James Lembeli, Esta Bulaya: Hatuitaki tena CCM

James Lembeli, Esta Bulaya: Hatuitaki tena CCM

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
12,416
Reaction score
39,522
Mbunge wa jimbo la Kahama ndugu James Lembeli (CCM) amewaeleza bayana viongozi wa CCM wilaya ya Kahama kuwa hana hamu tena na hataki kuisikia CCM.

James Lembeli hata hivyo hajabainisha rasmi mustakabali wake mpya wa kisiasa ingawa habari zilizozagaa mjini Kahama ni kuwa mbunge huyo aliyemaliza muda wake yupo mbioni kutimkia Chadema.

Aidha katika hatua nyingine, mbunge wa viti maalum CCM ndugu Esta Bulaya naye amesema wazi kuwa hana tena mpango wa kuendelea kubaki CCM.

Mbunge huyo machachari bado hajadokeza chama atakachohamia na/au kuachana na siasa na hakuna uvumi wowote unaomhusu ulioenea au kuenezwa mpaka sasa.
 
Taarifa ambazo zimepatikana baadaye zinasema, Lembeli anatarajiwa kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), muda wowote kutoka sasa.
Aidha, wabunge wengine wa CCM majina tunayo, wanatarajiwa kujiunga na chama hicho na kugombea ubunge katika majimbo mbalimbali nchini
CHANZO; MWANAHALISI ONLINE
 
Karibuni Sana majembe. Chadema chama cha wapenda Haki. Mungu awabariki sana
 
Waje wasaidie kupiga kampeni.
Hawana nafasi ya kupata nafasi ya uongozi.
 
Wasakatonge, wameona nafasi zao CCM ni finyu wanatafuta pa kutokea

Kwel Tz n ajabu la 8, yan bulaya unamwita msaka tonge? Lember msaka tonge?
Wasaka tonge ni hao waliobak humo kwenye uchafu. CCM na mgombea wao nafananisha na mtu aliyezama kwenye kinyesi anakaribia kufa akaja mtu kwa matumain ya kumuokoa alafu akamuacha juu ya ardh, huyu aliyeokolewa hajiwez akadhan atapata msaada mkubwa kutoka kwa huyo aliyemuokoa kwasababu eti amemtoa kwe shimo la kinyesi hvo atakamilisha huduma yote na ktmuacha salama. Hali ikawa tofauti muokoaji akamwacha bila kumpa huduma we unadhan hapo nzi hawatamfuata, na maradhi hayata mfuata? Mwisho wa siku si atakufa tu.
 
Mbunge wa jimbo la Kahama ndugu James Lembeli (CCM) amewaeleza bayana viongozi wa CCM wilaya ya Kahama kuwa hana hamu tena na hataki kuisikia CCM.

James Lembeli hata hivyo hajabainisha rasmi mustakabali wake mpya wa kisiasa ingawa habari zilizozagaa mjini Kahama ni kuwa mbunge huyo aliyemaliza muda wake yupo mbioni kutimkia Chadema.

Aidha katika hatua nyingine, mbunge wa viti maalum CCM ndugu Esta Bulaya naye amesema wazi kuwa hana tena mpango wa kuendelea kubaki CCM.

Mbunge huyo machachari bado hajadokeza chama atakachohamia na/au kuachana na siasa na hakuna uvumi wowote unaomhusu ulioenea au kuenezwa mpaka sasa.

G Sam leo unahangaika
 
Last edited by a moderator:
Ningetamani pia na watu kama Deo Filikunjombe na Kangi Lugola wachukue uamuzi kama huo. Ninatamani CCM ibakiwe na waropokaji tu kama Lusinde.
 
Waje wasaidie kupiga kampeni.
Hawana nafasi ya kupata nafasi ya uongozi.

Msipowapa uongozi hawaji,ngojeni tu na huko kwenu kutawaka moto tu. Mapesa yoote ya ubunge hayo hamna chama kitabaki salama. Lazima udikteta utumike kuamua mambo,hapo ndio moto utawaka
 
Esther Bulaya akija CHADEMA na akapata ubunge basi Chadema itakuwa imeongeza idadi ya vichwa. Huyo dada namkubali sana ana uwezo wa kujenga hoja japo yupo gambani. karibu CDM
 
Khaa!! Kama unaona mbele giza nafasi zimejaa utafanyaje na siasa ndiyo inakufanya uende WC??
 
. Acheni kushangilia,ni moto huo unakuja kwenu,wako waliosota kwa miaka huko,sasa kama mnahisi kuna neema inakuja halafu ichukuliwe na wengine unadhani patakalika hapo. Msipowapa uongozi hawaji,ngojeni tu na huko kwenu kutawaka moto tu. Mapesa yoote ya ubunge hayo hamna chama kitabaki salama. Lazima udikteta utumike kuamua mambo,hapo ndio moto utawaka
 
Back
Top Bottom