WomanOfSubstance
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 5,457
- 956
Kabla sijasema ninachokikusudia, naomba niwatakeni radhi kwa vile inaweza kuwagusa baadhi ya wana JF moja kwa moja.Siyo kusudio langu kumuudhi mtu lakini kiungwana unapoona jambo na likakusumbua basi ni vema ukaliweka wazi.
Baada ya kuwatakeni radhi naomba niseme: Kwanini mara kwa mara tunaona wana jamvi wakiteka nyara thread na kuanza kuchomekea hoja ambazo hazina uhusiano? Mfano watu wanazungumzia jambo zito jukwaa la siasa au jamii intelligence, unashtukia hoja imeshapotoshwa na kuanza kuonekana ina ladha au harufu ya udini au mapenzi!
Asanteni kwa kunisoma na samahani kwa nitakayemkwaza kwa namna yoyote ile.Ukiona nimekukera basi badala ya kunizodoa hapa, tukutane kwenye jukwaa la chit chat tupige gumzo vizuri.
WAKATABAHU!
WoS
Baada ya kuwatakeni radhi naomba niseme: Kwanini mara kwa mara tunaona wana jamvi wakiteka nyara thread na kuanza kuchomekea hoja ambazo hazina uhusiano? Mfano watu wanazungumzia jambo zito jukwaa la siasa au jamii intelligence, unashtukia hoja imeshapotoshwa na kuanza kuonekana ina ladha au harufu ya udini au mapenzi!
- Kwanini wahusika wasiache tu kuchangia badala ya kupotosha mtiririko wa mada?
- Kwanini wahusika wasihamie jukwaa la dini kulumbana kuhusu dini zao?
- Kwanini wahusika hawahamii MMU pale wanapojisikia wanataka kuambizana mambo matamu matamu?
- Au basi kwanini tusiwashukuru Mods kwa kuanzisha jukwa la chit chat na tukalitumia vilivyo pale tunapokutana na wapendwa wetu ndani ya majukwaa mengine tukaambizana tutoke chemba tukutana CHIT CHAT ili tuendeleze gumzo la nini kilijiri baaya ya kuachana jana yake kwenye viti virefu au kwenye nyama-choma?
Asanteni kwa kunisoma na samahani kwa nitakayemkwaza kwa namna yoyote ile.Ukiona nimekukera basi badala ya kunizodoa hapa, tukutane kwenye jukwaa la chit chat tupige gumzo vizuri.
WAKATABAHU!
WoS