Wasakatonge, wameona nafasi zao CCM ni finyu wanatafuta pa kutokea
Hatuta pokea makapi kutoka CCM-dr slaa
Huogopi kuwa mmbea mbona wiki iliyopita bulaya kachukua fomu kugombea ubunge jimbo la bunda au unazungumzia esther yule dada yako?Mbunge wa jimbo la Kahama ndugu James Lembeli (CCM) amewaeleza bayana viongozi wa CCM wilaya ya Kahama kuwa hana hamu tena na hataki kuisikia CCM.
James Lembeli hata hivyo hajabainisha rasmi mustakabali wake mpya wa kisiasa ingawa habari zilizozagaa mjini Kahama ni kuwa mbunge huyo aliyemaliza muda wake yupo mbioni kutimkia Chadema.
Aidha katika hatua nyingine, mbunge wa viti maalum CCM ndugu Esta Bulaya naye amesema wazi kuwa hana tena mpango wa kuendelea kubaki CCM.
Mbunge huyo machachari bado hajadokeza chama atakachohamia na/au kuachana na siasa na hakuna uvumi wowote unaomhusu ulioenea au kuenezwa mpaka sasa.
Bulaya na Lembei,Kunjombe wamekuwa wakweli tanga zamani kama ulikuwa unafutilia kwa miaka mitano iliyopita utakubaliana na Mimi walikuwa kama NI WABUNGE WA UPINZANI HATA KTK BUNGE LA KATIBA WALIONYESHA UKOMAVU MKUBWA KWA KUUNGA MKONO SERIKALI TATU NA KURA ZA SIRI.
Taarifa ambazo zimepatikana baadaye zinasema, Lembeli anatarajiwa kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), muda wowote kutoka sasa.
Aidha, wabunge wengine wa CCM majina tunayo, wanatarajiwa kujiunga na chama hicho na kugombea ubunge katika majimbo mbalimbali nchini
CHANZO; MWANAHALISI ONLINE
Ester akihama CCM ni pigo kubwa