James Mbatia kumtuhumu Rais Magufuli kwa Ukanda: Anamlinganisha na nani?

Mgambilwa ni mntu

JF-Expert Member
May 30, 2017
2,869
3,188
Wiki hii wakati wa Mjadala wa Bajeti ya Maliasili na Utalii, Mbunge wa Vunjo, mkoani Kilimanjaro, James Mbatia, ambaye ni Waziri Kivuli wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, alimtuhumu Rais John Pombe Magufuli kwa tamko lake kuwa, "Watu wa Kaskazini wasubiri kwanza."

Katika kujenga arguments zake, Mbatia alijaribu kuonyesha jinsi kodi zilivyo nyingi katika sekta ya utalii (57) na kwamba fedha za utalii zinazorudi kwa wananchi wanaoishi maeneo ya kitalii ni ndogo na siyo 7% iliyopo kisheria. Mbatia alisifia juu ya mapato makubwa ya utalii kwenye TANAPA yatokanayo na Hifadhi tano zilizoko Kaskazini - Kilimanjaro, Manyara, Tarangire, Ngorongoro na Serengeti.

Hakutaja maeneo mengine ya kiutalii ndani ya Nchi bali alitetea na kusifia ubora wa Ukanda wa Kaskazini kiutalii. Bahati mbaya hakumpa Rais Magufuli, the benefit of doubt, ukizingatia kuwa, Rais aliyasema hayo akiwa katika Ukanda wa pili kwa Utalii nchini - Iringa.

Kwa kuwa, CHADEMA ndio wamekuwa mstari wa mbele kumuita Rais Magufuli kuwa anapendelea watu wa Kanda ya Ziwa, nimelazimika kufuatilia Wizara Kivuli 18 za Kambi ya Upinzani Bungeni kuona jinsi Wabunge kutoka Kanda zote nchini wamezigawana. Majibu yalikuwa ifuatavyo:
  • Kanda ya Kaskazini - 15, ambapo Wenyeviti wa Kamati wana Wizara - 08.
  • Kanda ya Ziwa - 07, ambapo Wenyeviti wa Kamati ni - 03.
  • Nyanda za Juu Kusini - 05, Wenyeviti wa Kamati ni - 02.
  • Kanda ya Mashariki - 04, Wenyeviti wa Kamati - 00.
  • Kanda ya Zanzibar - 02, Wenyeviti wa Kamati - 02
  • Kanda ya Kati - 01, Wenyeviti wa Kamati - 01.
  • Kanda ya Kusini - 01, Wenyeviti wa Kamati - 00.
  • Kanda ya Magharibi - 01. Mwenyekiti wa Kamati - 01.
Ndipo hapo nimekuwa najiuliza: Hivi Magufuli kuitwa mukanda, mudini na mukabila, wanamlinganisha dhidi ya nani?

 
Jambo unalolijua baya na kisha wewe ukamfanyia mwenzio, au ukaliona likifanywa kwa watu fulani na wewe kukaa kimya ukiona halikuhusu, kudra ya Mungu ni kuja kufanyiwa wewe jambo kama hilo.

Mlipoweka mfumo wenu usio rasmi wa kuwatenga watu wa kusini, pwani na "wavaa vipedo", mkadhani Mungu alikuwa usingizini? Kuleni tu faida ya mlichokipanda.
 
  • Kanda ya Kaskazini - 15, ambapo Wenyeviti wa Kamati wana Wizara - 08.
  • Kanda ya Ziwa - 07, ambapo Wenyeviti wa Kamati ni - 03.
  • Nyanda za Juu Kusini - 05, Wenyeviti wa Kamati ni - 02.
  • Kanda ya Mashariki - 04, Wenyeviti wa Kamati - 00.
  • Kanda ya Zanzibar - 02, Wenyeviti wa Kamati - 02
  • Kanda ya Kati - 01, Wenyeviti wa Kamati - 01.
  • Kanda ya Kusini - 01, Wenyeviti wa Kamati - 00.
  • Kanda ya Magharibi - 01. Mwenyekiti wa Kamati - 01.

Naona ungefanya vyema kuja na baraza la mawaziri Magufuli kwenye mchanganuo kama huo hapo juu ili tujiridhishe kama sio/ni mkabila/mkanda
 
Watu wawili wakiwa wanatembea barabarani mmojawapo yupo nyumba kilometa 2, na safari walianza pamoja, kama unataka wafike wakati mmoja kituo chao cha mwisho inabidi yule aliyeko nyuma aongeze kasi na juhudi kumfikia yule wa mbele na si kumsimamisha yule aliyeko mbele ili wa nyuma amfikie
 
Angalia hizo takwimu vizuri. Licha ya Kaskazini kuwa na jumla ya Wabunge 15 pekee, imeingiza kwenye Kamati Wabunge 13, huku kati yao wanane (08) wakipewa uenyekiti. But Kanda ya Ziwa yenye Wabunge Saba (07) licha ya kuingiza sita, imeambulia unaibu zaidi licha ya kuwa na Wabunge wachache.
 
Kwenye suala la udini: Katika jumla ya Wabunge 34 wa CHADEMA, ni Mbunge mmoja pekee ambaye ni muislamu.

Sasa, mjiulize ilikuwaje watu wa aina moja tu ndio wakaaminika na kuteuliwa na Chama hicho? Kama wa Imani nyingine walikuwa wanashindwa kwenye chaguzi, kwa nini hiyo ilitokea? Hapa tatizo lilikuwa la CHADEMA ama wananchi?

Tofautisheni na CCM ambayo ina Wabunge wa kuchaguliwa wanataka 70 wa kikristu na 50 wa kiislamu.
 
Back
Top Bottom