Mkuu umedhurumiwa nini na unataka upewe nini ?
Unalalamika dhuluma je wapagani hindus na wenye imani nyingine za mizimu nao vipi ?
Mkuu fanya kazi hii ni land of opportunity issue zako za imani tafuta wenye imani kama wewe na mfanye kile mnachotaka (ili mradi msivunje sheria) kwa wakati wenu na hakuna atakayewasumbua.., haya mambo ya kusubiri spoon feeding au kutaka serikali ikufanyie hiki au kile utakufa kabla ya siku zako kwa stress na kuharibu vizazi vinavyokuja kwa kutangaza chuki zako na kuweka sumu ya utengano..,
Hivi kwa kutumia pesa zako, akili yako na watu wenye imani kama yako mnashindwa kufanya chochote kweli (within legal boundaries) hata kama imani yenu ni kuabudu mizimu ?, ni nani atakayewakataza ?, tafadhali ndugu imani yako isiwe kero kwa wengine..
Mada hailalamiki.
Inaeleza historia ya Waislam na mambo yaliyojiri katika nchi yetu.
Wahindu na Wapagani hawajapata kuwa tatizo Tanzania.
Chukua wakati kujielimisha kiasi unapoandika watu wapende kukusoma.
Ondokana na vitu visivyo na maana katika kujenga hoja zako.
Jifunze kufikiri kwa ubongo wako usiupe moyo nafasi.
Ukifanya hivyo mengi yatakupita.
Mada hii na nyingine nilizoandika mfano wa hizi zimehifadhiwa kwingi
na ni rejea kwa wanafunzi wa African history katika vyuo vingi.
Huwezi kufahamu lakini wajuzi wanasema sehemu ambayo inaweza kulipuka katika Afrika ni
Tanzania.
Wenzetu washaziona dalili.
Askari polisi na JWT weshaingia mitaani kupambana na Waislam.
Magari ya deraya, helikopta zinaruka kuwadhibiti Waislam...
Tumefika vipi hapa?
Kwa nini mada yangu inaogopesha kwa hiyo inatolewa JF isisomwe?
Kwa nini kitabu "Mwembecha Killings..." kinawatisha watawala na hivyo
kukipiga marufuku kisisomwe?
Jiulize anaetishwa na maandishi haya ni nani na kwa nini?
Punguza hamaki, jitulize usome na kisha isaili nafsi yako.
Bado hatujachelewa na wewe hujachelewa kuwa mtu mjuzi hata kama hukubaliani
na nisemayo.
Nafasi bado unayo ya kujifunza na nchi bado ina nafasi ya kuepuka balaa.
Waislam si wavivu.
Wamepigana na Mjerumani.
Wameongoza harakati za kudai uhuru.
Baada ya uhuru wametaka kujenga Chuo Kikuu lakini kikahujumiwa na
Nyerere na Kanisa Katoliki.
Miaka ya 1990 Waislam wametaka kujenga Chuo Kikuu cha Kiislam serikali ikahujumu chuo hicho
kikajengwa Mbale, Uganda.
Ungejadili haya ukumbi ungefaidika.
Nilitaka nikupuuze nisikujibu lakini nimeona nikujibu huenda ukawa msaada katika kuleta utengamano.
Mwisho nakunasihi.
Jiepushe na ufedhuli.
Iko siku watu watakusoma miaka mingi baada ya leo.
Naamini usingependa wasomaji watakaokusoma wakuone ulikuwa kijana mwenye kibri
na aliyejaa ufedhuli na jeuri.
Vinginevyo utajitukanisha wewe na wazazi wako kuwa hawakukupa malezi na kukufunza adabu stahiki.
M
PS:
Nimekuona unatia maneno ya Kiingereza katika uandishi wako.
Mimi nina Merit Pass (First Class) English Oral, Cambridge Examination.
Nimetihaniwa lugha ya Kiingereza nazungumza na kusikilizwa na walimu wa Kiingereza.
Wamenipasisha ngazi ya kwanza.