Jana nimeng'atwa na nyoka mguuni!

Jana nimeng'atwa na nyoka mguuni!

Hizi Antvenom zinauzwa wapi?Kwa uzoefu wangu nimeshaona mara kadhaa watu wanazikosa kwenye hospitali za serikali tena za ngazi ya wilaya,
Samahani nielekeze zinapatikana wapi ili nikanunue hata kama sijui kuchoma ikitokea dharula naweza chomwa na nesi yeyote mtaani inapobidi.
Mfano nimeshuhudia mara kadhaa watu wengi wanaong'atwa na mbwa vichaa kwa ukanda wa pwani na dar hospitali yenye uhakika wa hizo sindano ni dar mnazi mmoja ie hata muhimbili huwa wakati fulani wanazikosa.
Lakini hivi antvenom uking'atwa na black mamba inafanana na kama umeng'atwa na cobra?
Antivenom ni ghali kiasi kwa huko bongo bei yake yafika 200k pia kuwa na Antivenom hakukupi uhalali wa kupona baada ya Shambulio sababu kuna yapaswa ujue umeshambuliwa na specie gani ya nyoka pia unapochoma yapaswa uwe na Adrenaline Pembeni kuzuia Anaphylatic reaction nikimaanisha hutoweza kujichoma pia kama watu wajichomavyo Insulin! Mwisho nikutaarifu tu sio kila nyoka anayo Anti-venom ila kwa sababu ya ukanda uliopo yaweza kuwa rahisi kujua walau ni jamii gani hupatikana ukanda fulani na ukanda fulani kama ambavyo ipo kwa wanyama wa kawaida tu
 
Antivenom ni ghali kiasi kwa huko bongo bei yake yafika 200k pia kuwa na Antivenom hakukupi uhalali wa kupona baada ya Shambulio sababu kuna yapaswa ujue umeshambuliwa na specie gani ya nyoka pia unapochoma yapaswa uwe na Adrenaline Pembeni kuzuia Anaphylatic reaction nikimaanisha hutoweza kujichoma pia kama watu wajichomavyo insulin! Mwisho nikutaarifu tu sio kila nyoko anayo Anti-venom ila kwa sababu ya ukanda uliopo yaweza kuwa rahisi kujua walau ni jamii gani hupatikana ukanda fulani na ukanda fulani hawapo kama wanyama wa kawaida tu
Thnx mukenya,ujuee hapa bongo jua vile ni kali kuna yapaswa kujua pesa mfukoni nakauka kabisa!!!!!
 
Kipindi Niko shule msingi nilishawa kung'atwa na green mamba! Nilipooza mwili mzima macho tu ndiyo yalikua yanaona ila kwenye dark mode!

Thanks to my teacher mallya alihakikisha napata tiba haraka
 
Mama alipo sema nipelekwe hospital
Nikasikia Watu wanasema hospital Hakuna dawaa ya nyoka....
Hapo
Ndipo hofu na woga ulipo zidi sikutamani kuiaga dunia huku najiona live......
Inaonekana ilikuwa miaka mingi nyuma, sasa hivi dawa za kuzuia sumu ya Nyoka kusambaa mwilini zipo hospital.
 
kuna elimu niliwahi kupataa kuhusu nyokoka ni kwambaa!!

1: kuna nyoka aina mbili kuna wale wenye kichwa cha pembe tatu- hawa nyoka wana sumu sana , ikitokea umeumwaa na huyu nyoka basi wahi hospitalini sana na uwaeleze ni aina gan ya nyoka.
2: pia kuna wale wenye kichwa mduara hawa hawana sumu kivile, ilq ikitokea umeng'atwa na hawa pia nenda hospitalini na pia uwaambie aina ya nyokaa.
 
Vipi maumivu yake?na kwanin ulimuacha aende ulitakiwa umuue
 
Watanzania
Tujifunze First Aid

Tuwe na First Aid kits majumbani kwetu. Tuwe na antivenom majumbani kwetu na tuwafundishe wote tunaoishi nao jinsi ya kutumia hizo aid kits.

Tukifanya hivi tutapunguza vifo vingi visivyo na msingi

Sent using Jamii Forums mobile app

Weka picha
 
Naam, huku awali walikuwa wakiniogopa ila baadae waliponifuata na kutaka michango ya Madrasa nikawa natoa, michango ya ujenzi wa kanisa ninatoa, michango ya kununua mpira timu ya mtaani ninatoa....na hapo wakasema kumbe huna tatizo tulikuwa tunakufikiria tofauti sana.

Sent using Jamii Forums mobile app

Usingetoa pesa ungekuwa na tatizo? Yaan mpaka pesa ndio uonekane mzuri
 
Ondoa Nge hapo. Nge akikugonga maumivu yake hata usipoweka dawa yadumu 24 "hours" halafu yanaaondoka yenyewe ghafla. Ila huyo mwingine naogopa hata kumtaja maana wanasema ukimtaja taja sana huchelewi kumukuta mguuni kwako.

Hahahaha
 
Huyo nyoka hakuwa na sumu.
Hayo madawa uliyopewa ni kuongeza sumu tu mwilini.Kilichokufanya upate nafuu na pressure iwe sawa hadi kujiona mzima ni imani tu kuwa umepewa dawa.

Kwa sasa sidhani kama kuna hospitali yoyote ya serikali ina dawa za sumu ya nyoka.

Pili ni madaktari wachache na pengine hawazidi 20 ambao wana utaalamu na jinsi ya kuchoma sindano za dawa za kuondoa sumu ya nyoka.Zaidi kuna wanasiasa tu watazungumza nadharia nyingi tu za kutosha ila kiuhalisia hawawezi kutibu.

Tatu kuna watu wana miaka hadi kumi kazini hawajawahi kuiona dawa hiyo ya sumu ya nyoka.

Mwisho,kichupa kimoja cha dawa kinauzwa hadi laki sita,na unaweza chomwa zaidi ya kimoja.
Najua kama ungetoa pesa hiyo lazima hapa ingekuwa ndiyo mada kwani bima ya afya haigharimii issue kama hizo za kung'atwa na nyoka.

Mwisho pole sana kwa tukio hilo,mkumbuke Mungu aliyekupa Neema ya kuwa mzima

Sent using Jamii Forums mobile app

Tukiumwa na nyoka tujitibu na nini?
 
Vipi maumivu yake?na kwanin ulimuacha aende ulitakiwa umuue
Hamaki ilikuwa kubwa sana na huku nikifikiria hatma yangu hasa nikizingatia ni usiku wa maanane.
Maumivu yake hapo kwa hapo si makali ila kadri sumu inavyopanda ndiyo kimbembe.
 
Usingetoa pesa ungekuwa na tatizo? Yaan mpaka pesa ndio uonekane mzuri
Yapo mambo automatically yanahitaji pesa na wenzako wote wanatoa, sasa wewe usipotoa na ni mgeni hii inamaanisha umekataa taratibu ulizozikuta na ni sawa na kukataa ushirikiano hivyo huleta hali ya kuonekana mbaya. Unanielewa?
 
Back
Top Bottom