Mbavu za Mbwa
JF-Expert Member
- Jan 2, 2011
- 303
- 154
Imekuwa ni kawaida sana kwa mzazi(mwanamke) aliyejifungua kulifunga tumbo lake kwa mkanda au kitambaa ili kulifanya lirudi katika hali yake ya kawaida. Hii inafanyikaa sana kwa akina mama ambao hujifungua kwa njia ya kawaida. Swali langu ni hili: mke wangu alijifungua kwa njia ya kupasuliwa miezi 7 iliyopita. kutokana na kupasuliwa huko, hakuwahi kulifunga tumbo hilo na sasa limekuwa kubwa na linampotezea shepu yake halisi. je, anaweza kulifunga kwa sasa? Au kuna madhara pindi atakapofanya hivyo ukizingatia kuwa ana mshono. Kama si kufunga anaweza kutumia njia gani mbadala iliyo salama ili kupunguza tumbo? Naombeni msaada wenu