Je hata humu watu waandamane?

Je hata humu watu waandamane?

Umeanza vibaya jibu lako.
Hebu soma ufunguzi wa kauli yako.

Namna hii haipatikani tija na mjadala unakosa umakini.
Kukosolewa ni kitu asichoweza kukiepuka yeyote yule anaeingia katika mjadala.

Mimi hilo halijapata kunitisha.
Nina uwezo wa kusimama na yeyote kwa hoja na nimefanya hivyo kwingi tu.

Isome historia ya Waislam na nini kilitokea baada ya uhuru kupatikana.
Kwa muhtasari nimeeleza katika post ambayo hapa JF imeondolewa.

Mada hii kwa namna tofauti nimeizungumza kwingi duniani na kwa hakika imeleta
changamoto kiasi nitakufahamisha kuwa nilipomaliza kuiwasilisha pale ZMO Berlin
niliombwa nikazungumze University of Humburg.

Nyinyi ndiyo mnatishika na historia hii.

Kwa wenzetu ni kitu kipya ambacho watafiti
wa historia ya Afrika wanathamini.

Insha Allah natayarisha mada "The Reversion of History and the Dangers of Fallacy."

Mungu akipenda nitaiweka hapa JF kuonyesha maradhi yanayowasibu watu wanapoletewa
mashujaa wapya katika historia iliyofutwa.

Angalia hofu na hamaki iliyoingia baada ya kubainika kuwa si Nyerere aliyeasisi TANU bali
ni rafiki yake Abdulwahid Sykes.

Hadi leo bado watu wamechanganyikiwa hawajui la kufanya.

Sheikh Mohamed Said Ahsante sana kwa darasa unalolitoa humu ndani. naona wamechanganyikiwa sasa ati wanaleta habari za yesu...... Na hiyo mada uliyoitaja hapo juu tunaisubiri kwa hamu. Ama kweli, ukweli ukidhihiri uongo hujitenga! Uongo haudumu. wameshatudanganya sana hawa watu kuhusu historia ya nchi hii, lakini sasa umeshawaacha uchi.
muungwana akivuliwa nguo huchutama sasa naona wao wanakimbia wanazidi kujifedhehasha. Bravo sheikh! endelea kutoa darasa.
 
Hoja inajengwaje kistaarabu? Kwa kuanza na Takbir au?

Sikutegemea ujibu anyway kwa kuwa umekosolewa. Ila ushauri wangu ni kwamba, tumia muda wako vizuri kuifundisha jamii ya Waislam isiyo na elimu na sio kuipotosha.

Maneno meengi ya kumsingizia fulani kuwa anakukwamisha si tija wala hoja mfumbuzi ya taabu zako. Kushindwa kwenu kunaanzia kwenye ngazi ya familia, acha lawama kwa watu wengine

las uko juu sana.napenda hoja zako,kila sku wanalalamika tuuuuu.wanaker
 
Sio kwamba umeshindwa kumusoma mkuu La Mas Bobos, umeshindwa kujibu hoja nzito za Bobos kwa sababu wewe umezowea kupokea sifa za kijinga kutoka kwa wajinga wanaopokea mahubiri yako ya kichawi na fitna dhidi ya watu wengine. Mohamedi Saidi kubali kuwa wewe ni muovu na wala huwatakii mema jamii ya islam. Huna tofauti na shetani, na kwa kifupi wewe ni shetani mwenyewe. Huishi visingizio na fitna. Kaa tulia soma tena andiko la Bobos, jibu hoja hizo na ukome kujiita kuwa wewe nini msomi kwani huna cha usomi wowote zaidi ya uganga njaa tu, shame on you old fool!

Like 1000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000
 
Sheikh Mohamed Said Ahsante sana kwa darasa unalolitoa humu ndani. naona wamechanganyikiwa sasa ati wanaleta habari za yesu...... Na hiyo mada uliyoitaja hapo juu tunaisubiri kwa hamu. Ama kweli, ukweli ukidhihiri uongo hujitenga! Uongo haudumu. wameshatudanganya sana hawa watu kuhusu historia ya nchi hii, lakini sasa umeshawaacha uchi.
muungwana akivuliwa nguo huchutama sasa naona wao wanakimbia wanazidi kujifedhehasha. Bravo sheikh! endelea kutoa darasa.

Marehemu Prof. Haroun Othman si mtu mjinga.

Alipokisoma kitabu changu na kugundua mengi ambayo kwake yalikuwa
mapya aliathirika sana.

Khasa kuwa harakati za kuwakusanya wananchi kuwa kitu kimoja chini ya African
Association ilianzwa na baba yake Abdulwahid Sykes Mzee Kleist mwaka wa 1929.

Pili aliposoma kwa ushahidi wa nyaraka kuwa Abdu Sykes alikichukua chama alichoasisi
baba yake na kuanza mipango ya kuuunda TANU mwaka 1950.

Tatu kuwa hata ile hotuba iliyosomwa na Nyerere UNO 1955 chanzo chake kilikuwa TAA Political Sub
Committee katibu akiwa Abdu Sykes.

TAA Political Sub Commiittee ndiyo iliyoandika hotuba ile waandishi wakiwa Sheikh Hassan bin Amir,
Abdulwahid Sykes, Hamza Mwapachu, Stephen Mhando, Dr Vedasto Kyaruzi na Said Chaurembo.

Lakini zito kwake Prof. Haroub ni pale aliposoma njama za Nyerere katika kupiga vita historia hii na kuhujumu
juhudi za Waislam katika kujenga taasisi za elimu.

Prof. Haroub alipitia ushahidi wote nilioweka katika kitabu na kama haitoshi alikwenda kuzungumza na Ahmed
Rashad Ali rafiki yake Abdulwahid Sykes toka 1939 kutafuta ukweli wa maneno yangu.

Huko nako alishibishwa.

Siku nilipokutananae uso kwa uso Prof. Haroub alikuwa kapwelewa kwani kwake yeye Nyerere alikuwa kila kitu.
Kiongozi muadilifu atoae haki kwa raia wake wote bila ubaguzi, hana udini nk. na nk.

Aliniuliza mengi na mimi nilimjibu kila swali lake alilouliza.

Kwa mara ya kwanza mimi ambaye nilikuwa mwanafunzi wake Mlimani akinisomesha Theories of Development
sasa nikawa namsomesha Prof. wangu historia ya kweli ya Tanganyika.

Prof. Haroub alikuwa kama wengi walivyokuwa - hawakumjua Nyerere wala historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.
Nilikuwa nimemfungulia mlango ambao hakuwahi kupita hata siku moja.

Sishangai hapa JF ninaposoma kejeli na matusi.
Hakika hawa wenzetu wana haki ya kupata mshtuko.

Kuja kujua ukweli baada ya miaka 50 si jambo dogo.
Inahitaji wapewe muda wasafishe bongo zao ili ziwe tayari kupokea elimu mpya.

Baada ya miaka 50 Rais Kikwete anatoa nishani kwa Abdulwahid Sykes na Ally Sykes.

Kwanini hakutoa nishani kwa baba yao Kleist Sykes au kwa Hamza Mwapachu, Stephen Mhando, Zubeir Mtemvu, Sheikh Hassan bin Amir na wengine hili ni swali linalohitaji majibu.

Historia hii bado inahitaji utafiti zaidi na iandikwe.
 
Like 1000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000000

Nayapokea matusi yako kwa masikitiko.

Maalim wangu wa madras Sheikh Haruna (Mungu amuweke pema) alinifunza adabu ya mnakasha (yaani majadiliano).
Akasema ikiwa mwenzio katika majadiliano atatoa matusi basi sitisha majadiliano na yeye ili apate kutulizana.

Akitulia manaweza mkaendelea.

Ukiendelea na mjadala wakati mwenzio ameghadhibika kitachufuata ni kuwa atakutoa ngeu.
Wakati nikisoma ilm hii ni kijana mdogo wala haya mambo ya computer bado kabisa.

Humu hutoweza kunitoa ngeu lakini nasitisha mjadala na wewe sitakujibu kwa kufuata usia wa maalim
wangu.
 
Marehemu Prof. Haroun Othman si mtu mjinga.

Alipokisoma kitabu changu na kugundua mengi ambayo kwake yalikuwa
mapya aliathirika sana.

Khasa kuwa harakati za kuwakusanya wananchi kuwa kitu kimoja chini ya African
Association ilianzwa na baba yake Abdulwahid Sykes Mzee Kleist mwaka wa 1929.

Pili aliposoma kwa ushahidi wa nyaraka kuwa Abdu Sykes alikichukua chama alichoasisi
baba yake na kuanza mipango ya kuuunda TANU mwaka 1950.

Tatu kuwa hata ile hotuba iliyosomwa na Nyerere UNO 1955 chanzo chake kilikuwa TAA Political Sub
Committee katibu akiwa Abdu Sykes.

TAA Political Sub Commiittee ndiyo iliyoandika hotuba ile waandishi wakiwa Sheikh Hassan bin Amir,
Abdulwahid Sykes, Hamza Mwapachu, Stephen Mhando, Dr Vedasto Kyaruzi na Said Chaurembo.

Lakini zito kwake Prof. Haroub ni pale aliposoma njama za Nyerere katika kupiga vita historia hii na kuhujumu
juhudi za Waislam katika kujenga taasisi za elimu.

Prof. Haroub alipitia ushahidi wote nilioweka katika kitabu na kama haitoshi alikwenda kuzungumza na Ahmed
Rashad Ali rafiki yake Abdulwahid Sykes toka 1939 kutafuta ukweli wa maneno yangu.

Huko nako alishibishwa.

Siku nilipokutananae uso kwa uso Prof. Haroub alikuwa kapwelewa kwani kwake yeye Nyerere alikuwa kila kitu.
Kiongozi muadilifu atoae haki kwa raia wake wote bila ubaguzi, hana udini nk. na nk.

Aliniuliza mengi na mimi nilimjibu kila swali lake alilouliza.

Kwa mara ya kwanza mimi ambaye nilikuwa mwanafunzi wake Mlimani akinisomesha Theories of Development
sasa nikawa namsomesha Prof. wangu historia ya kweli ya Tanganyika.

Prof. Haroub alikuwa kama wengi walivyokuwa - hawakumjua Nyerere wala historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.
Nilikuwa nimemfungulia mlango ambao hakuwahi kupita hata siku moja.

Sishangai hapa JF ninaposoma kejeli na matusi.
Hakika hawa wenzetu wana haki ya kupata mshtuko.

Kuja kujua ukweli baada ya miaka 50 si jambo dogo.
Inahitaji wapewe muda wasafishe bongo zao ili ziwe tayari kupokea elimu mpya.

Baada ya miaka 50 Rais Kikwete anatoa nishani kwa Abdulwahid Sykes na Ally Sykes.

Kwanini hakutoa nishani kwa baba yao Kleist Sykes au kwa Hamza Mwapachu, Stephen Mhando, Zubeir Mtemvu, Sheikh Hassan bin Amir na wengine hili ni swali linalohitaji majibu.

Historia hii bado inahitaji utafiti zaidi na iandikwe.
Mohamed Saidi, kama kawaida ya wazandiki umeamua kumtaja marehemu kuwa shahidi wa uzandiki wako kwa kuwa unajua maiti haina kauri na kwa kuwa Prof. Haroub hawezi kuja hapa jamvini. Wacha hizo, ondoka na siasa zako za uchochezi!
 
Mohamed Saidi, kama kawaida ya wazandiki umeamua kumtaja marehemu kuwa shahidi wa uzandiki wako kwa kuwa unajua maiti haina kauri na kwa kuwa Prof. Haroub hawezi kuja hapa jamvini. Wacha hizo, ondoka na siasa zako za uchochezi!

Usiandike kwa hamaki.
Tujadili kwa utulivu.

Mbona mimi nandika bila kumtusi mtu?

Nikuelezayo ni kweli kabisa na Prof. Haroub alikwenda kwa Nyerere na kumuomba
anijibu yote niliyosema kuhusu yeye.

Dr. Saida Othman aliyekuwa mke wa Prof. Haroub yu hai ukipenda mtafute na muulize.
Anapatikana Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam Idara ya Linguists.

Nitaje kwake ukipenda.

Je ungependa nikueleze majibu ya Nyerere kwa Prof. Haroub?

M

PS: Nina ombi moja kwako ndugu yangu.

Usinitukane tufanye mjadala wa kistaarabu ili ukumbi unufaike.
Sitofurahi na kwa hakika sitaki nikate mawasiliano na wewe
kwa sababu ya lugha chafu.

Nina mengi sana katika historia ya nchi yetu ambayo nipatapo changamoto
bongo langu nalo hucharuka.

Ningependa kutoa elimu hii kwa wote ili tija na faida ipatikane kwetu na kwa kizazi kijacho.
 
Kuja kujua ukweli baada ya miaka 50 si jambo dogo.
Inahitaji wapewe muda wasafishe bongo zao ili ziwe tayari kupokea elimu mpya.

.......................................................................................................................

Historia hii bado inahitaji utafiti zaidi na iandikwe.

Baada ya kujua yote hayo na muendelezo wa utafiti juu ya historia ya TZ ili iandikwe upya; Sheikh unafikiri hiyo kitu itatusaidia nini watanzania ambao tuko kwenye dimbwi la umaskini?.
 
kazi kweli kweli shehe,yan unayoongea yanaingilia huku na kutokea huku.kila siku mnalalmika tu.haya way forwad 'nini!! mmmh hii inaitwa false consns.
haya wavuruge watoto lakin si great thinkers
 
Ndugu yangu Mohamed Said

Hivi ni mimi peke yangu ninayeona correlation ya ujumbe unaotoa na Propaganda za Jews na Nazis..., kutafuta mtu wa kumlaumu kwa matatizo ya sasa kwamba yametokana na tabaka fulani la kunyonya tabaka lingine..?

Haya mambo ya kusema Nyerere aliwabana hapa au pale au alikataa Chuo Kikuu fulani kisijengwe na mengineyo.., Je dhamira yake ni kuonyesha ubaya wa Nyerere, kueleza ukweli au kujenga chuki baina ya tabaka na tabaka na kuweka dhana ya wao na sisi..,

Hivi ni kweli kwamba kipindi kile ulienda kutafuta elimu sehemu fulani ukaambiwa ondoka sababu wewe ni dini fulani ?, na kama ni kweli wewe hii elimu uliyopata uliitoa wapi ?

Na kwa mwenendo huu si ndugu zetu wa-Asia nao itabidi ndio wachukue mapanga kabisa na kutuloga sababu shule zilizokuwa zinamilikiwa na wa-Asia zilitaifishwa ? (au wao sio watanzania) ?

Hivi kwanini tuna-concentrate kutafuta sababu ya matatizo yetu huko nyuma badala ya kujaribu kujikomboa na maisha yanayotukumba sasa..?

Ghafla adui yetu imekuwa Mfumo Kristo.., wakati maadui wa kweli Umasikini na Ujinga bado vinatunyemelea.., hizi mbegu za chuki na propaganda unazopanda sasa mkuu tafadhali usisahau kuandika kitabu kingine cha uharibifu na chuki ambazo zimetokana na propaganda zako.
 
Usiandike kwa hamaki.
Tujadili kwa utulivu.

Mbona mimi nandika bila kumtusi mtu?

Nikuelezayo ni kweli kabisa na Prof. Haroub alikwenda kwa Nyerere na kumuomba
anijibu yote niliyosema kuhusu yeye.

Dr. Saida Othman aliyekuwa mke wa Prof. Haroub yu hai ukipenda mtafute na muulize.
Anapatikana Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam Idara ya Linguists.

Nitaje kwake ukipenda.

Je ungependa nikueleze majibu ya Nyerere kwa Prof. Haroub?

M

PS: Nina ombi moja kwako ndugu yangu.

Usinitukane tufanye mjadala wa kistaarabu ili ukumbi unufaike.
Sitofurahi na kwa hakika sitaki nikate mawasiliano na wewe
kwa sababu ya lugha chafu.

Nina mengi sana katika historia ya nchi yetu ambayo nipatapo changamoto
bongo langu nalo hucharuka.

Ningependa kutoa elimu hii kwa wote ili tija na faida ipatikane kwetu na kwa kizazi kijacho.
Mohamed Saidi, hakika husitahili heshima hata kidogo. Huna nia njema na amani ya nchi yetu. Kwanini unataka nikamuulize mke wa marehem? Prof. Haroub alikuwa msomi aliebobea, alinifundisha UDSM, aliandika sana enzi ya uhai wake na kwa swala nyeti kama unalosema hapa naamini angekuwa ameliandika! Kama hakuliandika basi ni kwakuwa hakuuamini uwongo na uchochezi wako! Nimesikia mahubiri yako kupitia DVD, VCD na CD zako, matokeo ya mahubiri yako yamejaa chuki, uchochezi, hujuma na shari tupu. Vurugu tunazoanza kuzishudia sasa hivi ni matokeo ya uchochezi wako! Wala sijui ni Mungu gani unaye muabudu mtu mbaya kama wewe!! Sijui mjadala wa kiistaarabu ni upi huo wakati wewe mwenyewe hata sio mustaarabu!
 
Mohamed Saidi, hakika husitahili heshima hata kidogo. Huna nia njema na amani ya nchi yetu. Kwanini unataka nikamuulize mke wa marehem? Prof. Haroub alikuwa msomi aliebobea, alinifundisha UDSM, aliandika sana enzi ya uhai wake na kwa swala nyeti kama unalosema hapa naamini angekuwa ameliandika! Kama hakuliandika basi ni kwakuwa hakuuamini uwongo na uchochezi wako! Nimesikia mahubiri yako kupitia DVD, VCD na CD zako, matokeo ya mahubiri yako yamejaa chuki, uchochezi, hujuma na shari tupu. Vurugu tunazoanza kuzishudia sasa hivi ni matokeo ya uchochezi wako! Wala sijui ni Mungu gani unaye muabudu mtu mbaya kama wewe!! Sijui mjadala wa kiistaarabu ni upi huo wakati wewe mwenyewe hata sio mustaarabu!

Nilitaka ukazungumze na Bi Saida kwa kuwa hukuniamini.
Nilitaka usikie kutoka kwenye ulimi wake nini Nyerere alisema.

Prof. Haroub baada ya mazungumzo yetu alikwenda kwa Nyerere
kumwambia kuwa kuna vitabu viwili changu na cha Ali Muhsin "Conflict
and Harmony in Zanzibar," ambavyo vimemwandika vibaya.

Kwa ajili hiyo ni kheri yeye mwenyewe akajibu tuhuma hizo vinginevyo
historia yake atakayoacha nyuma itamchafua vibaya katika jamii.

Sasa nilitaka usikie jibu la Nyerere kutoka kwa mke wa Prof. Haroub.
Nini Nyerere alisema na kuamrisha.

Lakini kwa kukuongezea tafuta kitabu "Farewell to the Chairman."
Kitabu hiki kimechapwa na Dar es Salaam University Press (DUP) kama
kumbukumbu na kumuadhimisha Prof. Haroub Othman.

Katika utangulizi imeandikwa kuwa kabla umauti haujamfika Prof.
Haroub alikuwa katika kutayarisha kitabu kuhusu maisha ya Nyerere.

Chanzo cha kitabu hiki ni mazungumzo niliyofanya na mwalimu wangu
Msikiti wa Ibadh na nikamjibu kila swali alotaka kujua kuhusu Nyerere na
siku zake za awali Dar es Salaam.

Sikiliza ndugu yangu.
Kitabu changu kilikataliwa na kila publisher hapa nchini kwa kumuogopa Nyerere.

Wahariri wote walinambia kazi ni nzuri sana lakini itatuletea matatizo na
serikali. Sisi ni wafanyabiashara hatuwezi kustahamili kisasi cha serikali.

Ndipo nilipopeleka mswada wangu "The Life and Times Of Abdulwahid Sykes
(1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism
in Tanganyika" Uingereza.

Nina mengi sana ambayo naamini kabisa kwako ni mageni katia historia ya Tanganyika.

Namaliza kwa kukufahamisha kuwa wewe Prof. Haroub alikuwa mwalimu wako kama alivyokuwa
mwalimu wangu pia.

Lakini mimi Prof. Haroub ni jamaa yangu hatukuwa na pazia katika mazungumzo yetu.

Kwa ajili hii nikimjua vyema na ninajua ni vipi alimpenda Nyerere na ni vipi kitabu changu
kilimbadili.

Kuwa na subra ondoa hamaki na ghadhabu. Mie napenda mijadala tujiepushe na matusi na kejeli.
Utapata mengi na utakuwa mjanja zaidi.

M

PS: Mungu ninaemuamini ni Allah aliyewafunza Waislam kutodhulumu na kutokubali kudhulumiwa.
 
Wakatoliki wamejenga shule mbili kwa Dar Es Salaam kwenye maeneo ambayo yanakaliwa na waIslamu wengi kwa michango ya waumini wake wakati wa sadaka na misa mbali mbali je shule hizo walizitumia vizuri shule hizo yaani Loyola Na Mt.Anthony ya Mbagala? Kwa nini wanafunzi waligoma?Je waislamu wanahaki ya kuwachukia wakatoliki?Ifike mahali wenzetu fikirieni kabla hamjatenda kafir ni yule asiye amini mungu.Jaribuni kuacha kuita wakristu makafir.Mnachosha kwa kudai madai ambayo hayana kichwa wala miguu.Tuelezeni wenzenu tuwaelewe mnadai nini?
Kuna maeneo ambayo ukienda kufanya "Interview" kama siyo muislamu hupati kazi mbona siye tusio waislamu hatulalamiki? Tufanye kazi tuiletee Tanzania yetu maendeleo ili kizazi chetu kipate nafuu ya maisha.Tuone hizo nchi zilizotawaliwa kwa sheri leo ziko wapi?Libya,Sudan,Syria.....
 
Baada ya kujua yote hayo na muendelezo wa utafiti juu ya historia ya TZ ili iandikwe upya; Sheikh unafikiri hiyo kitu itatusaidia nini watanzania ambao tuko kwenye dimbwi la umaskini?.

Swali umelielekeza sipo.
Tuwaombe wachumi katika JF watusaidie.
 
Back
Top Bottom