kissa anyigulile
JF-Expert Member
- Apr 21, 2017
- 1,550
- 1,733
Nakumbuka miaka ya 80 kulikuwa na mwalimu mmoja Mcanada alikuwa anafundisha shule moja ya madhehebu ya Wasabato inaitwa Parane Secondary School. Alikuwa anafundisha Chemistry na Physics. Don Straub. Alikuwa mzuri sana katika masomo hayo. Sehemu hiyo inaitwa Mamba Myamba, Upareni.
Kuna kipindi alitembelewa na Baba Mkwe wake toka Canada ambaye amebobea katika mambo ya madini.
Alilizunguka like eneo karibu wiki nzima, akampa taarifa fulani Mkwe wake, naye hakusita kuiweka hadharani.
Taarifa ni kwamba eneo lote lile linsalozunguka shule ile kuna wingi mno wa madini ya dhahabu, kiasi kwamba ukichukua muda na kufuatilia mtoni unaweza ukapata dhahabu. Baadae yule mtaalam aliondoka, na pia yule Mwalimu Don Straub akaondoka baada ya kufiwa na mkewe.
Limenijia hili wazo ghafla sijui kwa nini.
Wataalam fanyieni kazi ugunduzi huu.
Kuna kipindi alitembelewa na Baba Mkwe wake toka Canada ambaye amebobea katika mambo ya madini.
Alilizunguka like eneo karibu wiki nzima, akampa taarifa fulani Mkwe wake, naye hakusita kuiweka hadharani.
Taarifa ni kwamba eneo lote lile linsalozunguka shule ile kuna wingi mno wa madini ya dhahabu, kiasi kwamba ukichukua muda na kufuatilia mtoni unaweza ukapata dhahabu. Baadae yule mtaalam aliondoka, na pia yule Mwalimu Don Straub akaondoka baada ya kufiwa na mkewe.
Limenijia hili wazo ghafla sijui kwa nini.
Wataalam fanyieni kazi ugunduzi huu.