JamiiForums - Maboresho ya mwaka 2018

JamiiForums - Maboresho ya mwaka 2018

Baada ya maboresho ya leo Nimekua sipati alerts za watched contents kwa njia ya email
 
Mm bado nasisitiza kuhusu notification. Ili suala bado halipo sawa. MSg inaweza ingia hata usielewe au mtu anaweza Quote au action yoyote. Tunahitaji powerful notification hasa kwenye Msg na Quote maana mdo Action Kubwa sana JF.
 
Nichukue fursa hii kuwashukuru wote kwa uvumilivu.

Tunaomba radhi kwa kupitisha muda, posts za JF ni nyingi na hatua ya kuzipitia upya ilikuwa ndefu.

Kwa sasa emojis zote ziko supported na mengine mengi.

Kuna vitu tunaendelea kuvirekebisha; ndani ya saa 48 zijazo mapendekezo yenu yatafanyiwa kazi.

Asante

Mkuu, kwanza kabisa hongera pamoja na timu yote yaliyoseviwa JF kwa kazi nzuri ya maboresho mliyoifanya. Inapendeza sana.

Well, kwa maboresho yote mliyoyafanya naona yapo sawa ila tunaomba mrudishe muda na siku husika mtu aliyo-post thread/comment kuepusha kufukua makaburi na pia kujua mada husika iliwekwa siku gani au comment ilichangiwa dakika/masaa mangapi yamepita.

Ahsante sana.
 
Mm bado nasisitiza kuhusu notification. Ili suala bado halipo sawa. MSg inaweza ingia hata usielewe au mtu anaweza Quote au action yoyote. Tunahitaji powerful notification hasa kwenye Msg na Quote maana mdo Action Kubwa sana JF.
Naunga mkono hii hoja
 
tunaomba mrudishe muda na siku husika mtu aliyo-post thread/comment kuepusha kufukua makaburi na pia kujua mada husika iliwekwa siku gani au comment ilichangiwa dakika/masaa mangapi yamepita.
Kweli mkuu ni kitu cha muhimu sana umezungumza.
 
Kwa walioshiriki utafiti huu watakuwa walipata kuwajua kwa sura na majina watafiti wetu. Wengine nilihojiana nao mwenyewe

Mngetuhusisha kwenye hiyo reserach labda tungetoa user stories/use cases anuani.

Hata hivyo hongereni kwa hili, kwa wapenda mabadiliko kama mimi tunaiona hii move ni progressive.
 
Wakuu,

Napenda kutoa taarifa mapema kuwa kutakuwa na maboresho kadhaa ili kutekeleza baadhi ya maombi ya wadau na kurekebisha kasoro kadhaa katika tovuti na app yetu.

Aidha, baada ya utafiti tulioufanya (tunawashukuru wote walioshiriki katika utafiti huu), kuna mengine yataendelea kuongezwa na kuboreshwa ndani ya siku 45 zijazo.

JF inayoonekana na kutumika sasa ilifanyiwa maboresho yaliyotokana na utafiti kwa wadau kati ya mwaka 2012 hadi 2016 ambapo Januari 2016 ilianza kutumika rasmi. Ni hii hii inayoboreshwa zaidi mwaka 2018 ili kuzidi kuifanya JF iwe rahisi kwa wengi kuitumia na kuifurahia.

Yanayotarajiwa:
1) Kuna ambao hawataona utofauti haraka kwani hatujacheza mbali na kilichozoeleka lakini wataona urahisi zaidi wa kuitumia JF
2) Kuna watakaoona baadhi ya vitu vimeondolewa - hivi vitatolewa sababu za kuondolewa kwake na kuoneshwa maboresho yaliyofanywa ili kutopoteza vitu hivyo
3) App: Waliokuwa wakikwama kwa mambo kadha wa kadha - yamerekebishwa kwa kadiri tulivyoweza
4) Mapendekezo ya wadau baada ya JF kufanyiwa maboresho haya yatafanyiwa kazi ndani ya siku hizo hizo 45
5) Search itakuwa inaleta matokeo haraka na relevant zaidi
6) Wanaotumia app wataona baadhi ya vitu ambavyo walikuwa wakikwama vikiwa vimetatuliwa
7) Emoji nyingi zitakuwa rahisi kutumiwa na yeyote (ziko supported)
8) JF itaanza kufunguka kwa kasi zaidi ya awali

Tunawashukuru kwa uvumilivu wenu na kushiriki katika utafiti uliofanywa (nje ya mtandao) ili kuboresha jinsi mnavyoutumia mtandao huu.

Asante
Muda (saa na tarehe) ambao mtu anacomment ingependeza viwepo.
 
Back
Top Bottom