Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,900
- 944
MH. JANETH MAHAWANGA AGAWA TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI WA KIKE 700.
Mbunge wa viti Maalum Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Janeth Elias Mahawanga ambaye pia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Tisha Mama Foundataion Kwa kushirikiana na Taasisi ya T-MARC Tanzania amekabidhi taulo za Kike kwa wanafunzi 700 katika shule ya Sekondari Makumbusho kuelekea kilelele cha maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani tarehe 08/03/2023.
Mhe. Mahawanga ameipongeza sana T-MARC Tanzania kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kuhakikisha Watoto wa Kike wanaendelea kupata hedhi salama ili kulinda afya zao maana hakuna maisha bila hedhi salama.
Vile vile, Mhe. Mahawanga ameipongeza sana Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada kubwa inayofanyika kuhakikisha sekta ya Elimu inaboreshwa sambamba na kutengeneza mazingira rafiki kwa Wanafunzi kupata elimu bora ikiwemo ujenzi wa madarasa, Elimu bure kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha sita na kuhakikisha inaweka mazingira mazuri ya kufundishia kwa Walimu.
Katika zoezi hilo Mhe. Mahawanga alipata wasaa mzuri wa kuzungumza na Mkuu wa shule na baadhi ya Walimu ambao ndio walezi ili kubaini changamoto za kiutendaji ambapo ameahidi kuziwasilisha mahali husika ili ziweze kushughulikiwa. Kwa upande wao Walimu hao wametoa shukurani zao kwa msaada wa taulo hizo kwani zitapunguza ongezeko la utoro shuleni.
Lakini pia Mhe. Mahawanga alikuwa ni wasaa mzuri sana kuzungumza na Wanafunzi wote wakike na wa kiume ambapo amewataka Wanafunzi hao kutochanganya mapenzi na masomo pia amewasisitiza zaidi kujiepusha na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia baina yao na kuwataka kila mmoja kuwa mlinzi wa mwenzie ili wote kwa pamoja wawe salama, wawe watoto wenye maadili na kulinda utu wao.
Sambamba na hayo Mhe. Mahawanga amewakumbusha Wanafunzi hao kusimamia malengo na ndoto zao na kuwasisitiza kuwa hawawezi kufikia malengo yao bila ushirikiano, juhudi binafsi na nidhamu. Vile vile amewasihi wazingatie kilichowapeleka shule na si mambo yasiyohusiana na masomo kwani wanajukumu kubwa la kupambania ndoto zao maana kila kitu kinawezekana.
Mwisho, Mhe. Mahawanga amewaomba wadau mbalimbali kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali kwani uhitaji kwenye jamii bado ni mkubwa mno hususani kwa vijana walio mashuleni ambao ndio Taifa la kesho.
#TishaMama.
#MamaVikoba
Mbunge wa viti Maalum Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Janeth Elias Mahawanga ambaye pia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Tisha Mama Foundataion Kwa kushirikiana na Taasisi ya T-MARC Tanzania amekabidhi taulo za Kike kwa wanafunzi 700 katika shule ya Sekondari Makumbusho kuelekea kilelele cha maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani tarehe 08/03/2023.
Mhe. Mahawanga ameipongeza sana T-MARC Tanzania kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kuhakikisha Watoto wa Kike wanaendelea kupata hedhi salama ili kulinda afya zao maana hakuna maisha bila hedhi salama.
Vile vile, Mhe. Mahawanga ameipongeza sana Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada kubwa inayofanyika kuhakikisha sekta ya Elimu inaboreshwa sambamba na kutengeneza mazingira rafiki kwa Wanafunzi kupata elimu bora ikiwemo ujenzi wa madarasa, Elimu bure kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha sita na kuhakikisha inaweka mazingira mazuri ya kufundishia kwa Walimu.
Katika zoezi hilo Mhe. Mahawanga alipata wasaa mzuri wa kuzungumza na Mkuu wa shule na baadhi ya Walimu ambao ndio walezi ili kubaini changamoto za kiutendaji ambapo ameahidi kuziwasilisha mahali husika ili ziweze kushughulikiwa. Kwa upande wao Walimu hao wametoa shukurani zao kwa msaada wa taulo hizo kwani zitapunguza ongezeko la utoro shuleni.
Lakini pia Mhe. Mahawanga alikuwa ni wasaa mzuri sana kuzungumza na Wanafunzi wote wakike na wa kiume ambapo amewataka Wanafunzi hao kutochanganya mapenzi na masomo pia amewasisitiza zaidi kujiepusha na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia baina yao na kuwataka kila mmoja kuwa mlinzi wa mwenzie ili wote kwa pamoja wawe salama, wawe watoto wenye maadili na kulinda utu wao.
Sambamba na hayo Mhe. Mahawanga amewakumbusha Wanafunzi hao kusimamia malengo na ndoto zao na kuwasisitiza kuwa hawawezi kufikia malengo yao bila ushirikiano, juhudi binafsi na nidhamu. Vile vile amewasihi wazingatie kilichowapeleka shule na si mambo yasiyohusiana na masomo kwani wanajukumu kubwa la kupambania ndoto zao maana kila kitu kinawezekana.
Mwisho, Mhe. Mahawanga amewaomba wadau mbalimbali kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali kwani uhitaji kwenye jamii bado ni mkubwa mno hususani kwa vijana walio mashuleni ambao ndio Taifa la kesho.
#TishaMama.
#MamaVikoba