Janja ya nyani: Tuoleane, Ukioa kwangu sitakutoza mahari! Huku nikijua kabisa sina mabinti wa kutosha kuozesha maana wengi walishaolewa

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Feb 17, 2015
13,663
18,037
Haya makubaliano ya kuoleana baina ya jamii mbili bila kutozana mahari tuyamulike! Jamii moja mabinti zake wengi walishaolewa tayari! Ndiyo inakuwa ya kwanza kupendekeza mambo ya kuoleana bila kulipishana mahari! Jamii nyingine bado ina mabinti wengi ambao hawajaolewa.

Japo kila jamii inapewa kibali kwenda kuoa bure jamii ya jirani lakini upande mmoja hauna mabinti wa kutosha! Utaenda kule na kutafuta binti wa kuoa na hutampata! Wao wakija kwako wataoa maana una mabinti wengi! Vijana wako utakuwa umewaongezea ushindani bila sababu ya msingi.

Hali kadhalika kwa Kenya kusema watanzania tuende huko kufanya kazi na biashara bila vibali. Huko kumebana!! Kwetu bado ni bwerere!! Hivi inahitaji mtu kuwa na PhD kuliona hilo. Ukinaswa kwenye mtego ulio wazi hivyo watu hawataamini kuwa umenaswa kwa bahati mbaya, bali ulikuwa na jambo lako.

Sisi Tanzania bado tunaongea habari ya kutoa ardhi kwa wawekezaji huko kwa wenzetu hakuna hiyo ardhi ya kumpa mwekezaji haipo!! Wao unyang'au uko kwenye damu na wanauonea fahari wakati sisi tumejaa "undugu"!! huwezi kutoboa!! Wanaoweza ni wafanyabiashara wakubwa tu kama kina Bakhresa.
 
Ningekuelewa mkuu kama mfano wako ungesema mabinti wapo kote kote na wana uzurii sawa tu ila tatizo unajua vijana wako wa kiume madomo zege.

Watanzania shida yetu competence na kujiamini. Vijana wadogo kabisa badala ya ku focus kwenye taaluma zao na kujenga experience tumekalia mara Team Membe, mara Team Lowasa, Mara team Legacy, ukikuta kijana anakuchambulia historia ya liverpool sports club utapiga saluti ila mwambie atetee expertise yake sasa, hata kama ni Engineer au banker anafanya kazi kwa mazoea tu na kuunga unga.
 
Katika hili suala kusema kweli Tanzania tupo katika upande wa kupoteza. It's not a win-win situation.
 
Tumuache Mama atekeleze ilani ya chama chake kuelekea 2025 kutokana na mipango aliyojiwekea kama Rais wa taifa letu. Kipindi cha mwendazake mambo ya diplomasia yalikuwa yamezorota mno, kwa hiyo tuache kulalama pale jambo muhimu linapoanza kupata ufumbuzi upya, tuache kuwa na nongwa. Twende na Mama kwa njia hii mpaka 2030.
 
0
Ningekuelewa mkuu kama mfano wako ungesema mabinti wapo kote kote na wana uzurii sawa tu ila tatizo unajua vijana wako wa kiume madomo zege.

Watanzania shida yetu competence na kujiamini. Vijana wadogo kabisa badala ya ku focus kwenye taaluma zao na kujenga experience tumekalia mara Team Membe, mara Team Lowasa, Mara team Legacy, ukikuta kijana anakuchambulia historia ya liverpool sports club utapiga saluti ila mwambie atetee expertise yake sasa, hata kama ni Engineer au banker anafanya kazi kwa mazoea tu na kuunga unga.
Kuna ukweli kiasi fulani katika hilo unalosema! Hali ni kwamba kwa mazingira ya sasa tupende tusipende hatuwezi tukajidanganya kuwa wakenya wakimiminika kwa wingi huko kwenye vijiji vyetu tutaweza kushindana nao!! Tutashuhudia wakiuziwa ardhi kwa bei ya kutupa, wakituolea kwa wingi na vitu kama hivyo!! Hatujawa tayari bado!!
 
Uzuri ni kwamba viongozi wetu wamesikia ofa tuliyopewa, lakini hawajasema na sisi njoni kwetu! Watanzania tuna utamaduni na desturi ya kukataa misaada/ofa yenye masharti. Kama Kenya watakuwa wanasubiri na sisi tuwape ofa kama hiyo basi WATASUBIRI SANA!!
 
Haya makubaliano ya kuoleana baina ya jamii mbili bila kutozana mahari tuyamulike! Jamii moja mabinti zake wengi walishaolewa tayari! Ndiyo inakuwa ya kwanza kupendekeza mambo ya kuoleana bila kulipishana mahari! Jamii nyingine bado ina mabinti wengi ambao hawajaolewa! Japo kila jamii inapewa kibali kwenda kuoa bure jamii ya jirani lakini upande mmoja hauna mabinti wa kutosha! Utaenda kule na kutafuta binti wa kuoa na hutampata! Wao wakija kwako wataoa maana una mabinti wengi! Vijana wako utakuwa umewaongezea ushindani bila sababu ya msingi!
Hali kadhalika kwa Kenya kusema watanzania tuende huko kufanya kazi na biashara bila vibali!! Huko kumebana!! Kwetu bado ni bwerere!! Hivi inahitaji mtu kuwa na PhD kuliona hilo!! Ukinaswa kwenye mtego ulio wazi hivyo watu hawataamini kuwa umenaswa kwa bahati mbaya, bali ulikuwa na jambo lako!
Sisi Tanzania bado tunaongea habari ya kutoa ardhi kwa wawekezaji huko kwa wenzetu hakuna hiyo ardhi ya kumpa mwekezaji haipo!! Wao unyang'au uko kwenye damu na wanauonea fahari wakati sisi tumejaa "undugu"!! huwezi kutoboa!! Wanaoweza ni wafanyabiashara wakubwa tu kama kina Bakresa!
Daud Albert Bashite unahaha Sana , meko alikutema, mama hakuhitaji, pole Sana bro
 
Haya makubaliano ya kuoleana baina ya jamii mbili bila kutozana mahari tuyamulike! Jamii moja mabinti zake wengi walishaolewa tayari! Ndiyo inakuwa ya kwanza kupendekeza mambo ya kuoleana bila kulipishana mahari! Jamii nyingine bado ina mabinti wengi ambao hawajaolewa! Japo kila jamii inapewa kibali kwenda kuoa bure jamii ya jirani lakini upande mmoja hauna mabinti wa kutosha! Utaenda kule na kutafuta binti wa kuoa na hutampata! Wao wakija kwako wataoa maana una mabinti wengi! Vijana wako utakuwa umewaongezea ushindani bila sababu ya msingi!
Hali kadhalika kwa Kenya kusema watanzania tuende huko kufanya kazi na biashara bila vibali!! Huko kumebana!! Kwetu bado ni bwerere!! Hivi inahitaji mtu kuwa na PhD kuliona hilo!! Ukinaswa kwenye mtego ulio wazi hivyo watu hawataamini kuwa umenaswa kwa bahati mbaya, bali ulikuwa na jambo lako!
Sisi Tanzania bado tunaongea habari ya kutoa ardhi kwa wawekezaji huko kwa wenzetu hakuna hiyo ardhi ya kumpa mwekezaji haipo!! Wao unyang'au uko kwenye damu na wanauonea fahari wakati sisi tumejaa "undugu"!! huwezi kutoboa!! Wanaoweza ni wafanyabiashara wakubwa tu kama kina Bakresa!
Hili la Wakenya kukaribishwa kupewa ardhi, Rais SSH alirejee upya, lina ukakasi. Kuna kundi kubwa la vijana wenye elimu ya fani mbalimbali, Serikali yake iweke mazingira rafiki na wezeshi wasio na ajira waendeleze ardhi kwa kilimo kama ilivyo sasa kwa machinga na wachimba madini wadogo wadogo
 
Back
Top Bottom