Jarida la burudani la Sani limepoteleaga wapi

Jarida la burudani la Sani limepoteleaga wapi

Kipindi cha nyuma naona agenda kulikua hamna
Wakikaa ofisini wanaamua tu jaman tuchore tu katuni
Kabisa ilo la mwaka 85
images-40.jpg
 
SANI-Said(MM Bawji) na Nicco(Yembajo) walikuwa wabunifu sana.

Nicknames tatu za watu maarufu wa kipindi hiki zimetoka kwenye gazeti la Sani.

Mzee Meko a k a Mwendazake (R I P), Lodi Lofa(R I P) na Betina.
 
japo umechanganya wahusika wa majarida yote-sani,tabasamu,bongo.
kwa wakati huo hizi ndio zilikuwa instagram na facebook zetu.

mlezi wangu alikuwa anayaleta yote matatu kila mwezi akitoka town kufata mshahara,yaani unapokea mizigo huku mawazo yako yapo kwenye majarida.kuna jingine lilitwa ambha,lilikuwa na mashairi kibao.

uzuri wa haya madude yalisheheni visa visivyochosha kusoma,unaweza rudia hata mara tatu unaenjoy tu.
 
Walikuwa wanayauza sana kipindi hicho, walikwama wapi?. Wakati soko lilikuwepo? Au baada ya vifo vya wachoraji Kama John kaduma(R.I.P)
 
japo umechanganya wahusika wa majarida yote-sani,tabasamu,bongo.
kwa wakati huo hizi ndio zilikuwa instagram na facebook zetu.

mlezi wangu alikuwa anayaleta yote matatu kila mwezi akitoka town kufata mshahara,yaani unapokea mizigo huku mawazo yako yapo kwenye majarida.kuna jingine lilitwa ambha,lilikuwa na mashairi kibao.

uzuri wa haya madude yalisheheni visa visivyochosha kusoma,unaweza rudia hata mara tatu unaenjoy tu.
Dah kweli umenikumbusha jarida la ambha
 
Kila jambo hapa duniani, mwanzilishi wake 'akivuta', jambo hilo huishia kusambaratika na kufa kifo cha kawaida.

Hata akatokea mrithi, huwa hawezi kulipeleka kama mwanzilishi alivyoliendesha.

Kadhia ilianza pale mchoraji wao nguli Kaduma kufariki kifo cha mapema pamoja na waandishi wengine.

Waliofuatia hawakufikia viwango vya waanzilishi.

Na mabadiliko ya teknolojia ya mawasiliano, hasa simu janja kuzagaa mikononi mwa wadau, ndiyo basi tena.
 
Back
Top Bottom