My people hope mpo gud au sio,binafsi nipo gud sana ni usiku mwingine tena
Jamani leo nina ujinga flani hivi nataka kuuongea hapa,ila ubakie hapa hapa ndani ya Mastory ya Bey,maana hapa ndio sehemu ambayo huwa najiachia,yani kama bungeni vile,unajua wabunge wanalindwa na sheria kwa jambo lolote ambao watalijadili pale mjengoni basi hawashtakiwi,nami nisikuhukumiwe nikiwa katika zone yangu hapa.
Iko hivi ebu tuchukilie mfano kwamba watu wakitekwa wawe wanapelekwa vocation sehemu fulani ingawa tunaweza tusiijue wapi,lakini tunajua wapo salama na watarudi tu wakiwa bukheri wa afya
Je kama hivyo ndivyo,unafikiri tutakuwa na mashaka sana tukisikia wapendwa wetu wametekwa? Hatutakuwa na mashaka sana kwakuwa tunajua wapo salama na watarudi
Sasa tuje kwenye ujinga ambao nataka kuzungumza hapa,wote tunajua mtu akikuchukulia bwana wako au mwanamke wako,hapana shaka tunajua kwamba hatamuua wala kumdhuru ila tunajua atamkula na kisha huyo mpendwa wetu atarudi salama salimini,kama hivyo ndivyo sasa kwanini huwa tunapaniki sana na kutaka kujiua au kuua kwa ishu ambayo tunajua kabisa mwenza wako akila au akiliwa atarudi salama salimini,je nini shida?
Au labda tukibadili mtazamo wetu juu ya jambo hili huenda tutaepuka madhara mengi sana au mimi ndio nina shida kuwa na mtazamo huu?
Nakumbuka kipindi flani miaka ya nyuma girl wangu aliniambia akiwa mkoani huko,""unakuwa na wasiwasi gani kwani hii ni sabuni kwamba itaisha ikitumiwa"" hahaha she was just joking but she had a point kwa kiasi fulani,any way yalikuwa Mastory ya Bey
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.