JituMirabaMinne
JF-Expert Member
- May 4, 2020
- 3,327
- 9,328
Kuna baadhi ya watu huyakataa magari kwa kuangalia Cc za engine(Engine capacity). Lakini huenda kuna watu wameacha magari mazuri kwa sababu ya kigezo hiki. Hebu tuangalie baadhi ya mambo mengine ambayo yanaweza kuchangia ulaji wa mafuta kwenye gari.
1. Aina ya gearbox iliyotumika
Aina ya gearbox iliyotumika inaweza kuamua gari itumie vipi mafuta. Kwa mafano manual gearbox zinafanya gari itumie mafuta sana ukilinganisha na Traditional Automatic gearbox. Hata kwa Automatic Gearbox, DSG ambayo inatumiwa na VW na Audi inaongoza kwa kuwa na matumizi mazuri ya mafuta ikifuatiwa na CVT na mwisho ndio zinakuja Traditional Automatic Gearbox. Kwa kifupi engine yenye Cc2000 halafu ina gearbox ya CVT au DSG inaweza kwenda umbali sawa na engine yenye Cc1500 halafu ina tradional gearbox kwa kiasi cha mafuta kinachofanana. Mfano engine ya HR16DE yenye Cc1600 ambayo imefungwa kwenye Nissan Dualis ikiwa katika hali nzuri inaweza kwenda 18Km kwa lita moja kwa sababu ya gearbox ya CVT. Hiki kitu huwezi kukipata kwa gari yenye engine kama hiyo halafu inatumia gearbox ambayo ni Traditional AT.
2. Aina ya mafuta
Engine za diesel zina ufanisi zaidi na zinatumia mafuta kidogo ukilinganisha na engine za petrol. Kwa mfano sehemu ambayo kwenye gari ya petrol unaweza kutumia Lita 10 gari ya diesel unaweza kutumia lita 8. Na hapo pia itategemea ni aina gani ya gearbox unatumia. Pia bei ya Diesel ni ndogo ukilinganisha na bei ya petrol.
3. Mfumo unaotumika kuingiza mafuta kwenye engine
Mfumo unaotumika kuingiza mafuta kwenye engine unaweza kuchangia sana kwenye utumiaji wa mafuta wa engine yako. Siku za nyuma kwenye magari kulikuwa na Carburator ambayo watengenezaji wa magari waliamua kuachana nayo na sababu mojawapo ya kuiacha ilikuwa ni upotevu wa mafuta. Mfano pia 1AZ FSE na 1 AZ FE ni engine za familia moja lakini zimetofautiana kidogo sana kwenye ulaji wa mafuta na nguvu inazalishwa hii ni kwa sababu 1AZ-FSE inamwaga mafuta moja kwa moja kwenye combustion chamber wakati 1AZ-FE inamwaga mafuta nyuma ya intake valves.
4. Uwepo wa mifumo mbalimbali kwenye engine mfano EGR, VVT n.k
Exhaust Gas Recirculation (EGR) inasaidia kwa kiasi fulani kupunguza ulaji wa mafuta kwenye gari kwa kiasi fulani. Ukichukua engine mbili za aina moja ambazo moja ina EGR na nyingine haina, yenye EGR inakuwa na ufanisi mzuri kwenye matumizi ya mafuta ukilinganisha na ambayo haina EGR. The same kwa upande wa VVT. VVT inasaidia mafuta kuchomwa kwa wakati. Kuna muda muda mafuta yanatakiwa kuchomwa mapema(Ignition Advance) na kuna muda mafuta yanatakiwa kuchomwa kwa kuchelewa (Ignition Retard).
5. Undeshaji wako wa gari
Mnaweza kutoka hapa watu wawili wenye magari yanayofanana kila kitu na mkawekewa kiasi sawa cha mafuta kinachofanana. Kunaweza kuwa na utofauti mkubwa wa umbali ambao magari yenu yatazima kulingana na uendeshaji wa kila mmoja.
6. 4WD au AWD
Gari ambazo ni partial 4WD na AWD zinatumia mafuta mengi hasa muda ambao 4WD inapokuwa ON kwa maana nguvu kubwa zaidi inatumika kuzungusha tairi zote 4. Kama eneo unalokaa halina ulazima wa kuchukua AWD chukua tu gari ambayo ni 2WD itakupunguzia kiasi gharama za mafuta.
7. Gari kuwa Hybrid
Gari za Hybrid zinaweza zinatumia mafuta kidogo kutokana na kwamba kuna muda utaachana na engine na utatumia mfumo mwingine uliopo kama Umeme n.k. Mfano Nissan Fuga 2012 version ambayo ni Hybrid ikiwa na engine ya VQ35HR ambayo ina Cc 3500 tena ni petrol inaweza kwenye 19Km kwa lita moja. Yaani kwa lugha rahisi mafuta ya 100,000/= yanaweza kukutoa Dar mpaka Mbeya na yakabaki.
*************##############************
KAMA UNAHITAJI GATI USED IWE MKONONI AU YARD TUWASILIANE, TUKUTAFUTIE GARI ZURI.
*************############***************
PIA KWA WENYE MATATIZO MBALIMBALI YA MAGARI, TUNAFANYA:
1. FULL SYSTEMS DIAGNOSIS (GHARAMA NI TSH. 40,000/= TU KWA GARI HIZI, TOYOTA, NISSAN, SUZUKI, SUBARU, JEEP NA FORD).
2. ENGINE DIAGNOSIS KWA BRAND YOYOTE YA GARI. GHARAMA NI TSH. 20,000/= TU.
3. KUREKEBISHA MATATIZO KAMA GARI KUKOSA NGUVU, ENGINE KUMISI, KUWASHA TAA YA CHECK ENGINE, MATATIZO YA AUTOMATIC GEARBOX N.K.
***************##############***************
1. Aina ya gearbox iliyotumika
Aina ya gearbox iliyotumika inaweza kuamua gari itumie vipi mafuta. Kwa mafano manual gearbox zinafanya gari itumie mafuta sana ukilinganisha na Traditional Automatic gearbox. Hata kwa Automatic Gearbox, DSG ambayo inatumiwa na VW na Audi inaongoza kwa kuwa na matumizi mazuri ya mafuta ikifuatiwa na CVT na mwisho ndio zinakuja Traditional Automatic Gearbox. Kwa kifupi engine yenye Cc2000 halafu ina gearbox ya CVT au DSG inaweza kwenda umbali sawa na engine yenye Cc1500 halafu ina tradional gearbox kwa kiasi cha mafuta kinachofanana. Mfano engine ya HR16DE yenye Cc1600 ambayo imefungwa kwenye Nissan Dualis ikiwa katika hali nzuri inaweza kwenda 18Km kwa lita moja kwa sababu ya gearbox ya CVT. Hiki kitu huwezi kukipata kwa gari yenye engine kama hiyo halafu inatumia gearbox ambayo ni Traditional AT.
2. Aina ya mafuta
Engine za diesel zina ufanisi zaidi na zinatumia mafuta kidogo ukilinganisha na engine za petrol. Kwa mfano sehemu ambayo kwenye gari ya petrol unaweza kutumia Lita 10 gari ya diesel unaweza kutumia lita 8. Na hapo pia itategemea ni aina gani ya gearbox unatumia. Pia bei ya Diesel ni ndogo ukilinganisha na bei ya petrol.
3. Mfumo unaotumika kuingiza mafuta kwenye engine
Mfumo unaotumika kuingiza mafuta kwenye engine unaweza kuchangia sana kwenye utumiaji wa mafuta wa engine yako. Siku za nyuma kwenye magari kulikuwa na Carburator ambayo watengenezaji wa magari waliamua kuachana nayo na sababu mojawapo ya kuiacha ilikuwa ni upotevu wa mafuta. Mfano pia 1AZ FSE na 1 AZ FE ni engine za familia moja lakini zimetofautiana kidogo sana kwenye ulaji wa mafuta na nguvu inazalishwa hii ni kwa sababu 1AZ-FSE inamwaga mafuta moja kwa moja kwenye combustion chamber wakati 1AZ-FE inamwaga mafuta nyuma ya intake valves.
4. Uwepo wa mifumo mbalimbali kwenye engine mfano EGR, VVT n.k
Exhaust Gas Recirculation (EGR) inasaidia kwa kiasi fulani kupunguza ulaji wa mafuta kwenye gari kwa kiasi fulani. Ukichukua engine mbili za aina moja ambazo moja ina EGR na nyingine haina, yenye EGR inakuwa na ufanisi mzuri kwenye matumizi ya mafuta ukilinganisha na ambayo haina EGR. The same kwa upande wa VVT. VVT inasaidia mafuta kuchomwa kwa wakati. Kuna muda muda mafuta yanatakiwa kuchomwa mapema(Ignition Advance) na kuna muda mafuta yanatakiwa kuchomwa kwa kuchelewa (Ignition Retard).
5. Undeshaji wako wa gari
Mnaweza kutoka hapa watu wawili wenye magari yanayofanana kila kitu na mkawekewa kiasi sawa cha mafuta kinachofanana. Kunaweza kuwa na utofauti mkubwa wa umbali ambao magari yenu yatazima kulingana na uendeshaji wa kila mmoja.
6. 4WD au AWD
Gari ambazo ni partial 4WD na AWD zinatumia mafuta mengi hasa muda ambao 4WD inapokuwa ON kwa maana nguvu kubwa zaidi inatumika kuzungusha tairi zote 4. Kama eneo unalokaa halina ulazima wa kuchukua AWD chukua tu gari ambayo ni 2WD itakupunguzia kiasi gharama za mafuta.
7. Gari kuwa Hybrid
Gari za Hybrid zinaweza zinatumia mafuta kidogo kutokana na kwamba kuna muda utaachana na engine na utatumia mfumo mwingine uliopo kama Umeme n.k. Mfano Nissan Fuga 2012 version ambayo ni Hybrid ikiwa na engine ya VQ35HR ambayo ina Cc 3500 tena ni petrol inaweza kwenye 19Km kwa lita moja. Yaani kwa lugha rahisi mafuta ya 100,000/= yanaweza kukutoa Dar mpaka Mbeya na yakabaki.
*************##############************
KAMA UNAHITAJI GATI USED IWE MKONONI AU YARD TUWASILIANE, TUKUTAFUTIE GARI ZURI.
*************############***************
PIA KWA WENYE MATATIZO MBALIMBALI YA MAGARI, TUNAFANYA:
1. FULL SYSTEMS DIAGNOSIS (GHARAMA NI TSH. 40,000/= TU KWA GARI HIZI, TOYOTA, NISSAN, SUZUKI, SUBARU, JEEP NA FORD).
2. ENGINE DIAGNOSIS KWA BRAND YOYOTE YA GARI. GHARAMA NI TSH. 20,000/= TU.
3. KUREKEBISHA MATATIZO KAMA GARI KUKOSA NGUVU, ENGINE KUMISI, KUWASHA TAA YA CHECK ENGINE, MATATIZO YA AUTOMATIC GEARBOX N.K.
***************##############***************