JamiiForums - Maboresho ya mwaka 2018

JamiiForums - Maboresho ya mwaka 2018

Asante Max.

Mi napendekeza kitu katika uzi, zile reply zenye like nyingi ndizo ziwe zinaonekana za kwanza.

Yani katika uzi, reply zinazo ongoza kwa like ziwe zinajipanga na kuonekana mwanzoni.

Hii itasaidia watu kujenga hoja, majibu kupatikana kwa wepesi, na watu kujikita katika uandishi mzuri.

Unakuta mtu kauliza swali lkn unakuta jibu sahihi lipo #80 , mwanzoni ni masihara matupu.

Sasa huyu wa #80 akifikiiwa watu watampa like na kuonekana wa mwanzoni.

Kiufupi, mpangolio wa reply usiwe kutokana na mtu kawahi, bali hoja zilizopendwa ma watu

Cc Maxence Melo
Asante kwa wazo lako hili, ni Jema.
 
Idumu jamii forum kisiwa cha maarifa. Shukrani za dhati ziwafikie waanzilishi na uongozi mzima wa jamii forum. Bila kuwasahau wadau kwa taarifa, elimu, na maarifa mnayotoa.

Katika kuboresha App yenu itakuwa vyema pia mkiweka sehemu ya jumbe zilizo hifadhiwa (saved messages). Hii ni mahususi kwa mdau atakaye hitaji kufanya rejea, na akiwa nje ya mtandao (Offline).
 
Mbona unaanza kuwa na uwoga
Hili hapa Jibu lako...hopefully Umeelewa!

Its only addictive to us...not him! Just kidding tho !
IMG_20180721_214405_712.JPG
 
Wakuu,

Napenda kutoa taarifa mapema kuwa kutakuwa na maboresho kadhaa ili kutekeleza baadhi ya maombi ya wadau na kurekebisha kasoro kadhaa katika tovuti na app yetu.

Aidha, baada ya utafiti tulioufanya (tunawashukuru wote walioshiriki katika utafiti huu), kuna mengine yataendelea kuongezwa na kuboreshwa ndani ya siku 45 zijazo.

JF inayoonekana na kutumika sasa ilifanyiwa maboresho yaliyotokana na utafiti kwa wadau kati ya mwaka 2012 hadi 2016 ambapo Januari 2016 ilianza kutumika rasmi. Ni hii hii inayoboreshwa zaidi mwaka 2018 ili kuzidi kuifanya JF iwe rahisi kwa wengi kuitumia na kuifurahia.

Yanayotarajiwa:
1) Kuna ambao hawataona utofauti haraka kwani hatujacheza mbali na kilichozoeleka lakini wataona urahisi zaidi wa kuitumia JF
2) Kuna watakaoona baadhi ya vitu vimeondolewa - hivi vitatolewa sababu za kuondolewa kwake na kuoneshwa maboresho yaliyofanywa ili kutopoteza vitu hivyo
3) App: Waliokuwa wakikwama kwa mambo kadha wa kadha - yamerekebishwa kwa kadiri tulivyoweza
4) Mapendekezo ya wadau baada ya JF kufanyiwa maboresho haya yatafanyiwa kazi ndani ya siku hizo hizo 45

Tunawashukuru kwa uvumilivu wenu na kushiriki katika utafiti uliofanywa (nje ya mtandao) ili kuboresha jinsi mnavyoutumia mtandao huu.

Asante
1. Kwenye app likes zinaishia 5 tu kwanini? Embu pigeni hizo codes vizuri bhna

2. Private messages - toeni "subject" inafanya PM kama official email.. Toeni hiyo kitu

3. Kubold, font color etc kwenye app wekeni njia rahisi ya kufanya hivyo vitu sio maswala ya commands kama tunatumia Command prompt

4. Notifications kuna muda zinatokea kuna muda hazitokei
 
Mkuu kitu kingine ni kwamba, kwenye application ya jamiiforums [HASHTAG]#like[/HASHTAG] zinakuwa mwisho 5 wakati jf kwa njia ya browser zinaonekana kulingana na idadi ya watu waliolike.

Naamini hili ni jambo linaloonekana kwa kila mtumiaji wa application ya JamiiForums
 
Shukran mkuu, nafurahi nimepata nafasi moja kwa moja kutalk na boss, THREAD HUWA ZINAFUTWA NNO MKUU NA BAN ZINATEMBEA KAMA UMEME UKIANGALIA KOSA HULIONI NA WALA HUAMBIWI KOSA,. TUSAIDIE KWA HILI.
 
Hili huwa gumu; jaribio la kuruhusu watu kufanya hivi lilipekea watu kujiita “Mze Mwanakijiji” au “The Bos” na wengine watajiita “kulubulee”.

Tunafanya manually kubadili IDs ili pia kudhibiti wanaotaka kujiita majina yaliyo nje ya maadili
Sijakuelewa hapa
 
Kwakuwa bado tu wachache hapa jamvini hii ilisumbua kiasi chake watu kuigiliziana username. Mkuu atuwekee masharti kubadili kila baada ya Miezi 6 na Id zote ulizotumia zionekane kwenye profile yako kwa lazima. Tukiongezeka wapunguze masharti Labda.
"Nawaza tu"
Mimi na #Jf.
Wazo zuri... Majina ya iD ya mtu yote yaonekane
 
Back
Top Bottom