Jana nimeng'atwa na nyoka mguuni!

Jana nimeng'atwa na nyoka mguuni!

Pole sana kwani Mungu bado anakupenda na inavyoonekana nyoka aliyekung'ata hana sumu kali. Kama kuna kiumbe namuogopa duniani ni huyo nyoka. Mkuu ukiwa unaenda kufanyia "service" gari jitahidi uwe unabeba oil chafu ichangaye na dizeli kidogo halafu ukija unamwaga kidogo kidogo pembeni ya fensi/nyumba harufu yake inasaidia kwa kiasi fulani kuwafukuza hao wadudu. Pia hakikisha umefanyia usafi/kufyeka eneo lako lote na hata la jirani yako iwapo halijafanyiwa usafi wewe ingia tu gharama ulisafishe. Pia chukua tahadhari sana kipindi cha mvua/baridi kwani hao wadudu hawachelewi kuingi ndani kutafuta joto.
Akhsante sana mkuu
Hilo nitalifanyia kazi kwa usalama zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watanzania
Tujifunze First Aid

Tuwe na First Aid kits majumbani kwetu. Tuwe na antivenom majumbani kwetu na tuwafundishe wote tunaoishi nao jinsi ya kutumia hizo aid kits.

Tukifanya hivi tutapunguza vifo vingi visivyo na msingi

Sent using Jamii Forums mobile app

Shida ya hizi kitu, unaweza kukaa nazo kila mara unazicheki. Ila ikipita miaka kadhaa hujakutwa na tatizo hata kuangalia ufanisi wake unaacha. Siku la kutokea linatokea madude hayafanyi kazi,

Mfano rahisi ni kwenye Fire Extinguisher za magari, tunakaa nazo mpaka zina expire, au mwingine unakuta hata kutumia hajui.
 
Siku nyingine ikitokea fanya haya
1 ufunge mguu sumu isipande (hii nadhan ulifanya)
2 chanja mguu au sehem iliyoumwa ili ile damu iliyozuiwa na kamba iwe inatoka nje, inapotoka inatoka na sumu
3 kunywa mkojo

Halafu wahi hospital
Kuna hadithi ya kitambo sana Umenikumbusha, Tanga maeneo ya mabawa jamaa kang'atwa na nyoka... Akawa anaugulia asijue cha kufanya... Kuhu watu wengine wakijaribu kumsaidia lakini inaonekana nyoka alikuwa na sumu kali mno... Ghafla akapita bibi anauliza kinachoendelea,, kusikia kwamba jamaa kang'atwa na nyoka... Akamwambia asubiri dakika kadhaa akafuate dawa... Akamchukua binti aliyekaribu akaingia nae kwenye boma baada ya dakika chache wakarudi bibi kashikilia chupa ina maji... Jamaa anaambiwa hiyo ni dawa... Masharti yake unywe bila kuisikilizia.... Jamaa akanywa kisha akapona... Mwisho wa siku anaambiwa hiyo dawa ni mkojo.... Sikumbuki lilikuwa ni gazeti gani kati ya champion, kiu ama sani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siku nyingine ikitokea fanya haya
1 ufunge mguu sumu isipande (hii nadhan ulifanya)
2 chanja mguu au sehem iliyoumwa ili ile damu iliyozuiwa na kamba iwe inatoka nje, inapotoka inatoka na sumu
3 kunywa mkojo

Halafu wahi hospital
Hakuna chochote hapo kinachosaidia kw mtu aliyeng'atwa na nyoka, kikubwa uking'atwa na nyoka kuwa mtulivu, uspanic maana utasababisha mapigo ya moyo kwenda haraka na hivyo sumu kuenea kwa haraka mwilini, alafu usitumie kiungo kilichong'atwa na nyoka, then straight hospital

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bro unautalamu na hawa wadudu??... mana leo katika mishe za hapa na pale nimekutana na mmoja aisee yuko fasta sana ni mrefu usawa wa mkono wa mtu mzima halafu anakichwa kilichochongoka mithili ya pembe tatu hivi na mweusi ila siyo ya kukolea, baada ya kuniona alikimbia sana akafika kwenye kidimbwi cha maji akachumpa kwa speed sana na kudumbukia humo nilishanga sana maana sijawahi kuona nyoka wa aina ile na mbio za namna ile.
Hivi huyu ni nyoka wa aina gani boss au ndio swila mwenyewe??.
Huyo ni jini pepo kwanini hukukemea?
 
Pole sana kwa matatizo yaliyokukuta.Binafsi huwa siogopi nyoka hata kidogo nimewahi kung'atwa na nyoka Mara kadhaa lakini huyo nilipoka uhai wake.

Shukuru hakuwa black mamba/koboko kwa muda huu ungekuwa kaburini


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naam hakukuwa na anaejua kuendesha muda huo, mzee akiona naserereka kwenye kona na mia na ishirini alikuwa ananiuliza mara kwa mara najisikiaje....nadhani ni hofu ya kujua naanza kupoteza mdogo mdogo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Pole sana mkuu, Mungu yu mwema kwa watu wake, Kuna ndugu yangu alikua anatembea usiku hivi, duh kumbe kamkanyaga nyoka ,akang'atwa akapiga kelele nimeng'atwa na nyoka, watu wanakimbia kumsaidia tayari akawa kashapoteza fahamu yani,tunashukuru alipona lkn.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna hadithi ya kitambo sana Umenikumbusha, Tanga maeneo ya mabawa jamaa kang'atwa na nyoka... Akawa anaugulia asijue cha kufanya... Kuhu watu wengine wakijaribu kumsaidia lakini inaonekana nyoka alikuwa na sumu kali mno... Ghafla akapita bibi anauliza kinachoendelea,, kusikia kwamba jamaa kang'atwa na nyoka... Akamwambia asubiri dakika kadhaa akafuate dawa... Akamchukua binti aliyekaribu akaingia nae kwenye boma baada ya dakika chache wakarudi bibi kashikilia chupa ina maji... Jamaa anaambiwa hiyo ni dawa... Masharti yake unywe bila kuisikilizia.... Jamaa akanywa kisha akapona... Mwisho wa siku anaambiwa hiyo dawa ni mkojo.... Sikumbuki lilikuwa ni gazeti gani kati ya champion, kiu ama sani

Sent using Jamii Forums mobile app
Dah! Si mchezo!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom