nice 2
JF-Expert Member
- Aug 10, 2011
- 747
- 520
Mh Zitto Kabwe amewadanganya vijana wa kitanzania,baada ya kuwaahidi kuwa atapeleka bungeni hoja binafsi kuhusu tatizo la ajira kwa vijana ambalo limekuwa ni disaster kwa sasa..badala yake amesikika akipeleka hoja binafsi ya mambo ya kilimo cha mkonge na kupuuzia ile hoja ya ajira kwa vijana aliyowahaidi kupitia chombo kimoja cha redio hapa Tanzania..
Namuomba Zitto na wanasiasa wengine vijana msiwatumie vijana wenzenu kwa maslahi yenu binafsi,kama mmeshindwa kuwapigania basi waacheni waendelee ku-hustle kimpango wao msijifanye mnaumizwa sana na matatizo yao ikifika suala la kuwawakilisha inakuwa usanii mtupu..vijana ni waelevu wanausoma tu mchezo.
Amaa kweli wahenga walisema jambo usilolijua ni kama usiku wa giza, lakini pia kuuliza si ujinga.
Mkuu matumbo uliposikia Mh. Zitto akiwaahidi vijana kushughulikia suala la ajira ulifikiri zinapatikanaje, kwa miujiza kutoka mbinguni?
Kukusaidia kwa ufupi tu ni kwamba, uchumi wa nchi ukidorora, kila kitu kinadorora including ajira. Hoja anayoiwasilisha Zitto kuhusu kufufua zao la Mkonge kama itafanikiwa kupita basi kwa hakika itachangia kukua kwa uchumi, na hivyo kutoa nafasi nyingi za ajira za moja kwa moja kwenye mkonge, pamoja na fursa nyingine za ajira zitakazopatikana indirectly kutokana na kukua kwa uchumi utaochochewa na uzalishaji huo wa mkonge.
Next time usiwe mvivu wa kufikiri na kutanguliza lawama mbele, lakini pia ukiona umeshindwa basi ni vyema ukauliza.