Jamii imempora mwanamke nafasi yake

Hujasema kweli. Muda wa kazi unaisha saa tisa, je kazi hiyo unaifanyia nyumba ya pili? Je, watoto wote wanarudi saa 9 nyumbani? Je, majukumu ya kazi yatakuacha siku zote utoke saa tisa, usisafiri kikazi n.k?

Kwa hiyo unapinga mtoto kuwa karibu na mama zaidi? Unapinga hili?
 
As far as gender matters are concerned ;there's no turning back

Men simply have to brace for impact[emoji28][emoji28]
Not a laughing matter bt hamna namnaa
Wanawake ndio wana feel nock on effect. Wanazalishwa na kuachwa. Wanatumika na kuchoshww kisha siku zao zikipita wanaandamana kwenda kwa RC. Wananung'unika siku hizi wanaume hawaoi, wanawachomachoma tu na kuwaacha.

Godly women will always be the happiest on planet earth!!
 
Hao unaosema hawa exist wapo sana tu, God fearing women waliotunza asili yao. Nami nikuambie tu I have a happy marriage contrary to what you wish. Mtoto katika miaka yake ya awali atahusiana na mama zaidi kwa sababu ana muda naye mwingi hata baada ya kumwachisha ziwa. Kijana wa kiume akikua huambatana na baba yake zaidi lakini pia atakuwa na muda na mama yake, ndivyo ilivyo kwa mtoto wa kike kwa mama.

Social skills zinakuwa imparted hivyo, kila mzazi ana nafasi yake kwa wakati wake. Sisi tuliolelewa kwenye maisha hayo unayoyakashifu tuna amani sana kuliko hiki kizazi cha nyoka, kinachokidai kuzibuka lakini wanaishia kunasa kwenye tundu bovu.

Na kama unaamini mwanamume ndiye mwenye kuumia kwenye huu upuuzi, basi kweli haimo ndani yako. Hayuko mwanamume aliyekwenda kutafuta dawa ya kupata mke, ama kwenye nyumba za ibada, ama kwa waganga. Waganga wa jadi wamezidi kuwa wengi kwa sababu ya wanawake kuhitaji huduma, hawana amani tena. Bisha na hili
 

Kama kila mtu atasimama na kuitambua nafasi yake kwenye jamii hamna wazo wala fikra za utumwa kwenye ndoa hilijambo lazima watu walione.
 
Dada Nadhani ume interpret hii topic kwa jinsi unavyotaka wewe na sio kwa jinsi muandishi alivyo iwasilisha.

Hakuna mahali panaposema kwamba mwanamke hatakiwi kupata fursa ya elimu wala kufanya kazi kwani hizo ni haki za msingi ya kila mtu, na kujaribu kwa namna yoyote kuzuia mwanamke asipate haki hizi ni kosa la uvunjanji wa haki za binadamu.

Unachopaswa kuelewa hapa ni kwamba kinachopigiwa kelele ni namna elimu inavyotumika ambavyo ni kinyume na makusudio yake. Elimu anayopewa mwanamke leo hii imekuwa twisted kiasi kwamba ina mpotosha zaidi kuliko kumjenga.

Imagine kuna mwenzako hapa anasema eti amesoma hili asiwe mtumwa na utumwa wenyewe ni kuwa tegemezi. Sasa huyo kweli kaelimika au kapotoshwa?

Kwamba ukiwa tegemezi basi wewe ni mtumwa, hivi hii ndio maana sahihi ya utumwa kweli?

Hii elimu inayoitwa "ukombozi wa mwanamke" ina dosari kubwa mno na imewameza wengi. Kwanza inamuaminisha akishakuwa na uhuru wa kiuchumi basi mwanaume kwake ni kitu cha ziada tu na hivyo anaweza akaishi kama mwanaume na yeye.

Tunafahamu kuwa na maarifa ni kitu kizuri, lakini maarifa hayo yasiwe nyenzo ya mashindano yasiyokuwa na tija. Na kwa bahati mbaya sana wengi wameangukia kwenye hili kundi.

Dunia imebadilika ndio lakini mabadiliko hayo faida zake ziko outweighed na hasara na kwenu nyie walengwa sio rahisi kuliona hili sana sana mtaona mko mahali pazuri.
 
Mbona unataja wanawake wenye shida tu ?
Hamna wanaume wenye shida?

Na hamna wanawake wanaofurahia maisha simply bcz wamejiendeleza kwa namna flani?.

Naona una bias flani hivii
Mwanaume kutokuoa sio hoja he also remains single like the woman..
Na siku akioa ataoa mwanamke na si mwanaume mwenzake..ts even..ndoa ya wawili jmn..y u feel women always loose and men always win?..reality haiko hivo

If Godly women were only the happiest wasingekimbilia upepo wa kisulisuli vile😅
 
Its twisted simply because men twisted it first

It used to be kisa mwanaume ana elimu na pesa mwanamke utaisoma namba..utanyanyasika mana jamaa anakupangia anavotaka yeye smtimes bila kujali how you feel...japo sio wote ila baadhi
Ss sikuhz women have that pia naona ndo mana wanaume mnateseka...

Afterall si wanawake wote wanatumia elimu zao vibaya..jifunzeni kuchagua tu vizuri
 
Hili linapaswa kuwa mjadala wa kitaifa na hizi taasisi za kimataifa zinazotetea huwa zinafanya hivi kwa maslahi ya nani?

Amini usiamini ni kwa maslai yao,kwani wanajua misingi yote ipo ndani ya familia na kama wakifanikiwa kuharibu huo msingi maadili hayatakuepo na watao athirika hapa ni watoto.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]kiazi mbatata wee ....navyompenda Mama yangu, na ninvyosimaam kwa ajili ya mama yangu..

Niwe nmekosa nn?? Hihihi kaone ,kapanya weee
Amekugusa sehemu husika?mbona umecatch feelings ss?.

Tujaribu kuja na walau hoja na si maneno ya kejeli/matusi
 
Hakika sio wote na ndio maana mada imeletwa mezani ili tujifunze na kukumbushana masuala haya muhimu kabisa kwani kupotoka huku ndio kunakopelekea kuzalishwa kwa taifa dhaifu lisilo na dira.
Huwa nasikitika sana kwa aina fulana ya malezi hasa yatolewa na baadhi ya akina Mama wanao ona wamejitosheleza(wenyewe wanadai hawataki kutawaliwa)na kulea mtoto kwa aina fulana ya taratibu za Hollywood basi mtoto hakanywi wala kuhojiwa kwa lolote yeye junior atafanya atakalo hata kama ni upuuzi.
Sasa hoja kama hizi zisipopenyezwa na jamii kutambua athari zake kwa kizazi cha kesho basi lazima tuamini na kufahamu kuwa kama taifa tutashindwa pakubwa
 
Haha mbona mnaumia sana mwanamke kumuona mwanaume kama kitu cha ziada?.

Hio ndo mentality ya baadhi ya wanaume..imeanzia upande wa kiumeni...
Mwanaume anaona mwanamke ni chombo cha starehe, asiestahili kupiga hatua ktk yale anayopenda maishani na vitu vingine km hivyo ambavyo si vizuri kwa binadamu yoyote
 
topic za Lizarazu , Nyenyere , Carlos The Jackal , Jokajeusi wote hawa hawajui upendo wa mama..mnajihangaisha bure..lol. ……………..
Naona unanijua sana mimi na familia yangu wewe dada.

Ila nikwambie tu mama yangu sio mwanamke wa cancerous generation of women ambao na wewe ni mmoja wao.

Mama yangu ni mwanamke anayefahamu nafasi yake kifamilia na kijamii kwa ujumla na wala hapana shaka juu ya hilo.

Mama yangu sio mwanamke anaendekeza mashindano yasiokuwa na tija ambayo hayana mwisho mzuri.

Mama yangu sio mwanamke aliyepumbazwa na tamaduni mpyaa zinazohalalisha kila aina ya upuuzi.

Mama yangu sio muhamasishaji na mbishi anayetete mambo ya kijinga kijinga kisa tu yanafanywa na watu wa jinsia yake.

Mama yangu sio mjinga wa kuona single motherhood ni kitu cha kawaida mpaka kufikia hatua ya kuhamasisha kabisa.

Mama yangu ni mtu mwenye upendo wa dhati kwanzia kwa familia yake mpaka kwa wanajamii wanaomzunguka.

Mama yangu ni mwanamke bora kabisa aliyezaliwa kwenye kizazi bora cha wanawake na hichi ambacho kinaonekana kilichopotea.
 
Kiuhalisia utegemezi siyo utumwa, lakini wanaume wengi ndiyo wamefanya wanawake waamini hivyo.

Kwa sababu kuna wanaume wanaona kama kuwahudumia wake zao ni kuwafanyia favour, kwahiyo wana haki ya kuwapiga na kuwanyanyasa wake zao vyovyote wanavyojisikia kwa sababu wanajua kuwa wanawategemea na hawana pa kuenda.

Hata tukiangalia mada nyingi humu za kuhusu uchumba na ndoa utasikia wanaume wengi wakisema "mimi mwanamke niliyemtolea mahari hawezi kunibabaisha", unaweza kuona ni jinsi gani kuna wanaume wanaona kama kutoa mahari ni kuwafanyia favour wanawake na ndiyo maana wanaona kama wana haki miliki za kuwapiga au kuwanyanyasa wake zao wanavyojisikia.

Kwahiyo mimi nadhani wanaume waache kuwa na mitazamo ya ajabu kwamba eti "kufanya kitu fulani ni kumfanyia mwanamke favour hivyo naweza kumfanya chochote ninachojisikia" hii ndiyo inafanya wanawake waone kama kuwa wategemezi kwa wanaume ni utumwa.
 
Exceptions are okay..ndio maisha
Muhimu wazazi kutengeneza muda zaidi kuwa karibu na kuweka mazingira salama ya mtoto na kumfuatilia kadri utakavyoweza anapokua

miezi 4 ya mwanzo u can stay full time na mtoto kwa waajiriwa...kwa wafanyabiashara hata mwaka..
Then unaenda kazini masaa machache for 6 months zinazofuata by miezi 10 hadi mwaka mtoto kafika mbali sana
Mda unakua nao mzuri tu kumfuatilia
Mama ajipange namna ya kuwaattend watoto
They grow and they grow fast..

U cant be around your child 24/7 no matter how much you love them..but you can create comfort and security hata kama haupo

Ukifa mtoto hatoishi kwani?..
 
Mbona unataja wanawake wenye shida tu ?
Hamna wanaume wenye shida?

Nataja walio wengi, exception cases zipo ila majority.

Na hamna wanawake wanaofurahia maisha simply bcz wamejiendeleza kwa namna flani?.

Nimepata kuzungumz na wanawake wengi waliohesabika kufanikiwa, wote walonyesha kuumizwa na kutokuwa na ndoà. Mfano mwingine ni Sophia Simba aliwahi kuhojiwa live kwenye TV na alikiri hayo. Wanawake waliojiendeleza na wakawa na ndoa imara wana furaha kuliko waliojiendeleza na kubaki kudanga mitaani. Kuna tofauti kati ya mwanamke mwenye ndoa na asiye na ndoa, hata heshima yao ni tofauti, huo ndio ukweli.

Naona una bias flani hivii
Mwanaume kutokuoa sio hoja he also remains single like the woman..
Na siku akioa ataoa mwanamke na si mwanaume mwenzake..ts even..ndoa ya wawili jmn..y u feel women always loose and men always win?..reality haiko hivo

Sina bias, nayatazama maisha katika uhalisia. Mwanamume akiamua kuoa anaoa, mwanamke akiamua kuolewa anasuniri ampate mwanamume, the difference is clear. Wote wakishatumikia anasa wakaamua kuingia kwenye ndoa, mwanamke atategemea bahati wakati mwanamume atachagua amtakaye. Nimekosea wapi hapo?
If Godly women were only the happiest wasingekimbilia upepo wa kisulisuli vile[emoji28]

Kukimbilia upepo w kisulisuli sio kipimo cha godly women. Mwanamke mcha Mungu hawezi kuwemo kwenye kundi lile la wanawake walio desperate. Huyu hufichwa katika Bwana na mwanamume amwonaye ni yule aliye sahihi tu, that is the Bible. Uliowaona hapo ni wale waliokwenda kanisani kutafuta muujiza wa ndoa.
 
Hongera kwa mama ni mfano wa kuigwa
Ila umepanic
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…