali ya China, hizi hazina masharti, Nyerere kwa busara kwamba kwa kutumia busara, anaamua kupeleka Waislam wengi huko kwa kuwa anajua Wakristo tayari wana fursa kwenye nchi zingine, napo Mohammed Said na wenzako mnasema mnapelekwa kwenye nchi zisizo na tija. Sasa mfanyiwe nini?
Mohammed Said (mnafiki), unasahau kuwaambia Waislam wasio na uelewa kuwa, hata hizo zisizo na masharti zilikuwa ngumu kwa Waislam kupewa kwa sababu ili uende lazima uwe na vigezo fulani vya elimu ambavyo tayari wengi mlikuwa hamna kwa kuwa hamkuwa tayari kusoma kwenye shule za Mission. Huu ni UPUUZI kuwafundisha watu.
Mohammed Said na wenzake, hawawaelezi waislam wao kuwa kukua kwa jamii ya Kikristo kunatokana na character ya Mkoloni aliyeleta dini yao kuwajenga kwa namna hiyo unayowaona leo wako na kwamba aliyeleta Uislam hata yeye mwenyewe huko alikotoka hamna msisitizo wa elimu kama ilivyo kwa walioleta Ukristo.
Amini nawaambia wakuu wa JF, kuna watoto wa kiislam ambao hawahudhurii madarasani tangu shule za msingi, baba zao wanayajua hayo na still wakifeli wapo mstari wa mbele kulaumu kuwa wamefelishwa. Hii inatokana na mahubiri ya Mohammed Said na wenzake. Wanawafanya watoto waamini kuwa, watoto wa Wakatoliki hawasomi kama wao lkn mitihani yao inasahihishwa
beautifully kwa hiyo wanafaulu.
Mifano ya ujinga wa MAHUBIRI ya Mohammed Said unaweza kuonekana juzi tu hapa kwenye shule ya Sekondari ya Ndanda. Wanafunzi wa Kiislam wanagoma kusoma kwa kisingizio cha kunyanyaswa na uongozi wa shule. Hoja yao ya msingi ilikuwa Shuleni kuna Kanisa lkn wao wanakatazwa kujenga msikiti shuleni.
Kwa akili ya kawaida isiyotaka uchunguzi unaweza kuona pana hoja, lkn ukiirejea historia ya shule utaona ni upuuzi. Hiyo shule ilijengwa na Kanisa hilo hilo wanalolipinga. Cha pili utagundua tu kutumiwa kwa wanafunzi hao na watu fulani kutokana na maelezo yao na namna ya wanafunzi wenyewe (ni wale watoto wasio na mahudhurio mazuri darasani na hata hiyo dini yao yenyewe sio wahudhuriaji)
Mohammed Said na wenzake, wako bize kuelezea yaliyotokea Mwembechai, lkn hamna anayeelezea ni nini chanzo cha polisi kufika pale na je ilikuwa ni sahihi kwa wao kupanda majukwaani kukashifu imani za wenzao.
Mohammed Said ni aina ya Waislamu wanaoamini kuwa Waislam wana haki ya kusema wanachojisikia kuhusu Yesu lkn wasiambiwe ukosoaji wowote kuhusu Mohammad (Mtume) Kwao hao matukano kwa wengine yanaitwa hoja ila nukuu yoyote dhidi yao inaitwa KUFURU dhidi ya mtume wao.
Kuna ujinga mwingi katika mahubiri ya Mohammed Said ambayo yanachosha kwa kweli. Lakini ni nini kinachompa Mohammed Said msukumo wa kuongea pumba kwa nguvu?
Ni ule ukweli kwamba, Uislam hauna uongozi wenye kutambulika. Hii inatoa fursa ya mtu yeyote kuongea au kufanya jambo la kijinga kabisa na kusema
'Haya ni matakwa ya Waislam'. Hakuna msemaji wa dini hii wala hakuna baraza la pamoja. Leo Ponda anasimama na kusema hili na hili ni maoni ya Waislam, kesho anasimama mwingine na kusema hayo ni maoni ya Mawahabi ambao ni wakorofi, keshokutwa anasimama Ponda na kusema Mufti ni Kaffir, ili mradi Uislam umekuwa nyumba ya Kambale ambapo familia nzima ina ndevu hajulikani nani baba nani binti.
Mohammed Said na wenzake wangepaswa kujiuliza ni kwa nini Muarabu hakuacha shule (za aina hii tunayogombea) na kwa nini nchi za kiarabu hazitoi misaada ya kielimu na ufadhili mwingine wa maana zaidi ya kuishia kutoa Mabillioni ya fedha za FATWA kwa kushabikia mauaji ya mtu aliyekosoa Quran.
Mohammed Shosi anasema Serikali haipendi kukosolewa, lkn anasahau kuwa hata imani yake inayomwongoza hapa haipendi kukosolewa na ndio maana leo ulimwengu wa Kiislam umeweka dau la
$3.3m kumuua Sulman Rushdie.
Mna mambo mengi ya kuwaeleza Waislam wa hali ya chini badala ya kuawafanya waamini kisicho cha kweli
1. Uke wenza ni kikwazo cha malezi ya familia
2. Uzazi wa mapango ni msingi wa malezi na utunzaji bora wa familia
3. Elimu kwa mtoto haiishii darasani bali hadi nyumbani. Mzazi afuatilie maendeleo ya mtoto wake shuleni
4. Dhiki si mpango wa Mungu kwa mwanadamu kwa hiyo familia ijibidiishe (Waislam wengi wanaamini kuwa ukiwa fukara ndio unaenda peponi)
5. Imani za kishirikina zinarudisha nyuma maendeleo n.k
Kwa waislamu mnaohisi mnaonewa, jifunzeni kwa waislam wenzenu walioenda shule kwa jinsi wanavyokazania elimu kwa watoto wao na sio kujiunga na kambi za manung'uniko za Mohammed Said anayefadhiliwa na watu wa nje kusema yasiyo na maana kwenu.